Header Ads

MTAMBALIKE KUMVAA ROSTAM IGUNGA

Na Happiness Katabazi

MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Deusdedit Mtambalike, ametangaza rasmi nia ya kuwania ubunge katika Jimbo la Igunga ambalo kwa sasa linaongozwa na Rostam Aziz.


Akizungumza na Tanzania Daima juzi jijini Dar es Salaam, Mtambalike alisema amefikia uamuzi huo baada ya kuona jimbo hilo halipigi hatua za kimaendeleo.

Mtambalike ambaye ameishawahi kuwa mkuu wa wilaya katika Wilaya ya Muleba, Igunga, Ngara, Tunduru na Ludewa, alisema nia yake ni kutaka kuleta maendeleo katika jimbo hilo kwani Wilaya ya Igunga anaifahamu vema.

“Nia yangu ni njema nataka kuleta maendeleo kwenye Jimbo la Igunga kwani si siri wakulima wa pamba, tumbaku, na wafugaji hawana mtu wa kuwasemea wala kuwapigania haki zao,” alisema

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Julai 8 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.