Header Ads

UDHAIFU HUU MAHAKAMA YA KISUTU HADI LINI?



Na Happiness Katabazi

HII siyo mara yangu ya kwanza kuandika makala zaidi ya nne sasa zinazoushauru mhimili wa mahakama uanchane na ukirimba na mambo ya kizamani na badala yake ikubali mabadiliko katika mambo kadhaa kutoka na wakati tuliopo.

Leo hii tena nimelazimika kuandika makala hii ya kuinyoshea kidole mhimili wa mahakama ya Tanzania ya kuiomba mhimili huo uamke katika usingi wa pono uliolala na uone kuwa hivi sasa mhimili wa serikali kupitia Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP),DK.Eliezer Feleshi kuanzia Oktoba 18 mwaka jana ,hadi 
Februali 18 mwaka huu, tayari umeishafungua zaidi ya tano za jina.

Ambapo kesi hizo zinawakabili baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu ikiwemo kesi ya uchochezi na wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh.milioni 59 inayomkabili Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49.

Kesi hizo zote chanzo chake ni tuhuma za kuchoma makanisa huko Mbagala mwaka jana, kufanya maandamano haramu katika Wilaya ya Ilala.Na kesi zote hizo zimeanza kusikilizwa tena kwa kasi ya ajabu na nitakuwa ni mnyimi wa fadhila kama sitapongeza jeshi la polisi kwa kuarakisha upelelezi na mahakama kwa kuanza kusikiliza tena kesi ya Ponda na kesi nyingine inayowakabili wafuasi wake 54 walioandamana Ijumaa iliyopita zimeanza kusikilizwa mfululizo na kwa kasi ya ajabu.

Kwa sisi waandishi wa habari za mahakamani ni mashahidi wa hilo, ila kikubwa kinachotukera na hatua ya mhimili wa mahakama kushindwa kusoma harama za nyakati kwa ama kutoa fedha za dharula katika bajeti yake kwenda kununua hata feni nne tu kufunga katika kumbi mbili za mahakama hiyo zinazotumika kuendeshea kesi ya Ponda ina jumla ya washtakiwa 49, kesi ya wafuasi wa Ponda inajumla ya washtakiwa 54.

Si hilo ,mhimili huo umeshindwa kubaini kuwa mashahidi wanaotoa ushahidi hawasikiki vizuri kwa watu wanaofuatilia kesi hiyo na saa nyingine hata mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo wamekuwa wakilazimika kuwataka mashahidi hao watoe sauti ya juu ili waweze kuwasikia, lakini mahakama imeshindwa kuleta vipaza sauti katika uendeshwaji wa kesi hizo ambazo zinafuatiliwa kwa karibu na umma.

Tunashangazwa na kukerwa na hali Novemba 2008 kesi nane za wizi katika Akaunti ya EPA, zilipofunguliwa na kaunza kusikilizwa, ni mahakama hii ililalazimika kwenda Mahakama Kuu Kitengo cha Biashara na kuwachukua wale wataalamu waliokuwa wanakuja wakati kesi hizo zikisikilizwa wakiwa na Kompyuta na Vipaza sauti ambavyo vilikuwa vikirekedi mwenendo mzima wa kesi hizo kwa njia ya Elektonicki.

Kesi moja ya EPA ilikuwa ikiwakabili washtakiwa wawili, watatu hadi wa tano, sasa ajabu ni kwamba kesi hizi ambazo chanzo chake kinaelezwa ni chokochoko za udini hapa nchini, mhimili huu wa mahakama unashindwa kuleta vipaza sauti hivyo?

Hivi uongozi wa Mahakama ya Kisutu chini ya Hakimu Mkazi Elvin Mugeta, mlikuwa na uharaka gani wa kung’oa zile feni ambazo zilifungwa baada ya vyombo vya habari kupiga makelele wakati kesi za EPA zilipofunguliwa ndipo tukaona mahakama imenunua feni zile na kuzifunga,wakati kumbe bado hamjapata feni mpya za kuzifunga na na ukarabati bado haujamalizika ambapo hivi sasa ukarabati wa mahakama ya Kisutu unaonekana ni wakusuasua.
Nawala hizi si za uongozi wa Mahakama ya Kisutu, lawama hizi ziuendee uongozo wa mhimili wa mahakama nchini, ambao unafahama fika kesi hizo ambazo zinapewa uzito wa kipekee na mahakama yenyewe na serikali lakini inashindwa hata kuandaa mazingira mazuri ya waandishi wa habari, wanausalama wanaofika mahakamani hapo kwaajili ya kuudhulia kesi hiyo?

Tunafahamu kuwa mhimili huu umekuwa bingwa wa kulalamika kuwa haina fedha za kutosha, lakini mbona siku ya Law Day  sherehe hizo zinafana kwa kula na kunywa vitafuno, na fedha za ukarabati na kuweka samani katika baadhi ya ofisi za Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa zinatakowapi?

Hivi kulikuwa na ulazima gani wa ukaratabi wa mahakama ya Kisutu kuanzia nje kwa kujenga fensi, choo,kupaka rangi baadhi ya ofisi za mahakimu wakati mahakama za wazi zote tatu zikiwa hadi hivi sasa hazijaanza kukarabatiwa wakati mahakama hizo hasa ndiyo zinazotumiwa kuendeshea kesi?

Mbona mahakama za wazi za mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Mahakama Kuu Disheni ya Kazi, Kitengo cha Biashara na Mahakama ya Rufaa mbona zina feni na AC? Kwani hii Mahakama za wazi za Mahakama ya Kisutu zimekosa nini?Au ni kwasasabu wanaondesha kesi zile ni Mahakimu na siyo Majaji?

Jaji Mkuu Mohamed Chande Othman ni mwanasheria ambaye amepata fursa ya kufanyakazi ya Kisheria katika nyanja za kimataifa, atatunamuomba yale mazuri aliyokuwa akiyaona ule nje ya nchi ayalete kwenye mahakama zetu na kuhusu hali hii ya mahakama za wazi za Kisutu kuwa ni kama  maghofu tunaomba aingilie kati mara moja na kama fedha za ukarabati zimeisha basi aende serikalini akaombe fedha ukarabati uendelee ili wananchi wanaofika mahakamani hapo waweze kuketi sehemu nzuri na paendane na mahali panapoheshimiwa na wananchi kuwa ni mahali pakutolea haki.

Kwani hivi sasa baadhi ya kordo za mahakama hiyo na vyumba viwili vya wazi vya mahakama hiyo vilivyopo chini vimegeuka kuwa stoo ya kutunzia mambao yaliyoalibika ambayo yamejaza mavumbi makali,kuna uhaba wa mabenchi wa watu kukalia. Naimba mhimili wa mahakama uzinduke usingizini na uchukue hatua za dharula za kuboresha mahakama hizo za wazi.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Februali 21 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.