Header Ads

MAHAKAMA YAMNG'ANG'ANIA MSHARIKA WA PONDA



Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imetupilia mbali pingamizi la mawakili wa upande wa utetezi    
katika  kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh.milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya ya na Taasisi za Kiislamu Sheikh Issa Ponda na wezake, lilokuwa linataka mahakama hiyo isipokee  kama kielelezo maelezo ya ungamo yaliyotolewa na mshitakiwa  wa tano katika kesi hiyo Mkadamu Swaleh Abdallah,polisi  kama kielelezo.

Uamuzi huo uliotokana na kesi ndogo iliyofanyika jana asubuhi, ulitolewa na Hakimu Victoria Nongwa jana saa nane mchana ambapo alisema mahakama yake jana asubuhi ilipata fursa ya kuendesha kesi ndogo iliyoendeshwa jana asubuhi mahakamani hapo  ambapo upande wa jamhuri unaowakiliwa na wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka na Zuberi Mkakatu ili kuthibitisha maelezo yale ungamo ya Mkadamu yalikuwa yamekidhi matakwa ya sheria walileta mashahidi wawili ambao ni Sajenti Masikini ambaye alimkamata Mkadamu na Sajenti Mkombozi Mhando ambaye ndiye aliyemchukua maelezo mshtakiwa huyo , ambao walitoa ushahidi wao na upande wa utetezi ulileta shahidi mmoja ambaye ni Mkadamu naye alitoa ushahidi wake mfupi.

Hakimu Nongwa akitoa umuzi wake alisema mahakama yake imefikia uamuzi wa kulipokea ungamo hilo chini ya kifungu cha 169 cha Sheria ya Makosa ya Jinai ya mwaka 2002  licha ni kweli ungamo hilo limevunja matakwa ya kifungu cha 50(1)(a) kinachomtaka ofisa wa polisi amchukue maelezo mshitakiwa ndani ya saa nne tangu alipokamatwa lakini Mkadamamu alichukuliwa maelezo hayo masaaa manne yalikuwa yamepita na hivyo kufanya ongezeko la muda la masaaa matatu.

“Licha mahakama hii inakipokea kielelezo hiki ambacho kimeandaliwa nje ya muda wa sheria unavyotaka lakini ieleweke kwamba kifungu cha 169 cha Sheria ya Makosa ya Jinai, kinailazimisha mahakama kupokea kielelezo cha aina hiyo ambacho kimezidisha muda kwani mahakama hii imeona kuongezeka kwa masaa matatu nje ya muda wa sheria uanvyotaka hakukuweza kumshawishi mshitakiwa huyo kukiri makosa yake ndani ya ungamo hilo ambalo amekiri kutenda makosa yanayomkabili likiwemo kosa la kuingia kwa jinai katika kiwanja cha Chang;’ombe Markas na kwamba anakipokea ungamo hilo kama kielelezo’alisema hakimu Nongwa.

Kufanyika kwa kesi hiyo ndogo kulitoka na pingamizi lilowasilishwa juzi na mawakili wa utetezi Juma Nassor  wakati shahidi wa nane wa upande wa jamhuri Sajenti Mkombozi Mhando kuomba maelezo hayo ya onyo yapokelewe kama kielelezo kwasababu yamekidhi matakwa ya kisheria na ndipo mawakili hao wa utetezi walipinga kisipokelewe na ndipo mahakama juzi ikatoa amri ya jana kuiendesha kesi ndogo ili kubaini ukweli kuhusu maelezo hayo ambapo ilikubali kuyapokea kama kielelezo.
  
Baada ya uamuzi huo kumalizika kutolewa saa 8:30 mchana, kesi kubwa ilianza kusikilizwa ambapo shahidi wa tisa wa jamhuri Sajenti Juma alianza kutoa ushahidi wake na kudai kuwa yeye ndiye mpelelezi wa kesi hiyo na kwamba alipewa jukumu la kwenda kutembelea eneo la tukio la kiwanja cha Chang’ombe Marks na kushuhudia uharibu mkubwa ulikuwa umefanywa na washtakiwa hao ambao wanadaiwa kuingia kwa jiani katika eneo hilo na kujenga msikiti wa muda.Kesi hii inaendelea leo tena leo kusikilizwa mfululizo.

Wakati huo huo , Mkuu wa Upelelezi Kanda ya Kipolisi Mkoa wa Dar es Salaam(ZDCO), Hemed Msangi ambaye ni shahidi wa kwanza katika kesi ya kula njama na kufanya maandamano haramu inayowakabili Salum Bakar Makame na wenzake 53 jana alieleleza mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa kati ya Februali 11-17 mwaka huu, yeye alikuwa ndiye Kamanda wa Kanda ya Maalum ya Dar es Salaam, na kwamba  Februali 11 alipokea barua toka Shura ya Maimamu iliyokuwa ikimuomba kibari cha kufanya maandamano ya kwenda ofisi kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), kumhoji ni kwanini hampatii dhamana  Ponda na kwamba maandamano hayo walikuwa wakitaka yafanyike Februali 15 baada ya swala ya Ijumaa na wataandamana kutokea misikiti mbalimbali.

Kamishna Msaidizi huyo wa Polisi, Msangi alidai  yeye na maofisa wenzake walitafakari hiyo barua  ambayo ilikuwa na saini ya Sheikh  Juma  Idd ambaye ni Amir wa Shura ya Maimamu  Temeke na walijiuliza uzito wa maandamano hayo na kwamba jeshi hilo walibaini kuwa hawakuwa na askari wa kutosha wakuwapeleka kila msikiti kwaajili ya kuyalinda waandamanaji hao na hivyo uhaba huo wa askari ungeweza kuleta usalama mdomo na pia walifikia uamuzi wa kuyakaza maandamano yake kwasababu waliona ofisi ya DPP ipo katikati ya jiji na ina sehemu finyu hivyo maandamano hayo yangeruhusiwa yangweza kuathiri haki za watu wengine wanaotumia jengo hilo la ofisi ya DPP ambalo linatumiwa na maofisi mengi na watembea kwa mguu.

“Pia jeshi la polisi lilitazama kuwa kesi ya Ponda ipo mahakamani hivyo ingewaruhusu waandamanaji hao kwenda mahakamani ni kama kuingia huru wa mahakama  na kwamba jeshi lilipata taarifa toka kwa DPP kuwa DDP alikuwa amepokea barua toka kwa Baraza la Wanazuoni iliyokuwa ikimuomba wakazungumze naye na kwamba tayari DPP alishalikubalia baraza hilo kuwa angekutana nao Februali 28 mwaka huu, ....kwasababu hiyo mimi niliwandikia barua ya kuzuia kufanyika kwa maandamano kwa sababu hizo zilizozitaja hapo juu kwani pia jeshi lilikuwa limepata taarifa za watu walikuwa wamepanga kufanya vurugu katika maandamano hayo”alidai ZDCO-Msangi.

Aliendelea kueleza kuwa licha ya kuwapelekea zuio hilo la maandamano kwa maandishi waombaji hao wa maandamano, pia yeye aliutangazia umma kupitia vyombo vya habari kuwa jeshi la polisi limezuia maandamano hayo lakini ilipofika Februali 15 washitakiwa hao walikaidi amri hiyo ya jeshi polisi waliandamana wakiwa na mabango, mawe,na silaha za jadi na mwishowe waliishiwa kukamatwa,kuhojiwa na kufikishwa mahakamani.

Hata hivyo washtakiwa hao ambao walifikishwa kwa mara ya kwanza juzi ,jana wakati Msangi akitoa ushahidi wake walilazimika kumhoji maswali kwamba anauthibitisho gani kwamba wao ni wafuasi wa Ponda na kwamba una ushahidi gani kama hao washitakiwa walikuwa wameandamana siku hiyo lakini hata hivyo shahidi huyo na hakimu Sundi Fimbo waliwataka washitakiwa hao wasubiri mashahidi waliowakamata siku wakija kutoa ushahidi mahakamani ndiyo wawaulize maswali hayo kwani shahidi huyo Msangi siye aliyewakamata na kesi hiyo imearishwa hadi leo ambapo shahidi wa pili anakuja kuanza kutoa ushahidi na washitakiwa wote wamerudishwa gerezani kwasababu dhamana zao zimefungwa na DPP na mahakamana.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Februali 20 mwaka 2013.



No comments:

Powered by Blogger.