Header Ads

WAZIRI DAFTARI ASHINDA KESI

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemfutia kesi ya madai ya kashfa iliyokuwa ikimkabili Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,Dk.Maua Daftari kwasababu hati ya madai ina dosari za kisheria.


Uamuzi huo umetolewa na Jaji Agustine Mwarija ambapo alisema amefikia uamuzi wa kuifuta kesi hiyo kwasababu amekubaliana na pingamizi la awali lilowasilishwa mbele yake na wakili wa mdaiwa, Peter Swai liloiomba mahakama hiyo iifute kesi hiyo kwasababu mlalamikaji kupitia hati yake ya madai ameshindwa kuonyesha maneno ya nini alichokuwa akikilalamikia.

“ Mahakama imepitia kwa kina hoja za pande zote mbili na linakubaliana na pingamizi la wakili wa utetezi Peter Swai kwamba hati ya madai ina dosari za kisheria kwa mujibu wa hati hiyo ya mlalamikaji hajataja sababu ya kufungua kesi hiyo na na kwa mujibu Kanuni 11(a) amri ya VII ya Sheria ya Madai ya mwaka 2002 inamtaka mlalamikaji ataje sababu za kufungua kesi;

“Na kwa mujibu Amri ya VII Kanuni 11(a) ya Sheria ya Madai ya mwaka 2002 inaipa mahakama mamlaka ya kuifuta hati ya madai ambayo mamlalamikaji ajataja sababu ya kulalamika….na kwa mamlaka hayo niliyopewa na kanuni hiyo, naifutilia mbali hati ya madai kwasababu nimebaini ina dosari za kisheria na niaamuru mlalamikaji alimpe mdaiwa(Dk.Daftari)gharama zote alizozitumia kwaajili ya kuendesha kesi hiyo”alisema Jaji Mwarija.

Kesi hiyo ya madai Na.34 ya mwaka 2008 ilifunguliwa mahakamani hapo na mlalamikaji Fatma Salmin ambaye kwa mujibu hati hiyo ya madai iliyofutwa, alikuwa akidai kuwa mdaiwa ambaye ni Dk.Maua Daftari Novemba 14 mwaka 2007 katika ofisi za Bunge mjini Dodoma ,muda mfupi baada ya kupokea taarifa toka kwa wakili wake Peter Swai ambaye ofisi zake zipo Dar es Salaam, alizungumza na waandishi wa habari ambapo alikuwa akipinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, dhidi yake katika kesi nyingine ya madai Na.21 ya mwaka 1999 iliyofunguliwa na mlalamikaji Fatma Salim ambapo mahakama ilimtaka naibu waziri huyo alimpe fidia ya Sh milioni 100.

Kwa mujibu wa hati hiyo Salmin alidai kuwa mdaiwa(Dk.Daftari) siku hiyo alikuwa akihoji uhalali wa hukumu hiyo ile ya Mahakama Kuu katika kesi hiyo Na.21 ya mwaka 1999, na kwamba wakati akihoji alimuita yeye ni ‘tapeli mkubwa’na kuuongeza kuwa tamshi hilo limemletea limemshushia hadhi kwenye jamii na kumfanya onekane siyo mwaminifu hivyo akaomba mdaiwa amuliwe kumlipa sh milioni 500.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Mei 11 mwaka 2010

No comments:

Powered by Blogger.