Header Ads

ASASI ZATAKIWA KUJIKOSOA

Na Happiness Katabazi aliyekuwa Dodoma

WANAHARAKATI kutoka asasi zisizo za kiserikali nchini,wametakiwa wajikosoe wenyewe kwanza katika matumuzi ya fedha na rasilimali wanazopewa na wafadhali.


Rai hiyo imetolewa na Mchumi toka Idara ya Bajeti Wizara ya Fedha na Uchumi, Oswald Kyamani wakati akichangia mada ya mkutano mkuu wa asasi hizo ulioandaliwa na Pact Tanzania ambao uliofanyika kwa siku mbili New Dodoma Hoteli mjini humo.

Kyamani alisema kimsingi asasi hizo zimekuwa zikifanyakazi nzuri hali ambayo imesababisha hivi sasa baadhi ya watendaji serikalini wamekuwa na nidhamu ya matumuzi ya fedha na rasilimali ya mali ya umma na wameongeza uwajibikaji nakuongeza kuwa serikali itaendelea kuthamini mchango wa asasi hizo kwa lengo la kuliletea taifa maendeleo.

“Serikali hasa wizara yetu inautambua mchango wetu ila asasi hizi zimekuwa zikifichua mabaya tu yanayofanywa na baadhi ya watendaji na mazuri yanayofanywa na watendaji hao wamekuwa hawayasemi katika ripoti zao….kwahiyo sisi serikali tupo tayari asasi zenu zifichue ubadhilifu unaofanywa na watendaji wetu lakini na nyie asasi za kirai mmekuwa mkituhumiwa kwa ubadhilifu wa fedha mnazopewa na wafadhili sasa wakati umefika nanyie asasi za kiraia mjisafishe na mnyosheane vidole.

“Kwasababu huwezi kuinyoshea kidole serikali kwamba baadhi ya watendaji wa wilaya zake zimefanya ubadhilifu wakati katika hizo asasi zenu miongoni mwenu mnafuja fedha mlizopewa na wafadhili kwaajili ya kufanya shughuli za maendeleo katika tauifa hili”alisema Mchumi Kyamani.

Aidha alizishauri asasi hizo pindi zimalizapo kuandika ripoti zao za matokeo ya ufutiliaji wa matumuzi ya fedha za serikali waakikishe wanatengeza mtandao ambao utawawezesha kuzifikisha ripoti hizo katika idara yake ili ziweze kufanyiwa kazi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Julai 3 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.