Header Ads

MAHAKAMA YAOMBWA KUFANYIA MAREJEO AMRI UTETEZI WA KAKOBE

Na Happiness Katabazi
WALIOKUWA wachungaji watatu wa Kanisa Full Gospel Bible Fellowship wameiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ifanye marejeo ya amri yake iliyoitoa Julai 11 mwaka huu, ambayo ilimtaka mdaiwa ambaye ni askofu Mkuu wa Kanisa hilo, Zakaria Kakobe awasilishe utetezi lakini akashindwa kutekeleza amri hiyo.


Wachungaji hao ambao ni walalamikaji katika kesi ya madai Na. 79/2011 ni mchungaji Dezidelius Patrick, Angelo Mutasingwa na Benedict Kaduma ambao katika kesi ya msingi iliyopo mbele ya Jaji Agustine Shangwa, wanamlalamikia Kakobe kuwa amekuwa akiliendesha kanisa hilo kinyume na taratibu.

Wadaiwa hao wamewasilisha ombi hilo la kuoiomba mahakama hiyo iifanye mapitio ya amri yake ikiwa ni siku chache tu baada ya mdaiwa (Kakobe) kuwasilisha utetezi wake ndani ya siku 21 ambapo siku hizo 21 zilianza kuhesabiwa Juni 29 mwaka huu, siku ambayo mdaiwa huyo alipokea hati ya wito wa mahakama(Summons) toka katika kampuni ya udalali ya Majembe Auction Mart na siku hizo 21 zilikuwa zikimalizika Julai 21 mwaka huu.

“Tunaiomba mahakama hii ichukulie uzito hili ombi letu kwamba mdaiwa(Kakobe) alikataa kukubali hati ya wito wa mahakama kaunzia Juni 23,25 na 27 mwaka huu wakati mwakilishi wa kampuni hiyo ya udalali ilipomlekea hati hiyo na mwakili huyo alirudi kwa kwa wakili wetu Miriam Majamba na kumweleza ameshindwa kumpatia Kakobe hati hiyo kwasababu hakuwepo wakati ukweli ni kwmaba alikuwepo Juni 29 mwaka huu.

“Siku hiyo hiyo ya Juni 29 mwaka huu, hati hiyo ya wito ilipokelwa na mtu mmoja aitwaye Mpokela kwaniaba ya mdaiwa na kwamba mdaiwa siku zote hizo alikuwepo hapa jijini Dar es Salaam, isipokuwa Julai 6 na 7 ambapo mdaiwa alikuwa safari mkoani Dodoma.

Aidha wadaiwa hao walidai kuwa kwakuwa mdaiwa alishindwa kuwasilisha utetezi wake ndani ya 21 alizopewa na mahakama na badala yake akawasilisha utetezi wake Julai 29 mwaka huu, alipaswa aiombe mahakama imuongee muda wa kuweza kuleta utetezi wake na kwakuwa ameshindwa kafanya hivyo ni kinyume na cha sheria ya madai na katiba ya nchi.

Katika utetezi wake huo Kakobe ameieleza mahakama kuwa walalamikaji wote waliwai kubainika kutenda vitendo viovu na kwamba uongozi wa kanisa hilo ulishawavua madaraka yao ya uchungaji hivyo na kuongeza kwa kuiomba mahakama hiyo itupilie mbali kesi hiyo kwani haina msingi wowote.

Aidha Jaji Shangwa aliairisha kesi hiyo hadi Septemba 5 mwaka huu, ambapo siku atasikiliza pingamizi lilowasilishwa na Kakobe.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Agosti 3 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.