Header Ads

MSILE SAMAKI WA MAGUFULI KABLA HAWAJACHUNGUZWA

Na Happiness Katabazi

DESEMBA 10 mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam ,ilikubali ombi la upande wa mshitaka katika kesi ya uvuvi haramu katika Bahari ya hindi eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lakutaka samaki wawage bure.


Uamuzi huo ulitolewa na Jaji Radhia Sheikh anayesikiliza kesi hiyo inayowakabili araia wa kigeni 37 wanaotetewa na wakili wa kujitegema Ibrahim Bendera na John Mapinduzi, ambapo alisema anakubaliana na ombi hilo la upade wa mashitaka na akatoa amri kwa upande huo wa jamhuri kwamba iwapo washitakiwa watashinda kesi hiyo basi ndani ya kipindi cha mwezi mmoja upande wa mashitaka,uhakishe unawasilisha sh 2,074,249,000 ili kiasi hicho wapatiwe washitakiwa.

Watanzania wenzangu amri hilo ya Jaji Sheikh ilipokelewa kwa mikono miwili na pande zote katika kesi hiyo.Na kwa mujibu wa hati ya kiapo kilichoapwa na Mkugenzi wa Uvuvi ,Nanyaro na kuambatanishwa na ombi hilo la kugawa samaki bure, Mkurugenzi huyo anaeleza kuwa thamani ya samaki hao imepungua kutoka sh bilioni mbili wakati walipokamtwa samaki hao kwenye meli ya Tawariq 1, Machi 8 mwaka huu, hadi kufikia dola za kimarekani laki saba na mia saba hasmini elfu hivi sasa.

Na kwamba Mthamini toka wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi ndiye aliyefanya tathimini hiyo.Kimsingi binadamu Yoyote mwenye akili timamu atakubaliana kwamba samaki nibidhaa ambayo inaaribika.Na kisheria tunaita (Perishable Commodity).Na kawaida kwenye sheria zetu za nchi vipo vipengele vya sheria vinavyoruhusu kuiomba mahakama iwapatie kibali cha kuwauza,au kuwagawa bure samaki hao ,wakati ule ule ilipowakamata samaki wale au bidhaa yoyote ambayo inaaribika mapema.

Sasa kuhusu samaki hao maarufu kama samaki wa John Magufuli, kwanini serikali iliisinzia wakati wote huo tangu ilipowakamata?
Sisi tulitazamia serikali yetu ingeomba amri ya mahakama ya kuwauza ili wasiaribike au kupoteza ubora wake wakati ule ule ilipowakamata?

Hata umeme ungekuwapo wa uhakika bado bidhaa hiyo ya samaki isingeishi mililele bila kuaribika kwakuwa samaki siyo mawe.

Minafikiri wizara inayoongozwa na aziri john magufuri ilifanya uzembe kwakutoomba mapema kibari cha kuwauza samaki walipowakamata na kuzembea huko kumeliingiza na kunaendelea kuliingiza taifa hasara ya mamilioni na wanahousika wanatakiwa kuchukuliwa hatua .

Kwani hao wataalamu waliopo kwenye wizara ya Mifugo kwanini walizembea muda wote huo?Ama waseme ni vihiyo na taasisi husika zitathimini vyetu vyao na katika uzembe huu, hawana budi kufikishwa pale Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa makosa ya uzembe na kuisababishia serikali hasara, kama walivyoshitakiwa maofisa wengine wa juu katika serikali ya awamu ya tatu ambao wengine wanaendelea kusota magerezani hadi sasa.Na hilo likishindikana kufanyika hilo tutalazimika kuamini yale madai kwamba wanaofikishwa mahakamani ni wale wasiyokuwa na kauli katika serikali hii ya awamu ya nne.

Binafsi nawashauri Watanzania wenzangu wasijaribu kula ha-o --samaki kabla ya samaki hao hawajachunguzwa na Mamlaka ya Chakula na Dawa(TFDA), ila atakaye kubali kuwala hao samaki bila TFDA kuwachunguza na kutoa tarifa yao ya uchunguzi, ale salama na asije kumlalamikia mtu.

Na hii tabia ya serikali kuzembea hadi bidhaa feki na mbovu zinaingia nchini kwake na wananchi wanazitumia na mwisho wa siku TFDA ndiyo inakuja kutuarifu tuache kuzitumia bidhaa hizo kwani hazifahi kwa matumizi ya binadamu inakera na ndiyo inayotupelekea baadhi y watu tutilie wasiwasi wa samaki hao kama hivi sasa wanafahaa kwa matumuzi ya binadamu.

Na hii tabia ya kutupia wananchi bidhaa mbovu mbovu iache kwani imesikia watanzania wanapenda kulishwa vitu vya bure.

Tunapaswa tujiulize sana ni kwanini serikali imeamua kuwagawa bure samaki hao waliokaa kwa muda usiyojulikana tangu wavuliwe baharini na washitakiwa hao na leo hii aamue kuwagawa mahospitalini,mashuleni, hivi serikali imesikia makundi hayo ya wananchi wenzetu ni mbwa wa jamii?.Iwaombe radhi haraka.

Pia tujiulize ni kwanini serikali imeamua kuwagawa bure ,kwasababu samaki hao ni samaki wanauzwa kwenye mahoteli makubwa duniani lakini hatujasikia wala kuona mahoteli hayo au wazabuni wakipigana vikumbo kutaka kuwanunua samaki hao ili waweze kwenda kuwauza kwenye mahoteli hayo.?

Bado tungali tukikumbuka siku samaki hao walipouzwa, ni watu wachache sana walijitikeza kununua samaki hao tena tulielezwa waliojitekeza kuwanunua ni watu wa hali ya chini kama mimi.

Nayasema haya kwasababu kuna baadhi ya watumishi wa serikali kwa siri kubwa wamekuwa wakitung’ata masikio baadhi ya ndugu na jamaa zao kwamba tusiwale samaki hao pindi watakapogawiwa.Ukiwauliza maswali kwanini wanayasema hayo hawataki kutoa ufafanuzi wa kina ila wanaishia kusema wao wanafahamu nini kinaendelea.

Kauli hizi zinajenga mashaka makubwa na ndiyo maana kwa maslahi ya taifa langu na serikali inayotuongoza nimeandika makala hii iliniweze kutoa angalizo kwa mamlaka husika.

Kwani hakuna Mtanzania yoyote wala idara zetu za upelelezi ,zinauhakika samaki hao walivuliwa lini au mwaka gani na washitakiwa hao.Tunachokifahamu sote ni siku ambayo samaki hao walikamatwa Machi 8 mwaka huu.

Sasa vyovyote iwavyo naomba kutoa angalizo kwa serikali yangu ili mwisho wa siku litakapokuja kutokea la kutokea kuhusu samaki hao,ni vyema ikachukua taadhari mapema ya kuwapima samaki hao kitaalamu na taarifa ya vipimo hivyo itangazwe adharani ili ifahamike.

Kuwalisha wananchi samaki hao bila kupimwa na TFDA au taasisi huru ya kuwapima samaki hao ,kutaonyesha kumbe serikali yetu ipo tayari kuwarisha sumu wananchi wake ili mradi ijionyeshe yenyewe ina uhuruma na wananchi wake.

Mwisho nawatakia wasomaji wote siku kuu njema ya Krismas na Mwaka Mpya.Lakini pia siku ya sikukuu ya Kristmas Desemba 25 mwaka huu, binafsi nitakuwa nasherehekea siku yangu yakuzaliwa ambapo nitakuwa natimiza miaka 30.

Mungu ibariki Tanzania ,Mungu ibariki Afrika

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi Desemba 24 mwaka 2009

No comments:

Powered by Blogger.