Header Ads

VIONGOZI WA DECI WANYIMWA DHAMANA

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imewanyima dhamana Wakurugenzi wa taasisitaasisi ya Development Entrepreneurship for Community Initiative (Deci) wanaokabiliwa na tuhuma za wizi wa sh milioni 18 kutokana na kukiuka masharti ya dhamana waliyopewa awali.


Katika hatua nyingine upande wa mashitaka katika kesi Na.109 ya mwaka huu, ya kuendesha na kusimamia mradi wa upatu kinyume na kifungu 111A(1,3)cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002, umeiambia mahakama kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na mahakama hiyo imepanga Januari 13 mwakani, washitakiwa watakuja kusomewa maelezo ya awali.Kesi hiyo pia iliyofunguliwa mahakamani hapo Juni 12 mwaka huu, inawakabili pia washitakiwa hao.

Akitoa uamuzi huo jana, Hakimu Mkazi, Alocye Katemana, alisema kwamba hakuna ibishi kuwa wshitakiw ahao ambao wanakabiliwa na kesi nyingine mahakamani hapo wamekiuka masharti ya dhamana ya kutotenda kosa lingine wakiwa nje kwa dhamana.

Washitakiwa hao ni Dominick Kagendi, Jackson Sifael Mtaresi, Timetheo ole Lating’ye na Samuel Sifael Mtaresi.

“Nakubakubaliana na pingamzi la upande wa mashitaka kwa sababu washitakiwa wazi wamekiuka masharti ya dhamana yaliyowekwa na mahakama hii katika kesi nyingine inayowakabili, hivyo naamuru warejeshwe rumande hadi Desemba 31 mwaka huu,” alisema Hakimu Katemana.

Kesi nyingine inayowakabili washitakiwa hao ambayo imeelezwa kwua upelelezi wake umekwishakamilika itaanza kusikilizwa Januari 13 mwakani kwa washitakiwa kusomewa maelezo ya awali.

Kampuni ya DECI iliyowanufaisha watu wengi hasa wale waliojiunga mwanzoni, iliibua malumbano kati ya serikali, viongozi wa kampuni hiyo na wanachama wao, waliopinga hatua ya serikali kusitisha shughuli zake kwa madai kuwa haiko kihalali.

Kusimamishwa kwa shughuli za kampuni hiyo, kulitokana na uamuzi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kutoa taarifa ya kuwatahadharisha Watanzania waliojiunga na upatu huo kuwa, taasisi hiyo haiko kisheria na wanaweza kupoteza fedha zao walizopanda.

Shughuli za kupanda na kuvuna mbegu DECI zilisitishwa baada ya serikali kusimamisha akaunti za kampuni hiyo hadi hapo uchunguzi utakapokamilika, hali ambayo baadaye ilisababisha uvunjifu wa amani katika ofisi za kampuni hiyo, baada ya wanachama wake kuamua kuchukua sheria mkononi kwa kuvunja vioo vya magari ya viongozi, wakitaka warejeshwe fedha zao.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Desemba 22 mwaka 2009

1 comment:

Mzee wa Changamoto said...

Dada Happy
Kwa niaba ya familia yangu na wapenda mema wote nakutakia kila lililo jema wakati huu wa sikukuu na usalama kuelekea mwaka mpya
Baraka kwako

Powered by Blogger.