Header Ads

MSOMI WA UDSM AJITOSA KUMRITHI ROSTAM


Na Happiness Katabazi
KADA kijana wa Chama Cha Mapinduzi(CCM), Ngassa Nichoulaus (26) jana alijitokeza kuchukua fomu za kuwania ubunge katika Jimbo la Igunga mkoani Tabora na kusema kuwa amefikia uamuzi huo kwasababu anataka kujenga misingi ya umoja na ushirikiano baina ya watendaji wa serikali na wananchi wake.


Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana mchana muda mfupi baada ya kuchukua fomu , Ngassa ambaye mwenye Shahada ya Siasa na Utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, akabidhiwa fomu hizo jana na Katibu wa CCM, Wilayani Igunga Neema Adamu ambapo alisema amefikia uamuzi huo wa kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM, ili aweze kuendelea kusukuma gurumu la maendeleo katika jimbo hilo na kuendeleza yote aliyoaanzisha Rostam Aziz ambaye alijiudhuru kiti hicho Julai 13 mwaka huu.

“Naomba chama changu CCM kinipe ridhaa ya kupeperusha bendera yake ili niweze kujenga uongozi wenye misingi yenye uwajibikaji wa kweli kwa wananchi wa jimbo la Igunga na taifa kwa ujumla ili kuakikisha wananchi wanapata fursa ya kutimiziwa mategemeo na matumaini yao yaliyojengwa kwa msingi wa imani kubwa ya juu ya serikali ya CCM chini ya Rais Jakaya Kiwkete”alisema Nichoulaus.

Aidha alisema endapo atapata ridhaa ya chama chake ataendelea kuwasemea kuwasemea wananchi wa jimbo hilo ndani ya Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kwa kujenga hoja na ushawishi katika kutekeleza ahadi za chama,ahadi za serikali na ahadi za rais kwa wananchi wa jimbo la Igunga.

Hata hivyo anawaomba wananchi wa jimbo hilo waiunge mkono kwa moyo mmoja na imani kubwa juu yake katika kuendelea kujenga Igunga yao yenye watu wachapakazi na rasilimali zenye umuhimu mkubwa katika kujenga uchumi wao katika kutimiza hilo atashirikiana nao katika kuimalisha sekta za kiuchumi,kijamii na kisiasa,kufukia malengo yao yanayoongozwa na dhamira ya kweli itakayojengwa katika misingi ya Dira ya maendeleo ya Taifa 2025,Mpango wa Maendeleo ya Taifa 2011/2012-2015/2016 na Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2010-2015.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Agosti 12 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.