Header Ads

JUBILEE YA MIAKA 50 YA KITIVO CHA SHERIA UDSM


*WALIMU,WANAFUNZI KUKUTANISHWA

Nappiness Katabazi
KITIVO cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,ambacho hivi sasa kinaongozwa na mwandishi wa habari na mwanasheria mbobevu , Profesa Paramaganda John Kabudi ni kitivo maarufu ndani na nje ya nchi yetu.

Umaarufu wake unatokana na umahiri wake wa kuwapika wasomi wengi wa upika wasomi wengi wa sheria ambao hivi sasa wameshika nyadhifa za juu serikalini, sekta binafsi na taasisi za kimataifa karibu kote duniani.

Lakini umaarufu mwingine wa kitivo hicho ni kwamba Kitivo hicho ndiyo kitivo cha kwanza kuanzishwa Oktoba 25 mwaka 1961 na ilipofika mwaka 1970 kitivo hicho ndicho kilichopelekea kuanzishwa rasmi kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Katika makala hii, Mkuu wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Kabudi anaanza kwa kusema kuanzishwa kwa kitivo hicho ni alama moja ya wapo ya uhuru wa Tanganyika. Kwani kitivo kilianzishwa kwanza halafu Desemba 9 mwaka 1961 Tanganyika ikapata uhuru wake.

“Ndiyo maana nasema kuanzishwa kwa kitivi hiki ni ala moja wapo ya uhuru wa Tanganyika “alisema Profesa Kabudi ambaye ni mbobevu katika sheria za mazingira na mwandishi wa Habari Kitaaluma.

Pofesa Kabudi anasema Oktoba 25 mwaka 1961 , Baba wa Taifa, Mwalimu Julias Nyerere alisema maneno yafuatayo alipokubali kuanzishwa kwa kitivo hicho cha Sheria;

“…my Government is so pleased that the law faculty is open even before Independence Day. Dar es Salaam..is the only place where East Africans can get training in law. Its is not by accident that we started with a law college. An essential part of our national philosophy must be a legal profession of great integrity which not only knows the formalities of law but also understands the basic philosophy which underlies our society”

Kwa tafsiri yangu isayo rasmi kuhusu nukuu hiyo , mwalimu Nyerere alisema uamuzi wake wa kuruhusu kuanzishwa kwa kitivo hicho haukuwa ajali , ulikuwa ni uamuzi sahihi kwani Dar es Salaam, ndiyo ilikuwa ni eneo pekee la kwa wananchi wa Jumuiya ya nchi za Afrika Mashariki kupata mafunzo ya sheria .Na kwamba taifa lilikuwa likiitaji kuwa na wasomi wa sheria ambao wanasimamia maadili na miiko ya sheria.

Akielezea historia ya kitivo hicho na maandalizi ya kuazimisha Jubilei ya dhahabu ya miaka 50 , anasema Kitivo hicho ni Kitivo cha kwanza kuanzishwa hapa Tanzania na nchini za Jumuiya ya Afrika Mashariki na ndicho kitivo kilichosababisha kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Profesa Kabudi anasema kwanza kabisa anaanza kwa kuwataka waadhili wastaafu, wahitimu wa fani ya sheria waliowahi kuhitimu kozi ya cheti na shahada mbalimbali za fani ya sheria katika kitivo hicho, wananchi na viongozi mbalimbali kushiriki kwenye maazimisho hayo yatakayofanyika chuo hapo.

Profesa Kabudi anasema Kitivo cha Sheria ndiyo kilikuwa kitivo cha kwanza kanzishwa katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati pia ndiyo kitivo cha kwanza kuanzishwa UDSM Oktoba 25 mwaka 1961 ambacho kuanzishwa kwa kitivo hicho ambacho kuanzishwa kwa kitivo hicho ndiyo kikaja kusababisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuzaliwa mwaka 1970.

Profesa Kabudi ambaye ni Mwenyekiti Mkuu wa Kamati ya Maandalizi ya maadhimisho hayo ya nusu karne anasema wiki ya maazimisho hayo yataanza rasmi Oktoba 17-25 mwaka huu na kwamba maazimisho hayo wameyapatia jina la ( Golden Jubilee Celebrations of The Faculty of Law October 25,1961-October 25,2011).

Anasema Kamati ya maandalizi ya maazimisho hayo inaongozwa na yeye mwenyewe, Profesa Gamalie Mgongo Fimbo, Profesa Leonard Shaidi, Profesa B.Rutinwa, Profesa F.Luoga, Dk Khoti Kamanga, Asina Omari, Ebenezer Mshana ,Consolata Lyimo, Reginald Mhango, Joaqine de Mello.

Aidha anasema siku hiyo ya kilele cha Jubilee ya dhahabu ya miaka 50,yatafanyika mahafali ya wanafunzi wa sheria wa kitivo tu katika ngazi ya cheti, shahada ya kwanza, ya pili na shahada ya uzamivu(PhD) ukilinganisha na mahafali ya miaka iliyopita.

Ambapo katika wiki hiyo ya maadhimisho kutafanyika kongamano mdahalo, kujadili mada ya Ukatiba na ujenzi wa Katiba mpya ya Tanzania, kusikiliza hotuba za wanafunzi 12 wa kwanza waliohitimu sheria katika kitivo hicho, pia hotuba zitakazotolewa waadhili wa kwanza wa kitivo hicho, pia wasomi wa sheria mbalimbali ambao wamewai kusomea fani hiyo katika chuo kikuu cha UDSM.

“Kitivo cha Sheria kimepata kutoa wasomi mbalimbali wa fani hiyo ambao leo hii wanafanyakazi katika ngazi mbalimbali duniani na Oktoba 25 mwaka huu, kitivo cha Sheria ndiyo kinatimiza miaka 50 tangu kilipoanzishwa na tunawataka umma utambue uanzishwaji wa kitivo hicho ni harama ya kwanza ya uhuru wa nchi yetu ambapo Desemba 9 mwaka huu, taifa linaazimisha miaka 50 ya uhuru hivyo utaona kitivo kilianza halafu miezi mitatu baadaye taifa likapata uhuru”alisema Profesa Kabudi.

Baadhi ya wanafunzi waliowai kusoma sheria katika kitivo hicho ni hivi leo wameshika nyadhifa za juu za kitaifa na kimataifa, Waziri Mkuu wa sasa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu Mstaafu, Jaji Joseph Warioba, Jaji Mkuu Othaman Chande, majaji wakuu wastaafu Agustino Ramadhani,Barnabas Samatta, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa, Dk.Edward Hosea na Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP), Elizer Feleshi.

Naibu Waziri Mkuu wa kwanza na Waziri wa wizara ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wa serikali ya Uganda, Eriya T.Kategaya, Jaji Mkuu wa Kenya Evan Johnston Gicheru,Jaji Mkuu wa Uganda, Benjamin J.Odoki,Jaji Mkuu wa Zanzibar, H.M.Hamid,marehemu jaji Mkuu wa Kenya
ZZ.S. Chesoni .

Majaji wanawake wa mahakama ya rufaa ya Tanzania, ambao walihitimu fani ya sheria katika kiito hicho ni, Jaji Eusebio Mnuo, Engela Kileo,Nataria Kimaro, Sauda Mjasiri na Katherine Oriyo.
Wanasheria wakuu waliowakusoma fani ya sheria katika kitivo hicho ni Mwanasheria Mkuu wa Kenya, Amos Wako, Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, Jaji Frederick Werema, Mwanasheria Mkuu wa zamani wan chi ya Gambia, H.B. Jallow, wanasheria wakuu wastaafu wa hapa nchini, Andrew Chenge na Johnson Mwanyika na mwanasheria mkuu wazamani wa Zanzibara Iddi Pandu Hassan.
Aliyekuwa Spika wa Bunge la Tanzania, Samwel Sitta na Spika wa zamani wa Bunge la Uganda, marehemu J.F.W. Wapakabulo.
Watumishi katika taasisi za kimataifa ambao walipikwa na kitivo cha Sheria ni Dk. Asha-Rose Migiro ambaye kwasasa ni Naibu Katibu Mkuu wa (UN), Lee C.Muthoga, S.h.Sekule ambao ni Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya mauaji ya Rwanda na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa mahakama hiyo ya mauji ya Rwanda S.H.Sekule na Balozi James Kateka ambaye kwasasa ni Jaji wa Mahakama ya Kimataifa inayoshughulikia masuala ya bahari.
Waziri wa Elimu ya Juu wa Malawi Peter Mutharika, Waziri wa Wizara ya Ulinzi A.Mbabazi na Waziri Sheria ya Katika wa Kenya Mutula Kilonzo.
Wanafunzi waliowai kusoma kitivo na mwisho wa siku wakawa wakuu wa majeshi yetu hapa nchini ni Meja Jenerali mstaafu, L.G.O. Mang’enya ambaye pia alikuwa jaji wakili wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi(JWTZ), Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema na mkuu wa jeshi la polisi mstaafu, Haruni Mahundi na Mkuu wa Jeshi la Magereza Mstaafu O.E. Malisa.
Wahitimu wengine ambao wamewahi kuwa makatibu wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki Amanya Mushenga na Juma Mwapachu.
Wahitimu wengine ambao wamekuwa na nyadhifa za wenyeviti, maofisa watendaji wakuu katika makambuni na mashirika mbalimbali ni Mwenyekiti wa Benki ya Barclays(Kenya), Francis Okoma-Okello, Deo Mwanyika ambaye ni Makamu wa Rais wa Barrick Gold Afrika, aliyekuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa Dar es Salaam,Dk.Hamis Kibola na afisa Mtendaji Mkuu wa Tanzania Breweries Ltd na Shirika la Maendeleo Tanzania(NDC), Anold Kilewo.

Mbali na majina wahitumu hao, Profesa Kabudi anasema tangu kitivo hicho kianzishwe, wasomi mbalimbali wa sheria waliwai kuchaguliwa kuwa wakuu wa kitivo hicho.

Mkuu wa kwanza kitivo hicho ni Profesa Arther Brain Weston,wapili ni Profesa y.Ghai , watatu D.Bishota,wa nne ni P.L.U. Cross,wa tano ni Profesa J.L Kanywanyi, wa sita ni Profesa Gamaliel Mgongo Fimbo, wa saba ni Profesa Costa Ricky Mahalu, wa nane, Profesa Zebron Stephen Gondwe, wa tisa ni Dk.Wilbert Kapinga,wa kumi ni Dk.Sengondo Mvungi, wa 11 ni Profesa Jaji Ibrahim Hamis Juma, wa 12 ni Profesa Sifuni Mchome na Profesa Kabudi ambaye ndiyo Mkuu wa kitivo hicho kikongwe kwa sasa.

Profesa Kabudi ambaye amewahi kuwa Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa Gazeti la Uhuru na Mzalendo, anasema maandalizi ya maamizisho hayo ambayo yatausisha wasomi mbalimbali wa sheria toka pande zote za dunia yamekamilika.

Na kwamba anawaomba wasomi wa fani hiyo na umma kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika wiki hiyo kuudhulia maazimisho hayo kwani watajifunza mengi hasa ukizingatia kitivo hicho ndiyo kitivo cha kwanza kaunzishwa na kitivo hicho ndiyo kilichopelekea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzishwa.

0716 774494
www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Julai 21 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.