Header Ads

MKURUGENZI BoT AFUTIWA KESI

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam,imemuachiria huru aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Benki Kuu(BoT), Bosco Kimela aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilioni 104 ambaye amesota rumande kwa miezi nane sasa kwaajili ya kesi hiyo.


Mbali na Kimela aliyekuwa akikabiliwa na kesi hiyo washtakiwa wengine ni Mkurugenzi wa BoT,Simon Jengo, Naibu Mkurugenzi wa Fedha za Nje, Kisima Mkango, Kaimu Mkurugenzi na Mkurugenzi wa Huduma za Kibenki , Ally Bakari.Ambao nao walifutiwa kesi hiyo ila baada ya muda mfupi washtakiwa hao watatu walikamatwa na kufunguliwa kesi mpya ya matumuzi mabaya ya ofisi ya umma.

Uamuzi huo wa kumuachilia huru Kimela ulitolewa mwishoni mwa wiki na Hakimu Mfawidhi ,Joyce Minde ambapo alisema amefikia uamuzi wa kumuachiria huru mshitakiwa huyo kwasababu Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP) Eliezer Feleshi aliwasilisha mahakamani hapo hati ya kumfutia kesi hiyo hivyo mahakama hiyo inamuachiria huru.

“DPP amewasilisha hati ya kumfutia kesi Kimela peke yake hivyo mahakama hiyo haina pingamizi na hati hiyo ya DPP hivyo inamwachiria huru mshitakiwa wa tatu, Bosco Kimela “alisema Hakimu Mfawidhi Minde.

Septemba mwaka jana, washitakiwa hao walifunguliwa mahakamani wakikabiliwa na mashitaka manne matumuzi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ambapo kosa la kwanza walilifanya mwaka 2004, walichapisha noti zenye thamani y ash milioni 500.Shitaka la pili linafanana la kwanza ambapo wanadaiwa kutumia nyaraka hizo kumdanganya mwajiri ili aweze kuongeza gharama za uchaopishaji wa noti zenye thamani hiyo kwa mwaka 2005.

Aidha ,wakili alidai shtaka la tatu, ni la kutumia madaraka yao vibaya, ambapo watuhumiwa hao kwa pamoja wakiwa na nafasi zao, waliongeza gharama za uchapishaji wa noti zenye thamani ya Sh bilioni 1.4 mwaka 2007.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Mei 9 mwaka 2010

1 comment:

Anonymous said...

FUKUTO? Mbona hukusema? Mbona hujataarifu kwa njia sahihi? Fukuto?

ndimara

Powered by Blogger.