Header Ads

MEREY BALHABOU AFUTIWA KESI

Na Happiness Katabazi

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Merey Ally Saleh, maarufu kwa jina la Merey Balhabou na mwenzake, Abdallah Said Abdallah, waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya wizi wa dola milioni 1.08 (zaidi ya sh bilioni moja) , wamefutiwa mashitaka.


Washitakiwa hao wamefutiwa mashitaka baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kuwasilisha hati ya kuwafutia mashitaka washitakiwa hao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Merey na mwenzake, wameachiwa huru chini ya kifungu 91(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai, ambacho kinampa mamlaka DPP kuwaondolea mashitaka watuhumiwa.

Kuachiliwa kwa washitakiwa hao kunafanya washitakiwa katika kesi hiyo kwa njia ya mtandao wa kompyuta, mali ya Benki ya Barclays kubaki tisa.

Washitakiwa waliobaki katika kesi hiyo ni Winford Mwang’onda, Shubira Mutungi, Naima Saria, Upendo Mushi, Magreth Longway, Emmanuel Mukoni na Ramadhani Khamis, ambao ni wafanyakazi wa benki hiyo na mfanyabiashara, Justice Rugaibura.

Washitakiwa hao Oktoba 29-30 mwaka jana, walikula njama katika eneo lisilofahamika jijini Dar es Salaam, walifanya udanganyifu na kuiibia benki hiyo fedha hizo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 3,2009

No comments:

Powered by Blogger.