Header Ads

WAZIRI MAUA AAMULIWA KULIPA SH MIL.100

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemwamuru Naibu Waziri wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Mawasiliano, Dk. Maua Daftari, kumlipa mfanyabiashara Fatma Salim, sh milioni 100.7 baada ya kubaini alivunja mkataba na mdaiwa huyo.


Hukumu hiyo, jana ilikuwa ni mara ya pili ikiwa chini ya Jaji Fedrica Mgaya, ambapo mwaka juzi hukumu hiyo, ilisomwa na jaji Laurian Kalegeya ambaye kwa sasa ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa ya Tanzania.

Jaji Fedrica, alisema amefikia uamuzi wa kutoa amri ya kumtaka mdaiwa (Dk. Daftari), alipe kiasi hicho cha fedha mdaiwa badala ya sh milioni 410, kiasi ambacho mdaiwa aliomba amlipe, baada ya kubaini madai mengine katika hati ya madai, Dk. Daftari ameshindwa kupeka ushahidi wa kuthibitisha madai hayo.

Jaji Mgaya, alisema dai la sh milioni 1,760 ni dai ambalo limeweza kuthibitishwa kwa vielelezo kwa sababu mdaiwa na mlalamikaji waliandikishiana kisheria na ndiyo maana ameamuru mdaiwa amlipe kiasi hicho.

Matukio hayo, yalitendeka kati ya mwaka 1994-1996 na kesi hiyo ilifunguliwa mahakamani hapo mwaka 1999 na wakili wa Dk. Daftari Peter Swai.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi,Julai 10 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.