Header Ads

KESI YA MRAMBA YAANZA KUUNGURUMA

na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa kwanza katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 11.7 inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na wenzake wawili, Nyero Matihiza (48), ameieleza mahakama kuwa ushauri wake wa kitaalamu alioutoa ulipuuzwa na viongozi wake.


Mbali na Mramba washitakiwa wengine ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafu Gray Mgonja.Wanaotetewa na mawakili wa kujitegemea Hurbet Nyange, Peter Swai, Profesa Leonard Shaidi, Cuthbert Tenga.

Matihiza ambaye alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Sheria na Masuala ya Uchumi katika Wizara ya Nishati na Madini wakati huo ikiongozwa na mshitakiwa wa pili, Daniel Yona, alitoa madai hayo jana mbele ya jopo la mahakimu wakazi John Utamwa, Saul Kinemela na Sam Rumanyika wakati alipokuwa akiongozwa kutoa ushahidi wake na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Fredrick Manyanda na Stanslaus Boniface.

Matihiza alidai kitaalum yeye ni Diolojia alieleza yeye alikuwa mmoja wajumbe wa Kamati iliyopewa jukumu la kuaandaa mchakato wa kutafuta kampuni ya nje itakayokuja nchini kwaajili ya kukagua thamani na kiasi cha dhahabu kinachopatika kwasababu jamii ilikuwa ikitilia shaka takwimu ya dhahabu inayopatikana nchini haina ukweli wowote.

“Kamati yeti ilifanyakazi yake vyema na nilitoa mapendekezo kwa waziri wangu enzi hiyo(Yona)kwamba Kampuni ya Alex Stewart Gorvenment Bussiness Corporation imeshindwa kazi na ilikuwa imelenga kuficha ukweli na pia nikapendekeza kuwa ada ya asilimia 1.9 inayolipwa kampuni hiyo ni kubwa sana na zabuni itangazwe upya.”alidai Matihiza.

Ifuatayo ni mahojiano kati ya wakili wa serikali Manyanda na shahidi huyo.

Wakili:Wakati ukiwa na wadhifa huo, majukumu yako yaliyokuwa yapi?
Shahidi:Kuishauri wizara ya Nishati na Madini katika masuala ya sheria ya madini,uwekezaji katika sekta hiyo na mfumo wa kodi katika eneo hilo.
Wakili:Unajua nini kuhusu Mineral Assayers?
Shahidi:Ni ufuatiliaji wa madini yaliyo katika sampuli tofauti,mfano katika miamba dhahabu inapatikana kiasi gani.
Wakili:Unafahamu nini kuhusu Gold Asseyers Tanzania?
Shahidi: Mwaka 2002 nakumbuka kulikuwa na suala la wasiwasi kwa wananchi,wabunge kwamba makampuni yanayochimba madini yanaficha takwimu za ukweli kwahiyo kwahiyo majibu ya wakaguzi wa madini yalikuwa yakitiliwa wasiwasi.
Wakili:Kwanini kulikuwa na wasiwasi wa takwimu hizo?
Shahidi:Suala la uchimbaji wa madini katika taifa letu lilikuwa ni geni nandiyo maana wananchi walikuwa wanawasiwa kwamba madini yanayopatikana nimengi kuliko takwimu zonazotajwa.Na wizara iliamua kutafuta mkaguzi wa dhahabu ili kujua kitu gani kinaendelea kwenye sekta ya madini na baada ya hapo wizara kwa kushirikiana na BoT walipewa jukumu la kutafuta mkaguzi wa kutafiti dhahabu nchini.Wizara iliunda timu ya watu wanne na mimi nilikuwa mmoja wao ,tukafanyakazi yakuandaa maombi ya kutafuta mkaguzi wa dhahabu.
Wakili:Timu yenu ilitoa mapendekezo gani katika zoezi hilo la utafiti?
Shahidi:Tulipendekeza uwepo mifumo ya usimamizi ya uchimbaji wa madini,kukiaki taarifa za upatikanaji wa dhahabu na tukaweka vigezo kwamba kampuni ya ukaguzi wa madini tunayoitafuta isitokee kwenye nchi ambayo wachimbaji wa hapa nchini wametokea.
Wakili:Ni makampuni yapi mlipata baada ya kutangaza hiyo tenda?
Shahidi:Tulipata makampuni matano ambayo yalijitokeza ila ni kampuni moja ya Alex Stewart Asserys ndiyo ilishinda zabuni.
Wakili:Ni nani hao Alex Stewart Asseys?
Shahidi:Ni kampuni ambayo inafanya shughuli za ukaguzi wa madini Uingereza pia inatawi Marekani Na hiyo kampuni ya marekani ambayo ndiyo ilipewa kazi hapa nchini inaitwa Alex Stewart Government Bussiness Corporation.
Wakili:Alex Stewart Asseys na Alex Stewart Gorvement Bussiness Corporation zinahusiano gani?
Shahidi:Alex Stewart Asseys ni kampuni mama na hiyo nyingine ambayo inadaiwa inafanyakazi na serikali mbalimbali duniani na ndiyo maana serikali yetu ikaitafuta.Na ilitimiza vigezo vingi ila kigezo cha mtaji kilichomtaka alete vifaa(mahabara )hapa nchini kilimshinda na ndiyo maana kamati yetu tukaona hicho ni kikwazo kwetu.
Wakili:Mlifanya nini baadaya kuona haitimizi kigezo hicho?
Shahidi:Sisi kama kamati tulipeleka mapendekezo kwa Gavana marehemu Daudi Balali kwani nyiyo aliyekuwa anatusimamia.Na nimi nilipeleka dokezo kwa aliyekuwa waziri wa Nishati, Yona.
Wakili: Baada ya majadiliano yenu na kampuni hiyo nini kilifuata?
Shahidi:Uliandaliwa mkataba na ofisi ya Gavana.Waandaaji wa mkataba misikushiri ila nilishiriki kutoa mapendekezo.
Wakili;Mapendekezo ya kuikataa kampuni hiyo ya ukaguzi wa dhahabu uliandika lini?
Shahidi:Kabla ya mkataba kusainiwa na mapendekezo yangu niliyatoa wakati draft ya mkataba.
Wakili;Ni mapendekezo gani hayo?
Shahidi:Ada ya asilimia 1.9 kwa kampuni hiyo ilikuwa ni kubwa sana ikataliwe kwasababu taifa linapata mrahaba wa dhahabu wa asimilia 3.Hivyo nasisitiza mapendekezo yangu ya kitaalamu niliyompelekea Yona hakuzingatiwa.
Wakili:Utendaji wa Kampuni ulitakiwa uweje kwa mujibu wa mkataba?
Shahidi:Kuimarisha udhibiti na usimamizi na tulika kampuni hiyo itusaidie lakini haikuweza kutusaidia,eneo jingine ni ambalo utendaji wake haukulidhisha ni eneo la takwimu kwani katika mkataba kampuni hiyo iliaidi kupandisha takwimu za ukaguzi hadi asilimia 50 lakini ilishindwa kutimiza hilo,eneo jingine ni mafunzo kwa wataalum wa nchini ili kampuni hiyo ikimaliza muda wake na kuondoka wataalamu wetu waweze kuendelea.
Wakili:Bajeti ya 2003-2004 malipo ya mkaguzi huyo yalikuwemo?
Shahidi:Halikuwemo.

Kiongozi wa Jopo la mahakimu wakazi John Utamwa, aliairisha kesi hiyo hadi leo ambapo upande wa utetezi utakuja kumhoji shahidi huyo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 3,2009

No comments:

Powered by Blogger.