Header Ads

UAMUZI KESI YA MARANDA WAKWAMA

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilishindwa kutekeleza ahadi yake ya kuutoa uamuzi katika kesi ya wizi wa Sh bilioni 2.2 katika akaunti ya madeni ya Nje katika Benki Kuu, inayomkabili Kada wa CCM, Rajab Maranda na mpwa wake Farijala Hussein wa ama washtakiwa hao wanakesi ya kujibu au la.


Julai 4 mwaka huu, Jaji Fatma Masangi aliyekuwa akisaidiwa na Hakimu Mkazi Projestus Kahyoza na Catherine Revocati walijigamba mahakama hapo kuwa jana ndiyo wangekotoa uamuzi wa ama washtakiwa wanakesi ya kujibu au laa ikiwa ni saa chache siku hiyo wakili wa serikali Arafa Msafiri kumaliza kuwasilisha majuisho yake ambayo yaliomba mahakama hiyo iwaone washtakiwa wote ambao wanatumikia kifungo cha miaka mitano jela kwa makosa ya kuibia BoT, sh bilioni 1.6.

Kesi hiyo jana ilikuja mbele ya Hakimu Mkazi Ritha Tarimo ambapo alisema kuwa amepata maelekezo toka kwa jopo hilo kuwa hawataweza kutoa uamuzi huo jana na akaiarisha kesi hiyo hadi Julai 25 mwaka huu, ambapo siku hiyo ndipo jopo hilo litatoa uamuzi wa ama washtakiwa wanakesi ya kujibu au.

Katika kesi hii ya wizi wa sh bilioni 2.2, washtakiwa hao wanaotetewa na wakili Majura Magafu wanakabiliwa na makosa ya wizi, kughushi nyaraka na kisha kujipatia kiasi hicho cha fedha kutoka katika akaunti ya EPA.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Julai 19 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.