Header Ads

KESI YA JERRY MURRO YAAHIRISHWA


HATIMAYE Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, Gabriel Milumbe, amekubali ombi la upande wa Jamhuri katika kesi ya kuomba rushwa ya sh milioni 10 inayomkabili aliyekuwa mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1), Jerry Muro na wenzake wawili la kuahirisha usikilizaji wa kesi hiyo hadi wiki ijayo.

Hakimu Milumbe alikubali ombi hilo kwa kuwa Wakili Mkuu wa Serikali Stanslaus Boniface ambaye anaendesha kesi hiyo yuko likizo.

Mbali na Muro, washitakiwa wengine ni Deogratius Mgasa na Edmund Kapama wanaotetewa na mawakili wa kujitegemea Richard Rweyongeza, Majura Magafu na Pascal Kamala.

Hakimu Milumbe pia alisema anaahirisha kesi hiyo kwa kuwa hali yake kiafya si nzuri, hivyo anajiandaa kwenda hospitali. Kesi imeahirishwa hadi Agosti 18.

Juzi, Hakimu Milumbe aliuchachamalia upande wa Jamhuri kwamba kama haupo tayari kuendelea na kesi hiyo, ataifuta na kuongeza kuwa hayupo tayari kuahirisha kesi hiyo kwa sababu ya wakili Stanslaus kutokuwapo mahakamani.

Washitakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka matatu, likiwemo la kula njama za kutaka kupokea rushwa kutoka kwa aliyekuwa mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, Michael Karoli Wage.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Agosti 12 mwaka 2010


1 comment:

La Princessa said...

huyu jamaaa ana zali..anyway dont forget to pass by laprincessaworld.blogspot.com...love this site!

Powered by Blogger.