Header Ads

RUFAA YA BABU SEYA SASA KESHOKUTWA

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Rufani nchini, jana ilishindwa kuanza kusikiliza rufaa ya ya mwanamuziki mahiri wa dansi hapa nchini, Nguza Viking maarufu kwa jina la ‘Babu Seya’ na wanae watatu ilishindwa kuanza kusikilizwa kwasababu pande zote mbili katika kesi hizo hazikuwa tayari kuanza kusikiliza rufaa hiyo.


Mbali na Babu Seya, warufani wengine ni Papii Kocha Nguza,Nguza Mbangu na Francis Nguza ambao wanatatewa wakili wa kujitegemea Mabere Marando.

Jaji Nataria Kimaro,Salum Massati na Mbarouk Mbarouk walisema wanakubaliana na maombi yaliyowasilishwa na mawakili wa pande zote yaliyotaka shauri hilo liairishwe ili waweze kupata muda wa kupitia nakala ya rufaa hiyo.

“Jopo limeyakubali maombi yenu ya kutaka usikilizwaji wa rufaa hii uairishwe ili mpate muda wa kujiandaa, hivyo tunaairisha rufaa hii hadi Desemba 3 mwaka huu, siku hiyo itaanza kusikilizwa” alisema Jaji Nataria Kimaro ambaye ni kiongozi wa jopo la majaji wanasikiliza kesi hiyo.

Hata hivyo ukumbi Na.2 wa Mahakama ya Rufani, jana ulifurika watu waliofika mahakamani hapo kwaajili ya kusikiliza rufaa hiyo ambayo imekuwa ivuta hisia za watu wengi.

Awali kabla ya kuairishwa kesi hiyo wakili wa warufani Marando, aliiambia mahakama kuwa ameajiriwa kuendesha kesi hiyo wiki iliyopita na akabaini kichwa cha habari cha rufaa hicho kimeandikwa rufaa ya jinai Na.59/2009 badala ya kuandikishwa rufaa ya jinai Na.59/2005, hivyo akaomba kichwa hicho cha habari kiafanyiwe marekebisho na isomeke rufaa ya jinai Na.59/2005, ombi ambalo alikupingwa na upande wa mashitaka.

Aidha alieleza mahakama kuwa anatarajia kuongeza sababu nne katika rufaa hiyo na kisha kuziondoa sababu nne kati ya sababu 19 zilizowasilishwa awali na wakili wenzake Hurbet Nyange na kuongeza kuwa amechelewa kuwasilisha sababu hizo mapama kutokana na ukubwa wa nyaraka zilizomo ndani rufaa hiyo.

Akijibu hoja hizo Wakili Mkuu wa Serikali Justus Mulokozi aliambia mahakama kuwa waliopokea nyongeza ya sababu za kukata rufaa Ijumaa wakati muda wa kazi ulikuwa umekwisha hivyo naye akaomba wapewe muda ili waweze kuzipitia kwa kina ili wakati rufaa hiyo ikianza kusikilizwa wawe na majibu ya uhakikika.

Januari 27 mwaka 2005, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Thomas Mihayo alitupilia mbali rufaa yao iliyokuwa ikipinga hukumu iliyotolewa na aliyekuwa Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Addy Lyamuya ambaye aliwatia hatiani kwa makosa yote waliyokuwa wameshitakiwa nayo Juni 25 mwaka 2004.

Waomba rufani hao wanakabiliwa na makosa kumi ya kubaka watoto wa kike wenye umri kati ya miaka sita na nane na makosa mengine 11 ya kulawiti watoto wa kike wenye umri kama huo na kwamba wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya April na Oktoba 2003 eneo la Sinza kwa Remmy, jijini.

Aidha katika kesi hiyo mwalimu wa shule ya Msingi Mashujaa, Sigirinda Ligomboka, alishitakiwa kwa makosa mawili ya kumsaidia Babu Seya kutenda makosa ya kubaka na kulawiti kwa kuwaruhusu baadhi ya watoto hao kutoka madarasani.

Upande wa mashitaka ulileta mashahidi 24, ambao upande wa utetezi ulipinga vikali kutenda makosa hayo na uliita mashahidi nane.Katika hukumu yake Hakimu Lyamuya alitupilia mbali na utetezi wa Babu Seya na wanawe na akawatia hatiani kwa makosa hayo na hivyo kuwafunga kifungo cha maisha gerezani.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Desemba mosi mwaka 2009

No comments:

Powered by Blogger.