Header Ads

KESI YA MTIKILA YAPIGWA KALENDA

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mare nyingine tena jana ilijikuta ikishindwa kuendelea kusikiliza kesi ya uchochezi inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila kwasababu shahidi wa upande wa jamhuri kushindwa kufika mahakamani kwasababu ni mgonjwa.


Wakili wa Serikali Zuberi Mkakatu mbele ya Hakimu Mkazi Ritha Tarimo alidai kuwa shahidi waliyekuwa wakitarajia kumleta leo kutoa ushahidi wake anaugua hivyo wanaiomba mahakama iairishe usikilizwaji wa kesi hiyo.

Hakimu Tarimo alikubaliana na ombi hilo na akaiarisha hadi Septemba 7 mwaka huu, na akaamuru hati za wito wa wakuitwa mahakamani zitolewe kwa mashahidi na mashahidi wafike mahakamani bila kukosa.

Kesi hiyo ya uchochezi Na. 132/ 2010 , Mtikila anadaiwa kutoa maneno ya uchochezi dhidi ya Rais Jakaya Kikwete kuwa kiongozi huyo anaangamiza ukristo kwasababu amekuwa akiukumbatia uislamu hivyo kuwataka waskristo wote waungane haraka na waakikishe wanamuingiza rais mkristo Ikulu ili kuweza kuunusuru ukristo hapa nchini.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Agosti 11 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.