Header Ads

CCM YAGEUKA BENDI YA TAARABU?

Na Happiness Katabazi

MALUMBANO yakipuuzi yanayoendelea katika makundi yayohasimiana ndani ya chama cha mapinduzi yanathibitisha maneno ya mwenyekiti wa chama hicho rais Jakaya Kikwete,alipowaambia wananchi kwamba ndani ya ccm kuna makundi yanayochukiana na kuasimiana kiasi kwamba mtu anashindwa kuacha glasi yake ya maji kwa kuhofu uenda akawekewa sumu.


Kile ambacho CCM ilikipanda ndani ya vyama vya upinzani sasa kimewageukia na kinawatafuna sasa.

Hapo zamani ilikuwani shangwe na vigelegele kuwacheka wapinzani na kuwaita ni mabingwa wa mitafaruku lakini ssa CCM leo hii tuwaite ni vingunge wa ufisadi na umbeya au mapaka shume ,manyani au magwiji wa mipasho?

Kile wanachokifanya wabunge wa CCM kwenye Kamati ya Rais Hassan Mwinyi ,ni ukweli wa mambo na uchafu ulio ndani ya chama hicho tawala.Ni sawa na wachawi waliokengeuka wanapoanza kuloga mchana na kuanza kuweweseka na kuwataja watu waliowaua na kuwala nyama.

Habari toka ndani ya kamati hiyo zinatisha na kusikitisha.Lakini tunajua zote zina ukweli.La msingi kwa watanzania ni kujua hawa wote hawafahai kuwa viongozi wetu hivyo tusiwachague tena .

Haijalishi kwamba kundi moja linajitetea na kujikosha mbele za watu lakini ukweli ni kwamba kujikosha huku kunaandaliwa makusudi kwaajili ya uchaguzi mkuu ujao.

Una watu ambao wanataka kutumia mwanya huo na taasisi za umma kujisafisha ili wagombee na kuwa tena wabunge, marais wajao.

Inakuwa kana kwamba nchi hii wameumbiwa wao na hakuna Mtanzania mwingine mwenye sifa za kuongoza isipokuwa wao.Kama mtu alipewa nafasi ya kuongoza akawa fisadi anataka kurudi kufanya nini tena?Hanataka kujakufanya ufisadi kipeuo cha pili?

Ni vizuri na tunamsifu Mwenyekiti wa CCM Rais Kikwete kwa kuunda kamati ya ‘umbeya’ ikiongozwa na mwenyekiti mstaafu wa chama hicho rais mwinyi.

Lakini tukumbuke kwamba kila umbeya una unaupande.Tutakuja kujua huyu Mwinyi yupo kundi lipi nay eye mwenyekiti wa sasa Kikwete yupo kundi lipi.

Kwasababu makundi hayo yanayoendelea kuparulalana na kuvuana nguo adharani huwa yanageuka nyuma kuangalia wapambe waona katika hili hakuna moja ndani ya ccm awe kiongozi mstaafu au aliypo madarakani hauisiki kwa njia moja ama nyingine kwa kashfa zinazozungumziwaaua hazijazungumziwa.

Kwani tumeona na kusikia kashfa zile zile wakati ambapo kashfa mpya zinazaliwa kila siku.kwani kuna usemi usemao mlani mla leo mla jana kala nini.

Kashfa ya Richmond ,ndege ya rais,helkopta za JWTZ,mitambo ya IPTl,mikataba ya migodi,BoT,mifuko ya pesheni,kila moja ya hizo ina Mapapa ambao wapo ndani ya serikali na wengine wamestaafu na watanzania hawatakuja kujua ukweli wake kwasababu wengi walioopo madarakani wana mizizi katika kashfa hizo kwani watuhumiwa wa kashfa hizo ni ndugu zao au maswahiba zao .

Kamati ya ‘umbeya’ inayoongozwa na Mwinyi haina tija kwa taifa wala ccm ukiacha ukweli kwamba inafurahisha ‘manyani’ na kuwakela binadamu.Mtasemana,mtapalulana lakini walioshika nyadhifa wataendelea kuzishikilia ang’oki mtu ng’o na wasiojua watazani ccm itakayoibuka baada ya kmati hiyo kumaliza muda wake itakuwa safi zaidi.

Licha ya udhahidi huu mkubwa ,hakuna dalili kwamba vyama vya upinzani vitajifunza na kuwa na sifa zaidi kuizidi CCm.Inavyoonekana ama ni vishiriki katika ufisadi ama vinakosa nafasi ya kuwa mafisadi.

Madhara ya kuwa na makundi ndani ya vyama, mkundi yenye rangi ya ukabila, udini,tayari yapo katika vyama vikuba vya upizani na hivyo haviwezi kuinyoshea ccm kidole.

Kama kipo chama cha upinzani kitakachojifunza somo la haya yanayotokea ndani ya ccm hivi sasa ,hiyo itakuwa ni neema kubwa kwa taifa letu.

Mungu ibariki Tanzania ,Mungu ibariki Afrika

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Novemba 18, 2009

No comments:

Powered by Blogger.