Header Ads

LEMA ATOA SABABU 18 KUTETEA UBUNGE WAKE



Na Happiness Katabazi

ALIYEKUWA mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini(Chadema),Godbles Lema ,amewasilisha  sababu 18, kuiomba Mahakama ya Rufaa nchini, itengue  hukumu ya awali  iliyotolewa na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Aprili mwaka huu ambayo ilitengua ubunge wake.
 
Ombi hilo lilitolewa na mawakili wa mwomba rufaa(Lema),Method Kimomogoro na Tundu Lissu mbele ya jopo la majaji wa mahakama ya rufaa linaloongozwa na Natharia Salum Massati jana wakati rufaa hiyo iliyokatwa na Lema ilipokuja kwaajili ya kusikilizwa na ambapo ilisikilizwa na kunalizika.mawakili wa wajibu rufaa ni Aluthe Mugwai na Modest akida na wakili Msimamizi wa uchaguzi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni Timon Vitalis.

Wakili Kimomogoro , alieleza mahakama kuwa rufaa yao ya mteja wake ina jumla ya sababu 18 za kupinga hukumu iliyotolewa na jaji Gabriel Rwakibalila wa mahakama kuu kanda ya arusha ambayo ilitengua ubunge wake baada ya kumtia hatiani kwa makosa ya kutoa lugha za kumkashfu aliyekuwa mgombea mwenzie kwa tiketi ya CCM, Dk.Batrida Buriani na pia hukumu ile ilimfungia Lema kwa kipindi cha miaka mitano kugombea ubunge.

Alidai jaji Rwakibalila alijielekeza vibaya katika hukumu yake alivyosema kuwa kesi za uchaguzi hazitawaliwi na kanuni za sheria za Uingereza kwani kuna maamuzi ya kesi mbalimbali yalikwishatolewa na mahakama hiyo ya rufaa na mahakama kuu hapa nchini na yakuruhusu kesi za uchaguzi ziamliwe kwa kutumia kanuni za sheria za Uingereza.

Hoja ya ya pili wakili Kimomogoro alidai jaji rwakibalila alijielekeza vibaya kwa kuruhusu wajibu rufaa, wasitaje maneno kwenye hati yao ya madai ambayo walidai ni maneno ya udhalilishaji wa kijinsia na dini ambayo yalitolewa na mwomba Rufaa(Lema), kwenye kampeni dhidi ya Dk.Burian.

Hoja nyingine ni kwamba hakuna ushahidi wowote unaonyesha wajibu rufaa kweli ni walioandikishwa kupiga kura katika jimbo la arusha mjini.

Hoja ya nyingine ni ni kwamba jaji alikosea kisheria kusema kuwa mtu yoyote akiwemo mpiga kula ana haki ya kufungua kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo ambalo yeye ni mpiga kura na kuongeza kuwa wao wanaomba mahakama ya rufaa itamke kuwa wale wajibu rufaa (wapiga kula wa jimbo la arusha waliofungua kesi ile),walikuwa hawana haki ya kisheria ya kufungua kesi ile ya kupinga Ubunge wa Lema kwani mwenye haki ya kufungua kesi ile alikuwa Dk.Batrida kwani ndiye aliyekashfiwa na kuongeza kuwa mpiga kura hana haki ya kufungua kesi ya kupinga ubunge ule kwani haki zao hazikuvunjwa.

Aidha katika hoja nyingine alidai kuwa jaji yule hakutumia maamuzi ya kesi za mahakama rufaa wala vifungu vya sheria ambazo mawakili wa pande zote mbili ambazo kesi zilie waliziwasilisha mbele yake katika majumuisho yao ya mwisho ambapo maamuzi ya mahakama ya rufaa katika kesi zile mahakama ilisitiza kuwa nilazima kesi isitibitishwe bila kuacha mashaka yoyote na katika hukumu ile ya Jaji Rwakibalila imeacha mashaka mengi na ndiyo maana mwomba rufaa anadai jaji yule alikosea.

Baada ya Kimomogoro kuwasilisha hoja hiyo iliyodai jaji rwakibalila hakutumia maamuzi ya kesi zilizowasilishwa mbele yake na mawakili wa pnde mbili, Jaji Massati alisema alisikika akisema si lazima jaji au hakimu atumie kesi zilizowasilishwa mbele yake na mawakili katika kutoa uamuzi wake na kusababisha watu akuangua vicheko.

Hoja nyingine ni kwamba hukumu ile iliegemea katika ushahidi wa mdomo tu bila ya kuwepo ushahidi wa kuunga mkono ushahidi wa mashahidi wa mjibu rufaa, kwani mashahidi waliokuja kutoa ushahidi walidai kuwa walimsikia Lema katika mikutano ya kampeni akitoa maeno ya kumdhalilisha na kumkashfu Dk.Batrida lakini mashahidi hao walishindwa kuleta CD,mkanda wa video unaomuonyesha Lema akitoa matamshi yale.

“Tulimueleza jaji Rwakibarila kuwa mashahidi wa wajibu rufaa hawaamini na kwamba ushahidi wao ulikuwa ni wa mazingira lakini jaji katika hukumu yake hakuna sehemu alionyesha kukubali wala kukataa hoja yetu hii’alidai wakili Kimomogoro.

Wakili huyo alidai pia jaji yule alikosema alivyosema Lema ana bahati akukamatwa wala kushtakiwa kwa kitendo chake cha kutoa lugha za kashfa na udhalilisha katika mikutano ya kampeni za uchaguzi wa mwaka 2010 na kwamba mteja wake anaiomba mahakama rufaa itamke jaji rwakibalila alitamka neno hilo kwa bahati mbaya na kutamka kwake neno hilo ndiko kulikomsukuma kufikia uamuzi wa kumfungia Lema asigombee kwa kipindi cha miaka mitano.

“Kwa hoja hizo tulizoziwasilisha hapo juu, tunaiomba mahakama ya rufani nchini itengue hukumu ya Jaji Rwakibalila kwani ni haina vigezo wala hadhi ya kuifanya iwe hukumu na pia wanaiomba mahakama hiyo iwaamuru wajibu rufaa walipe gharama za uendeshaji wa kesi hiyo tangu ilipoanza mahakama kuu kanda ya arusha na sasa mahakama ya Rufaa”alidai wakili Kimomogoro.

Kwa upande wake wakili wa Mwanasheria Mkuu wa serikali na Msimamizi wa Uchaguzi jimbo la Uchaguzi, Timon Vitalis, yeye alidai sheria ya uchaguzi haiwaruhusu wapiga kura kufungua kesi ya kupinga ubunge wala wagombea ubunge,udiwani kutukana majukwaani na kwamba aliyepaswa kufungua kesi hiyo ya madai ya kukashfiwa ni Dk.Batrida na siyo wajibu rufaa ambao ni wapiga kura wa jimbo la Arusha na kwamba kesi hiyo ilikuwa njama za kisiasa ndani yake hali iliyosababisha watu kuangua vicheko mara kwa mara wakati akitoa hoja zake wakili huyo Mwandamizi wa serikali.

Akipangua hoja za mawakili hao wa mwomba rufaa, mawakili wa wajibu rufaa Mugwai na Akida walidai hukumu ile ni sahihi na haistahili kutenguliwa kwani imekidhi matakwa ya kisheria na kuomba mahakama hiyo ya juu nchini itupilie mbali rufaa ya Lema.

Wakili Mugwai alianza kwa kusema mawakili wa mwomba rufaa wa wanaipotosha mahakama walivyosema kuwa hakukuwa na uthibitisho wowote ulionyesha kuwa wajibu rufaa walikuwa ni wapiga kura wa jimbo la arusha mjini wakati ukurasa wa 10 katika hukumu ile zilitolewa namba za vitambulisho vya wapiga kura ambavyo ni vya wajibu rufaa na wakati vikitolewa mahakamani siku hiyo mawakili hao wa mwomba rufaa walikuwepo.

Kuhusu hoja ya jaji alijielekeza vibaya kusema kuwa sheria za uingereza hazitakiwi kutumika kuamua katika kesi za uchaguzi, wakili Mugwai alidai jaji rwakibalila yupo sahihi katika hilo kwani hata kifungu cha 1(2) cha sheria ya Uchaguzi sura ya 343 kinasema masuala yote ya uchaguzi yatashughulikiwa kwa kutumia sheria ya uchaguzi na kuongeza kuwa mawakili wa Lema wametumia kesi za mahakama ya rufaa zilizoamliwa kwa Sheria ya zamani ya uchaguzi ya mwaka 1985 wakati sheria hiyo ya uchaguzi imeishafanyiwa marekebisho na marekebisho ya mwisho hyalifanyika mwaka 2010 .

“Hata kifungu cha 2 (3) cha sheria ya Judicuture and application of Law(JALA), inakataza matumuzi ya sheria za nje kutumika kuamua kesi za uchaguzi wakati nchi yetu inayosheria ya mahususi ya uchaguzi kwaajili ya kuamua kwaajili ya kuamua kesi za uchaguzi na kwamba jaji alikuwa sahihi kusema hilo na pia jaji alikuwa sahihi kusema wajibu rufaa walikuwa na haki ya kufungua kesi ile na kwamba hoja hiyo ni butu”alidai wakili Mugwai.

Hata hivyo alipinga hoja ya mawakili wa Lema iliyodai jaji yule katika hukumu yake hakutumia kesi walizoziwasilisha mbele yake, ambapo alidai jaji yule katika hukumu yake alitumia baadhi ya kesi walizoziwasilisha mbele yake na kwamba hata hivyo jaji ana mamlaka ya kuchuja kesi anazotaka kuzitumia.

Kuhusu hoja ya kuwepo kwa ushahidi wa kuunga mkono, wakili huyo alidai hoja hiyo haina mantiki kwani aliyewaambia katika kesi ile ulikuwa ukiiitaji ushahidi wa kuunga mkono nani kwani mashahidi wote 14 walifika mahakamani na kutoa ushahidi wao ambapo kila shahidi alikuwa akitoa ushahidi unaounga mkono ushahidi wa mashahidi wengine.

Akijibu hoja ya kwamba hukumu ile iliegemea kwenye ushahidi wa mazingira tu, wakili Mugwai alikanusha hoja na kusema hakukuwepo na ushahidi wa mazingira kwani mashahidi waliomsikia Lema akitoa maneno yale ya kashfa kwenye mikutano ya adhara walifika mahakamani hapo na kutoa ushahidi wao ambapo walisema walimwona Lema akitoa maneno yale ya kashfa.

Hata hivyo wakati wakili Mugwai akiwasilisha hoja zake kuba baadhi ya watu wanaodaiwa ni wafuasi wa CHADEMA ambao walijazana ndani ya chumba cha mahakama walimfyonza na kuwa wakitoa vicheko hali iliyosababisha wakili huyo kuwaeleza majaji wawathibiti watu wenye tabia hiyo kwani mawakili wa Lema walipokuwa wakiwasilisha hoja zao walikuwa awafyonzwi ila yeye anavyonza na kutaka wale ambao wanakerwa nay ale anayoyawasilisha wavyumile hata hivyo majaji hawakuchukua hatua zozote kuhusu ombi hilo.

Badaa ya mawakili hao kumaliza kuwasilisha majumuisho yao katika rufaa hiyo Dar es Salaam jana saa tisa alasiri ambapo rufaa hiyo ilianza kusikilizwa tangu saa tatu asubuhi ambayo ilikuja kwaajili ya kusikilizwa ,majaji hao waliarisha shauri hilo na kusema tarehe ya kutolewa kwa uamuzi wa rufaa hiyo itatolewa kwa njia ya maandishi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Desemba 5 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.