Header Ads

SHAHIDI AZUA JAMBO KESI YA MRAMBA

Na Happiness Katabazi

SHAHIDI wa tatu katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh biliono 11.9 inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha Basil Mramba na wenzake, ja alisababisha watu wanaoudhuria kesi kuangua vicheko baada ya kuieleza mahakama kwamba yeye yupo tayari kupanda kizimbani kutoa ushahidi wake.


Mbali na Mramba washitakiwa wengine ni Katibu Mkuu Mstaafu Wizara ya Fedha, Gray Mgonja na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Daniel Yona ambao wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Hurbet Nyange,Peter Swai,Profesa Leonard Shahidi,Cuthbert Tenga.

Kesi hiyo ambayo jana ilikuwa imekuja kwaajili ya kuendelea kusikilizwa ambapo shahidi huyo wa tatu ndiyo alikuwa anatakiwa aanze kutoa ushahidi wake asubuhi lakini hata hivyo jopo la Mahakimu Wakazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu John Utamwa, Sam Rumanyika na Saul Kinemela lilifika lilingia mahakamani hapo saa 6:28 mchana kwaajili ya kuandelea kusikiliza kesi hiyo.

Shahidi huyo ni Geogre Mtigiti aliyasema hayo baada ya kuulizwa na jopo la mahakimu hao ambao walimweleza wamefikia uamuzi wa kumuuliza kwamba kama anaweza kupanda kizimbani kutoa ushahidi kwakuwa muda mchache uliopita Wakili Kiongozi wa Serikali, Stanslaus Boniface aliambia mahakama kuwa wanaomba kesi hiyo iairishwe hadi leo kwakuwa shahidi huyo alifika mahakamani hapo tangu asubuhi na mchana huo amewaeleza kuwa anaumwa maralia.

“Waheshimiwa mahakimu minipo tayari kupanda kizimbani kutoa ushahidi wangu”alidai shahidi huyo wakati alipoitwa mahakamani na mahakimu hao na kusababisha mahakimu na wananchi walifika kwenye kesi hiyo kuangua vicheko.
Hata hivyo wakati Hakimu Mkazi Utamwa na Sam Rumanyika wakimuuliza shahidi huyo kama yupo tayari, wakili wa serikali Boniface alikuwa akijaribu kuingilia kati lakini hata hivyo mahakamani hao walimweleza Boniface kuwa mahakama hiyo pia ina mamlaka ya kumhoji shahidi huyo kuhusu hilo hali iliyosababisha pia watu mahakimu na watu wanaoudhuria kesi kuendelea kuangua vicheko.

Kiongozi wa Jopo hilo ambaye pia ni Msajili wa Mahakama Kuu nchini, John Utamwa alisema. “Kwa kuwa pande zote mbili hazipingi kuairishwa kesi hiyo ….na kwakuwa Boniface aliambia mahakama shahidi wake anaumwa maralia lakini shahidi huyo jopo lilipomhoji akasema yupo tayari kuanza kutoa ushahidi wake ,tunaairisha kesi hii kesho(leo) asubuhi”alisema Utamwa huku akicheka.

Tayari mashahidi wawili walishatoa ushahidi wao na kesi hiyo ilipangwa kuanza kusikilizwa jana hadi Ijumaa wiki hii.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Jumatano, Desemba 16 mwaka 2009

No comments:

Powered by Blogger.