Header Ads

MAHAKAMA KUU YAMNYIMA DHAMAMA HASSANOR






Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imemnyima dhamana Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA), Hassan Othman Hassan ‘Hassanoo’ na kuwapatia dhamana wenzake  sita wanaokabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wa shilingi bilioni 1.1 kwa kusafirisha pembe za ndovu toka Tanzania kwenda Hong Kong, China kwa maelezo kuwa  Hassanor anakabiliwa na kesi hiyo mpya wakati yupo nje kwa dhamana katika kesi ya Na. 209/2011 ya tuhuma za kula njama na kuiba tani 26 za shaba zenye thamani ya shilingi milioni 400, mali ya Kampuni ya Liberty Express Ltd ya Dar es Salaam.

 Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Zainabu Mruke ambapo alisema ombi hilo la kuomba lipatiwe dhamana liliwasilishwa na Hassanor na wenzake sita waliokuwa wakitetewa na mawakili wa kujitegemea Richard Rweyongeza ambaye jana hakutokea mahakamani, Majura Magafu, Mark Antony, Charles Semgalawa na Aliko Mwamunenge na mahakama hiyo ikayasikiliza maombi hayo Ijumaa iliyopita na upande wa Jamhuri uliokuwa ukiwakilishwa na mawakili waandamizi wa serikali Biswalo Mganga,Faraja Nchimbi,Lilian Itembo, Bernad Ikongora na Mutalemwa Kishenyi ambapo walikubali mwombaji wa 2-7 wapewe dhamana isipokuwa mwombaji wa kwanza Hassanor asipewe dhamana kwasababu emetenda kesi hiyo mpya ya uhujumu uchumi wakati yupo nje kwa dhamana kwa kesi wizi wa Shaba Na.209/2011.

Jaji Mruke alisema baada ya kupitia hoja za pande zote mbili amefikia uamuzi wa kukubaliana na hoja wakili wa serikali Mganga za kumnyima dhamana Hassanor kwasababu anakabiliwa na kesi mpya wakati yupo nje kwa dhamana ya kesi nyingine na 209/2011 kwamba kifungu cha 36 (4)(c) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi ya mwaka 2002, na kwamba kifungu hicho kinakataza mshtakiwa alitenda makosa mapya wakati yupo nje kwa dhamana ya kesi ya nyingine inayoendelea ,asipewe dhamana na mahakama.

“Mimi ni jaji ninayefuata sheria kwahiyo siwezi kupindisha sheria na kwa kuwa kifungu hicho kipo wazi kabisa basi mahakama hii inatamka kuwa imemnyima dhamana Hassanor kwa sababu anakabiliwa na kesi nyingine na inawapatia dhamana washitakiwa wengine ambapo kila mmoja atatakiwa kusalimisha hati yake ya kusafiria,asaini bondi au fedha taslimu sh.Milioni 50, asitoke nje ya mkoa bila kibali cha msajili wa Mahakama Kuu, na nyaraka hizo waziwasilishe Mahakama ya Kisutu na kisha ziletwe kwa Msajili wa Mahakama Kuu kwaajili ya kuakikiwa”alisema jaji Mruke.
Na kwa uamuzi huo wa mahakama, utamfanya Hassanor hivi sasa aendelee kusota gerezani na  awe anatokea gerezani kuja katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuudhulia kesi zake hizo mbili zinazomkabili.

 Hata hivyo waombaji hao walishindwa kutimiza masharti hayo jana wakarudishwa rumande.Baadhi ya ndugu na jamaa wa Hassanor waliokuwa wamefika mahakamani hapo kusikiliza uamuzi huo, waliuwa wakijifuta machozi kwa uzuni.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne , Desemba 25 mwaka 2012.


1 comment:

Anonymous said...

It's not my first time to pay a visit this web page, i am visiting this web page dailly and get nice information from here every day.Watch The Twilight Saga: Breaking Dawn - Part 2 2012
My web-site ... Watch The Twilight Saga: Breaking Dawn - Part 2 2012

Powered by Blogger.