Header Ads

UPELELEZI KESI YA PAPA MSOFFE BADO




Na Happiness Katabazi

UPANDE wa Jamhuri katika kesi ya mauaji inayomkabili mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam,    Marijani Abdubakari Msoffe(50) maarufu kwa jina la “Papa Msoffe chuma cha reli akishiki kutu’   ’ jana umeieleza  tena Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Wakili Mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka mbaele ya Hakimu Mkazi Agnes Mchome alianza kwa kuikumbusha mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kwamba wanaomba tarehe ya kutajwa.

Hakimu Mchome alikubaliana na ombi hilo na akaiarisha kesi hiyo hadi Januari 9 mwaka huu,itakapokuja kwaajili ya kutajwa na ninaamuru mshtakiwa arejeshwe gerezani.

Agosti 10 mwaka huu, Msoffe ndiyo alifikishwa mahakamani hapo kwa mara ya kwanza ambapo wakili wa Kweka alidai kuwa mshtakiwa huyo ana kabiliwa na kosa la moja la kuua kwa kukusudia ambalo ni kinyume na kifungu cha  196 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002. Kuwa Novemba 6 mwaka 2011 huko Magomeni Mapipa Papa Msoffe anayetetewa na wakili wa kujitegemea Majura Magafu alimuua Onesphory Kituli.

Hata hivyo Hakimu Mchome alimtaka Msoffe asijibu chochote kwasababu mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo na kwamba ni Mahakama Kuu ndiyo yenye mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Desemba 28 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.