Header Ads

BABU SEYA ALIONEWA-WAKILI

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Rufani nchini, imeombwa kumwachiria huru mrufani mwanamuzi mahiri wa muziki wa dansi nchini,Nguza Viking maarufu kwa jina la ‘Babu Seya’ na wanaye watatu kwani hukumu zilizowatia hatiani zimejaa kubwa za kisheria.


Mbali na Babu Seya, warufani wengine ni Papii Kocha Nguza,Nguza Mbangu na Francis Nguza ambao wanatatewa wakili wa kujitegemea Mabere Marando na Hamidu Mbwezeleni toka Zanzibar.

Sambamba na hilo pia wakili wa warufani, Mabere Marando na Hamidu Mbwezeleni wamedai kuwa kesi hiyo ni ya kupangwa na kwamba hawajawahi kuona hukumu ya ovyo ya aina hiyo tangu waanze kufanyakazi ya uawakili kwa zaidi ya miaka 30 sasa.

Ombi hilo lilitolewa jana mawakili hao wawarufani wakati wakiwasilisha sababu nne za kupinga rufaa ya Mahakama Kuu iliyotolewa na Jaji mstaafu, Thomas Mihayo na hukumu ilioyotolewa na Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Addy Lyamuya, ambao wote walitia hatia washitakiwa kwa makosa ya kujamiana na hivyo kuwafunga kifungo cha maisha jela.

Mawakili hao wa utetezi ambao walianza kuwasilisha sababu hizo tangu saa 3:38 asubuhi hadi saa 7:27 mchana, mbele ya jopo la majaji watatu linaloongozwa Jaji Nataria Kimaro, Salum Massati na Mbarouk Mbarouk, huku mamia ya wananchi wakiwemo raia wa nchi ya Kongo wakifurika ndani na nje ya mahakama hiyo kwaajili ya kufuatilia kesi hiyo ambayo inavuta hisia za watu wengi na huku wananchi wengine wakati Marando akiwasilisha hoja zake wengine walikuwa wakibubujikwa machozi kwa uchungu.

Marando alianza kwa kueleza mahakama kuwa sababu ya kwanza, pili, tatu,tano,sita,saba,nane, 11,14 na 15 ambazo zinasomeka kwenye hati ya rufaa yao ameamua kuziacha na kwamba anatawasilisha sababu ya tisa ambayo inahusu mahojiano ya awali ya shahidi ambaye ni mtoto mdogo kama ilivyoeleza na katika rufaa ya Jaji Mihayo jinsi Lyamuya alivyowahoji mashahidi ambao ni watoto wadogo katika kesi hiyo.

Marando anachambua kuwa mstari wa 7-9 ukurasa wa 645 katika rufaa ya Mahakama Kuu, Jaji Mihayo anasema “Hakimu Lyamuya alitumia utaratibu wenye makosa na hatimaye alimalizia kwakusema kwamba hakimu huyo kwamba ‘kisheria na ukweli hakufanya mahojiano kihalali na hao watoto(mashahidi) kabla ya watoto hao kuanza kutoa ushahidi wao”;

Akadai kuwa lakini mwishowe katika ukurasa wa 647 mstari wa 25-27 Jaji Mihayo anasema pamoja na makosa hayo ushahidi ulitolewa na mashahidi hao unakubalika.

“Washimiwa na majaji wa mahakama ya rufani sisi tunasema jaji na hakimu huyo kwakusema hayo hakitaka hukumu zao walikosea kisheria kwani sheria inaitaka mahakama kabla haijaanza kuchukua ushahidi wa mtoto ni lazima ijiridhishe mtoto huyo anaakili timamu na anaelewa maana ya kiapo na kisha irekodi hayo kwenye jarada la kesi lakini Hakimu Lyamuya hakufanya hivyo wala kuandika rekodi ya hayo”alida Marando.

Marando akiwalisha sababu hizo kwa kujiamini alidai kuwa kwa makosa hayo ya kisheria yaliyofanywa na hakimu na Lyamuya huyo hadi wakafikia uamuzi wa kufunga kifungo cha maisha warufani, ni wazi kabisa walikuwa wanapinga na sheria za nchi na maamuzi yaliyotolewa na majaji wa mahakama za hapa nchini kwenye kesi mbalimbali , ambazo alizitumia jana kusapoti hoja zake.

“Mashahhidi 10 ambao ni watoto wadogo wenye umri kati ya miaka 6-8 ambapo upande wa mashitaka ulidai ndiyo walibakwa na kulawitiwa na warufani,walipofika mahakama ya Kisutu kutoa ushahidi wao hawakuhojiwa na wala mahakama aikujiridhisha kama wana akili timamu kwasababu hiyo tunasema kwamba ushahidi wa watoto hao ni batili na tunaliomba jopo lenu lisiukubali”alidai Marando.

Alionyesha ukurasa 661 ukurasa wa 20,Jaji Mihayo alisema Hakimu Lyamuya aliangalia kwa makini ushahidi wa upande wa mashitaka na utetezi.Marando alidai katika hilo jaji huyo hakutenda haki kwasababu mahakama ya chini iliangalia ushahidi wa upande wa utetezi kwa namna isivyolidhisha.

Akiwasilisha sababu 16,17 na 19 kwa pamoja Marando alionyesha kuwa katika ukurasa 661 haya 20,Mihayo aliendelea kusema mahakama ya Kisutu ilizingatia ushahidi wa upande wa utetezi lakini katika hukumu ya iliyotolewa na Lyamuya katika ukurasa wa 529 mstari wa 15, alidai hakimu huyo aliandika maoni yake binafsi ambayo yanapishana na mashahidi wa upande wa utetezi kitu ambacho kinapingana na sheria za nchi.

“Ukurasa wa 532 katika hukumu iliyoandikwa la hakimu huyo, utaona wazi hakimu huyo anabisahana na shahidi baada ya kumbishia shahidu huyo kwamba siyo Mzaramu,wakati shahidi huyo aliambia mahakama mama yake ni mzaramu na baba yake ni Mkongo....haya ni mambo madogo lakini yanaonyesha ni jinsi gani Hakimu Lyamuya alivyopuuza ushahidi wa upande wa utetezi.

“Waheshimiwa majaji na mahakama hii tukufu, sijawahi kuona hukumu kama hii kwa miaka 30 tangu zinaanze kazi yangu ya uwakili ...kwani sote tunachujua maoni ya hakimu katika hukumu yanaandikwa pembeni lakini katika hukumu hii hakimu ameweka maoni yake”alidai Mrando na kusababisha watu kuangua vicheko.

Akichambua ukurasa 541 mstari wa 15-16 katika hukumu ya Kisutu, mrufani wa pili, Papi Kocha anaeleza alivyokuwa mikoani akifanyaziara ya kikazi ya kimuziki, lakini hakimu Lyamuya katika hukumu yake akaweka mawazo yake kwakusema hata kama alikuwa safari anaweza kutenda makosa hayo ‘possibility crime’ aliporudi kutoka safari.

“Lakini majaji katika rufaa ya Mahakama Kuu hakuna ushahidi ulitolewa unaonyesha warufani walibaka...hayo yalikuwa ni mawazo ya hakimu kwamba lazima Babu Seya na watoto wake waende gerezani....narudia tena sijawahi kuona hakimu wa aina hii na hukumu ya aina hii ambayo hakimu aliamua kuweka maoni yake binafsi kwani kinachowatia hatiani washitakiwa katika kesi zote ni ushahidi nasiyo maoni ya hakimu”

“Ni wajibu wa mahakama kutafakari ushahidi wa utetezi hata kama hauana uzito sasa huyu Lyamuya katika hukumu yake amewataja mashahidi wa utetezi waliokuja kutoa ushahidi bila kueleza mashahidi kwa mapana walieleza nini”

“Kwa mkanganyiko huu uliofanywa na Hakimu Mkazi Mwandamizi Lyamuya siyo tu alikosea kisheria nasema alifanya makusudi na alikuwa ameshaamua kuwapeleka jela warufani” alidai Marando kwa hisia kali.

Akichambua ushahidi wa shahidi wa upande wa mashitaka Azah Hassan(7) ambaye akuapishwa,alidai shahidi huyo alifundishwa kusema uongo wa dhahiri kwani mtoto aliiambia mahaka walikuwa wakifundishwa Kiingereza na aliyekuwa mshitakiwa wa tano ambaye ni mwalimu wa shule ya Msingi Mashujaa, Sigirinda Ligomboka ambaye aliachiriwa huru.

“Watukufu majaji swali je kwanini watoto wote waseme uongo?Azah alisema alikamatwa na watoto wa Babu Seya,bila ya kutaja ni watoto gani kwa majina wala kuwatambua mahakamani ,sasa ushahidi wake siyo sahii.

“Ni Azah huyo huyo katika ushahidi wake alidai Babu Seya alimbaka lakini hakuna rekodi yoyote inayoonyesha shahidi huyo alimtaja mrufani pili,tatu na wanne.Na katika ukurasa114-115,shahidi huyo ametaja majina ya vijana waliomkamata ni Cheupe na Sembe na katika warufani wote hao hakuna mrufani mwenye majina hayo ya Cheupe na Sembe na upande wa mashitaka wala hawakuwaleta mahakamani watu hao ili wawe mashahidi.”alidai Marando na kusababisha wananchi kubaki vinywa wazi.

Akiendelea kuuchambua ushahidi wa Azah,unaonyesha shahidi huyo alikuwa akibakwa hata siku za shule na moja ya tarehe ni Oktoba 11,2004 tarehe ambayo ilikuwa ni siku ya Jumamosi ,wanafunzi hawaendi shule na kwamba tarehe hiyo tayari Babu Seya alikuwa ameishakamatwa nakuhoji kuwa sijui babu seya siku hiyo alitoka rumande na kwenda kumbaka shahidi huyo?.

Akichambua kwa ujumla ushahidi wa watoto hao ,alidai kuwa hakuna shahidi wa upande wa mashitaka aliyeiambia mahakama kuwa makosa hayo yalitendekea April,Mei,Juni,Julai,Agosti,Septemba na Oktoba isipokuwa hati ya mashitaka inasomeka kwamba makosa yote yalitendeka kati ya Septemba na Oktoba lakini Jaji na hakimu huyo wakaridhia.

Akiuchambua ushahidi wa shahidi wa 14 wa upande wa mashitaka,Days Safari ambaye aliambia mahakama ya Kisutu, kwamba hamfahamu Babu seya wala Papi na kwamba hawapo mahakamani na hata angeonyeshewa kisu asingeweza kuwatambua lakini hati ya mashitaka inasomeka shahidi huyo alibakwa warufani hao na Hakimu Lyamuya katika hukumu yake akasema kuwa upande wa mashitaka umethibitisha kesi hiyo pasipo shaka yoyote na Jaji Mihayo akamuunga mkono.

Kuhusu shahidi 11 wa upande wa mashitaka, Yasinta Mbegu katika ukurasa wa 26 wa hukumu ya Hakimu Lyamuya, aliambia mahakama hakufanywa chochote wala kubakwa na warufani,Marando alidai kwakuwa Lyamuya alikuwa ameishapanga warufani awapeleke jela akawahukumu kifungu cha maisha kwa ushahidi dhahifu na wakutunga kama huyo.

Akiendelea kuchambua ushahidi wa shahidi wa mtoto mwingine aitwaye Gift ambaye alidai mahakamani kuwa alibakwa Babu Seya na akamuambukiza Kisonono, na licha ya mrufani huyo kutaka akapimwe kama anaugonjwa huo ili ushahidi upatikane upande wa mashitaka ulikataa kwenda kumpima Babu Seya na hata hivyo ripoti ya daktari wa Hospital baada ya kumpima mtoto huyo ilibaini mtoto huyo hajaambukizwa ugonjwa huo na upande wa mashitaka ulikataa ripoti hiyo ya daktari itolewe kama kielelezo mahakamani.

Kuhusu ushahidi ulitolewa na shahidi wa tatu wa upande wa mashitaka Alocia Longino kwamba alitokwa damu baada ya kubakwa lakini taarifa ya daktari ikaja kusema shahidi huyo bado ni bikra na wala haonyeshi aliwahi kubikiriwa wala kuingiliwa kinyume na maumbile.

“Longoni alidai alikuwa anakamatwa chooni na alizishuhudia manii za Babu Seya ni nyeupe na zilikuwa zinaruka hewani kama nzi...jamani majaji huu ni uongo wa hali ya juu natunaomba jopo Hakimu Lyamuya alipata jazba wakati akitoa hukumu hiyo”alidai Marando na kufanya watu kushikwa na butwaa

Alihoji ni kilichofanya upande wa mashitaka kuficha ripoti ya daktari aliyewafanyia uchunguzi watoto hao wanaodaiwa walibakwa na warufani na kushindwa kuleta mashahidi ambao ni wanamuziki wa Bendi ya Achigo, mama wa Babu Seya na Mke wa Babu seya kwasababu waliona mashahidi hao wangewaumbua.

“Kesi hii ni ngumu kweyu sote na kama mahakama na sisitunaona warufani walifanya haya makosa tuwalaani ila mimi Marando nasema nimejiridhisha hawajafanya hayo makosa:

“Hivi tujiulize Kibaiolojia kweli inawezekana mtoto wa miaka sita apakwe na wanaume hawa(warufani)nyuma na mbele halafu mtoto wa umri huo aweze kutembea?Aiingii akilini hata kidogo nasema kesi hii ni ya kutunga kwani hata mwanamke mwenye umri wa utu uzima akifanyiwa unyama huo hawezi kutembea.”alidai Marando na kusababisha umati uliofurika kuendelea kuacha vinywa wazi kwa mshangao.

Akijibu hoja za mrufani, wakili Mkuu wa Serikali Justus Mulokozi ambaye alitumia nusu saa kujibu hoja hizo alidai kuwa kitendo cha shahidi kushindwa kumtambua mshitakiwa mahakamani siyo sababu inayopeleka ushahidi wa shahidi huyo kuonekana hauna thamani, jibu lilosababisha umati wa watu kuangua vicheko.

Mulokozi alidai pia mahakama ikiamini upande mmoja, halazimiki kuangalia upande mwingine lakini hata hivyo hoja hiyo ilipingwa vikali na Marando ambaye alidai kuwa hoja hiyo haikupaswa kutolewa na wakili mwandamizi kama Mulokozi kwani hoja hiyo inatofautiana na sheria za nchi na kauli hiyo ya wakili wa serikali imedhiirisha sasa ni kweli Lyamuya aliegemea uegemea ushahidi wa upande wa mashitaka tu.

Jaji Nataria Kimaro alisema jopo hilo tayari imeishamaliza kusikiliza rufaa hiyo na akasema jopo lake litatoa taarifa ya hukumu.

Baada ya kuairishwa kwa kesi hiyo umati wa wananchi waliofurika kufuatilia kesi hiyo walimrukia na kumkumbatia wakili Mabere Marando kwa furaha na kumpachika jina la ‘Simba wa Vita” huku wangeni wakilisukuma gari ambalo lilikuwa linawabeba warufani kuwarudisha gerezani na huku wengine wakiimba nyimbo mbalimbali za kujifari kwamba wanaimani na mahakama ya rufani chini ya jopo hilo litatenda haki.

Januari 27 mwaka 2005, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Thomas Mihayo alitupilia mbali rufaa yao iliyokuwa ikipinga hukumu iliyotolewa na aliyekuwa Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Addy Lyamuya ambaye aliwatia hatiani kwa makosa yote waliyokuwa wameshitakiwa nayo Juni 25 mwaka 2004.

Waomba rufani hao wanakabiliwa na makosa kumi ya kubaka watoto wa kike wenye umri kati ya miaka sita na nane na makosa mengine 11 ya kulawiti watoto wa kike wenye umri kama huo na kwamba wanadaiwa kutenda makosa hayo kati ya April na Oktoba 2003 eneo la Sinza kwa Remmy, jijini.

Aidha katika kesi hiyo mwalimu wa shule ya Msingi Mashujaa, Sigirinda Ligomboka, alishitakiwa kwa makosa mawili ya kumsaidia Babu Seya kutenda makosa ya kubaka na kulawiti kwa kuwaruhusu baadhi ya watoto hao kutoka madarasani.

Upande wa mashitaka ulileta mashahidi 24, ambao upande wa utetezi ulipinga vikali kutenda makosa hayo na uliita mashahidi nane.Katika hukumu yake Hakimu Lyamuya alitupilia mbali na utetezi wa Babu Seya na wanawe na akawatia hatiani kwa makosa hayo na hivyo kuwafunga kifungo cha maisha gerezani.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Desemba 4 mwaka 2009












o

2 comments:

Anonymous said...

Well done Happy! Keep it up!

Anonymous said...

Nakupongeza sana Happy, Mungu akuzidishie baraka.

Powered by Blogger.