Header Ads

MAWAKILI WAMBANA SHAHIDI WA EPA

Na Happiness Katabazi
SHAHIDI wa pili katika kesi ya wizi wa sh milioni 207 fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), inayomkabili Rajab Maranda na wenzake wanne, Emmauel Boaz, ameiambia Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kwamba alikuwa ni miongoni mwa waliousika kutoa maelekezo ya kampuni ya Rashaz inayodaiwa kuiba fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ilipwe fedha hizo.


Boaz ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Fedha za Kigeni(BoT) aliyasema hayo jana wakati alipobanwa na maswali kwa nyakati tofauti na jopo la mawakili wa utetezi Majura Magafu, Mpare Mpoki, Mabere Marando na Ademba Agomba kwani jana ilikuwa ni upande wa utetezi kumhoji shahidi huyo,mbele ya jopo la mahakimu wakazi Ignas Kitusi, John Utamwa na Eva Nkya.

Yafuatayo ni mahojioano kati ya mawakili hao na shahidi huyo kwa nyakati tofauti:
Swali:Pale Benki Kuu nani alikuwa anakaa na data base ya madeni?
Jibu:Sijui.
Swali:Kwa wewe ujui kama deni hilo lilikuwepo au la?
Jibu:Sijui.
Swali:Sasa ni kwanini ulikuwa miongoni mwa viongozi wa BoT mlioidhinisha malipo kwa kampuni hiyo wakati hata kuona data base?
Jibu:Mimi niliegemea katika idhini ya Gavana Daud Balali ambaye ndiye aliyeidhinisha kampuni hiyo iliopwe.
Swali:Wewe , Peter Noni, Isangya ,na Mkurugenzi wa uchumi na sera Benki Kuu, Kilato,kabla ya kesi za EPA kufunguliwa mliohijiwa je mlitoa maelezo kama haya unayotoa leo mahakamani ?
Jibu:Ndiyo.
Swali:Boaz kwa cheo chako hukuwai kupata nafasi kuwa na data base ya malipo ya EPA?
Jibu:Ndiyo sijawahi kupata nafasi ya kuiona.
Swali:Wewe ni mtaalamu wa masuala ya fedha kwa taaluma yako hiyo ,huwezi kuizinisha malipo bila kuwa na data base sasa ieleze mahakama ni kwanini uliidhinisha malipo bila ya kuona data base?
Jibu:Kimya.
Swali:Wewe ni msomi mwenye CPA na shahada mbili ni kwanini ulitoa maelekezo ya malipo na ukashindwa kumshauri kitaalamu gavana asilipe deni hilo?
Jibu:Naweza kumshauri Gavana siyo kumkataza.
Swali:Wewe ,Peter Noni ambaye sasa ni Mkurugenzi wa Benki ya TIB , Isanga mliohojiwa lakini hamjashitakiwa,ni kweli?
Jibu:Kimya.
Swali:Shahidi pamoja na usomi wako huo ,kabla ya kuelekeza deni lilipwe ulishindwa kubaini kasoro za kimaandishi katika fomu za maombi ya kulipwa deni?
Jibu:Sikuona.
Swali:Uliwahi kuona deed of assignment(hati ya kuamisha deni)?
Jibu:Sikuwahi kuona.
Swali:Ebu iambie mahakama hiyo shahada yako ya pili ulimaliza lini maana sikuelewi ?
Jibu:2005
Swali:Wewe na mshitakiwa wa nne(Esta Komu)wote ni kaimu wakurugenzi wa vitengo mkipewa maelekezo na Gavana mlikuwa mkiyapinga?
Jibu:Hapana,tuna tekeleza.
Swali;Sasa ni kwanini Komu, Mwakosya na Kimela ndiyo wameshitakiwa na siyo wewe na Peter Noni?
Jibu:Kimya.
Swali:Kwanini Gavana aliidhinisha deni la fedha za India milioni 8 zilipwe kwa dola za kimarekani milioni 1.2 wakati alikuwa akijua sh moja ya India ni sawa n ash 30 ya Tanzania na dola moja ya marekani ni sh 110 ya hapa nchini?
Jibu:Sijui.
Swali:Ieleze mahakama ni watu wangapi Benki Kuu walihusika kuidhinisha malipo hayo kwenda Rashaz (T)Ltd?
Jibu:Gavana.
Swali:Wengine ni wakinanani?
Jibu:Kimya.
Swali:Wewe ulihusika?
Jibu:Ndiyo.
Swali:mshitakiwa wa tano Bosco Kimela alihusika?
Jibu:Ndiyo.
Swali:Kaimu Mkurugenzi wa Fedha za Kigeni wakati huo(Peter Noni) alihusika?
Jibu:Ndiyo.
Swali:Yupo kizimbani?
Jibu:Hayupo kizimbani na wala hajashtakiwa.
Swali: Taja upesi mwingine nani alihusika?
Jibu:mshitakiwa wa tatu na wa nne Iman Mkwakosya, Ester Komu,Mkurugenzi wa Uchumi na Sera Issack Kilato na Gavana.
Swali:Kwa mujibu hilo jarada la maombi ya malipo, kuna utata wowote ulijitokeza kabla ya malipo kuidhinishwa?
Jibu:Sikuona tatizo la malipo hayo.
Swali:Nani alikuwa na mamlaka ya mwisho ya malipo yafanyike au yasifanyike?
Jibu:Gavana.
Swali:Na Gavana aliamua au alikuwa analidhika baada ya watu wote maofisa wake ukiwamo wewe ndiyo anaidhinisha malipo yafanyike kweli si kweli?
Jibu:Gavana, alikuwa anategemea ushahuri wa watalaam.
Swali:Wewe unavyojua kuna mtaalamu alimshauri vibaya katika hayo malipo?
Jibu:Siwezi kujua kwasababu lilikuwa linahusu idara nyingine.
Swali:Ni kwanini kabla ya nyie kuidhinisha malipo mlikuwa mkiitaji deed of asigment?
Jibu:Sijui.
Swali:Ni kitu gani kilikufanya uizinishe malipo ya Rashaz (T) Ltd bila kufuata taratibu hizo?
Jibu;Kimya.
Swali:Ulilidhika na maombi ya mwambaji kulipwa deni hilo, naomba ujibu swali hili kwani ni swali jepesi mno?
Jibu:Nililidhika baada ya mchakato wa kulipwa deni hilo kukamilika.
Swali:Wewe kama mtaalamu hata kama gavana angeizinisha na kuona malipo yanakasoro wewe ungekubali?
Jibu:Nisingekubali kuidhinisha.
Swali:Deed of assignment ya Rashaz T Ltd na Rashaz Tanzania ,sasa ni kwanini mlitoa malipo kwenye nyaraka hizo zenye dosari za kimaandishi na je wewe uliwai kubaini dosari hizo?
Jibu: Sijawai kubaini.
Swali:Utakubaliana na mimi watu wote mlioshughulikia malipo ya kampuni hiyo mlikuwa makini?
Jibu:Siwezi kujua wengine ila mimi nilikuwa makini.
Lifuatalo ni swali aliloulizwa shahidi na hakimu mkazi Ignus Kitusi:
Swali:Shahidi, ulikuwa na wajibu wa kujiridhisha taratibu za malipo zinafuatwa kabla ya kulipa kampuni hiyo?
Jibu:Ndiyo.
Baada ya mahojiano hayo kumalizika wakili wa serikali Vitalis Timon aliyekuwa akisaidiana na Fredrick Manyanda na Oswald Tibabyekomya waliwasilisha ombi la kuonyesha ushahidi kwamba jarada halisi la maombi ya malipo ya kampuni hiyo bado linaitajiwa Benki Kuu, na wakaiomba mahakama hiyo isikilize jana ombi hilo bila hata upande wa utetezi kupewa nakala la ombi hilo na kulipitia.

Akitoa uamuzi hukusu ombi hilo la upande wa serikali, hakimu Mkazi Kitusi alisema kwa mujibu wa sheria za kesi za jinai ni lazim a upande wa pili nao upewe nafasi ya kujibu ombi hilo hivyo akatupilia mbali ombi la upande wa mashtaka la kutaka ombi hilo lisikilize na kuutaka upande wa utetezi kuwasilisha majibu ya ombi hilo Jumatatu ijayo na kwamba Septemba 8 mwaka huu, ombi hilo litasikilizwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Septemba 5,2009

No comments:

Powered by Blogger.