Header Ads

MAHALU AANZA KUJITETEA

Na Happiness Katabazi
ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa alipofika katika ubalozi huo alikuta ofisi hizo zikiwa na hali mbaya hali iliyosababisha kutoa fedha zake mfukoni na kunua thamani zenye hadhi ya ofisi ya ubalozi.


Sambamba na hilo Balozi Mahalu mawasiliano kati ya rais wanchi, balozi,waziri wa Mambo ya Nje na Katibu uwa ya aina tatu.Aina ya kwanza ni mawasiliano ya maandishi yaani barua za kawaida, maandishi ya mafumbo na mawasiliano ya mdomo.Rais anamamlaka ya kumpigia simu balozi kokote alipo na kumpa maelekezo au kumwita balozi aje hapa nchini na kisha kumpa maelekezo ya ana kwa ana bila maandishi.

Profesa Dk.Mahalu alitoa maelezo hayo jana wakati akiongozwa kutoa utetezi wake na wakili wake Mabere Marando, Alex Mgongolwa kwa mara ya kwanza tangu alipofunguliwa kesi ya uhujumu uchumi mwaka 2007, mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi Ilvin Mugeta ambapo alidai kutokana na kuikuta ofisi hiyo ikiwa na hali hiyo mbaya alilazimika kutoa fedha zake mfukoni kwaajili ya kununulia thamani za ofisini.

Mahalu alidai kuwa Aprili 1 mwaka 2000 ndiyo siku aliyofika rasmi mjini Rome nchini Italia ikiwa ni siku chache baada ya aliyekuwa rais wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa kumteua kuwa Balozi wa Tanzania nchini humo, ambapo alieleza majukumu yake yalikuwa ni kulinda na kuyatetea maslahi ya Tanzania na wakati akiwa Balozi wa Italia pia wakati huo huo alikuwa pia ni balozi wa nchi tisa ambazo ni Griss, Turkey, Sebia,Slovenia,Croation, Mesedonia, Mountentenegro.

Alieeleza pia jukumu jingine ni kupokea maelekezo toka hapa nchini kuhusu kukuza mahusiano baina ya nchini na nchi na kwamba yeye ndiye aliyekuwa mkuu wa masuala yote ya utawala wa ofisi ya ubalozi na kwamba masuala yote ya utawala yalikuwa yakiletwa kwake na maofisa wa ubalozi na serikali kwa ujumla.

“Nilipofika Italia nilikuta hali ni mbaya inasikitisha kwani ubalozi wa wetu nchini Italia ulikuwa umefungwa tangu mwaka 1994 na nilipoteuliwa mimi kwenda huko ndiyo nikawa nimeenda kuufungua ubalozi huo uanze kufanyakazi.Na wakati nafika hapo kila kitu cha ubalozi kilikuwa kimeondolewa na kurudishwa nchini kikabaki kiofisi kidogo tu kwaajili ya kushughulikia masuala ya kilimo na mwaka 1997 ndiyo serikali ilimpeleka msimamizi wa ofisi hiyo.

“Nilipofika hapo Rome nilianzia kazi kwenye hicho kiofisi kidogo chenye ukubwa wa skwea mita kati ya 88 na 100, nikakuta ofisi hiyo ikiwa na meza ya miguu mitatu ,kiti kimoja ambacho kilikuwa kinaaribika mara kwa mara ambacho niliogopa kukitumia na kochi lililochoka na simu moja vitu vyote hivyo vikiwa vimechakaa, maofisa wake watatu ofisi zao zilikuwa ni vyumba vitatu vidogo vya kulala,huduma ya maliwato ilikuwa mbovu, jiko ndiyo tukaifanya ofisi ya kupokelea wageni ambapo dereva ,katibu mhutasi na wahudumu ndiyo walikuwa wakishinda humo wakati wa saa za kazi.

“…ikanilazimu kutoa fedha zangu mfukoni zikaenda kununua thamani za kisasa ambazo ni meza, seti ya makochi kwaajili ya matumuzi ya ofisi lakini kutokana na udogo wa ofisi hiyo ni makochi mawili tu ndiyo yaliyoingia makochi mengine yakakosa nafasi”alidai Profesa Dk.Mahalu.

Alidai kuwa baada ya kukuta hali hiyo alichukua hatua ya kumweleza aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa wakati huo, Balozi Kibeloh na kwamba aliyekuwa waziri wa wizara hiyo kwa kipindi hicho alikuwa Jakaya Kikwete ambaye kwa sasa ndiyo rais wanchi ambaye naye alifika katika ofisi za ubalozi huo na kushuhudia hali hiyo mbaya na kwamba Kikwete aliunga mkono hoja yake kwamba ofisi hiyo ni mbovu na akashauri ipatikane ofisi yenye hadhi ya ubalozi.

Aliendelea kueleza mbali na Kikwete, pia aliyekuwa Makamu wa Rais wa Serikali Dk.Ally Mohamed Shein naye alitembelea ofisi hizo za ubalozi na kushuhudia ubovu ule na akamuahidi mshtakiwa huyo kuwa akirudi nchini atafikisha tatizo hilo ili taratibu zifanywe za kupatikana jengo kubwa la ubalozi.

Profesa Dk. Mahalu alieleza kuwa baada ya kumueleza matatizo hayo ya ubalozi Katibu Mkuu, Balozi Kibeloh ,alikubaliana naye akasema ni muhumi kwa serikali kutafuta jengo jipya na kwamba Mei 2001, alitaarifa na balozi huyo kuwa Rais Mkapa atakwenda Brussels kwa ziara ya kikazi na kwamba yeye mshtakiwa akamuomba tena katibu mkuu huyo amruhusu akamweleza Mkapa matatizo hayo pindi atakapofika Brussels na katibu mkuu huyo alimruhusu.

“Rais Mkapa nilipokutana naye pale Brussels nikamueleza umuhimu wa kununua jengo jipya la ofisi ya ubalozi mjini Rome na kwasababu majadiliano ya kuaandaa bajeti ya serikali yalikuwa yameanza inawezekana rais mkapa akalieleza jambo hilo kwa mawaziri wake ili watenge bajeti ya kununua jengo la ubalozi huo…rais alinielewa na alikuwa akifahamu ubalozi huo ulikuwa umefungwa tangu mwaka 1994 na akaniakikishia serikali yake itajitahidi ipate fedha za kujenga au kununua jengo la ofisi hizo lenye hadhi na sifa za ubalozi.

“Niliporudi mjini Rome Italia, nilimjulisha kwa barua Katibu Mkuu Balozi Kibeloh mazungumzo yangu na rais Mkapa na balozi huyo naye akanijibu kuwa atazidi kulifuatilia jambo hilo na kuliweka kwenye bajeti ya wizara ya mambo ya nje na kwasababu hiyo ilikuwa ni sera ya wizara yake ya kutaka ofisi za ubalozi wetu nje ya nchi zinunuliwe majengo yao hivyo hoja hiyo itapelekwa bungeni na haitapingwa ”alidai Profesa Dk.Mahalu.

Mshtakiwa huyo aliendelea kueleza kuwa wakati akisubiri ahadi hiyo ya Katibu Mkuu huyo, mwanzoni mwa Juni 2001, Katibu Mkuu huyo alimpigia simu akimpongeza kwamba maombi ya wizara yao katika bajeti ya kutaka kila ofisi ya ubalozi inunue jengo lake itapitishwa na bunge na kuongeza kuwa Katibu mkuu alimtaka mshtakiwa huyo na maofisi wengine wa ubalozi kuanza kutafuta majengo na kwamba yeye mshtakiwa aliwaagiza maofisa wake kwenda kutafuta majengo ndani na nje ya mji wa Rome kwaajili ya kulinunua ili kulifanya ofisi ya ubalozi.

Alidai kuwa baada ya kupokea habari hiyo njema toka kwa Katibu Mkuu, yeye mshtakiwa alimuandikia barua katibu mkuu huyo ya kumshukuru ambayo ni barua ya Mei 4 mwaka 2009 ambayo ninakala na kwamba aliomba mahakama iipokee kama kielelezo na hakimu mkazi Mgeta aliipokea kama kielelezo cha kwanza.

Hakimu Mgeta aliairisha kesi hiyo Agosti 26 mwaka huu, ambapo mshtakiwa huyo wa kwanza Mahalu ambaye bado hajamaliza kutoa utetezi wake ataendelea kutoa utetezi wake.Mbali na Mahalu mshtakiwa mwingine wa kesi hiyo ya uhujumu uchumi wa Euro milioni mbili ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa ubalozi huo, Grace Martin.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima, Agosti 5 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.