Header Ads

UAMUZI KESI YA SAMAKI WA MAGUFURI JULAI 14/2011

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imesema Julai 14 mwaka huu itatoa uamuzi wake wa ama kuwaona washtakiwa katika kesi ya Uvuvi haramu ukanda wa Tanzania katika bahari ya Hindi inayowakabili raia 36 wa kigeni ama wanakesi ya kujibu au la.

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Jaji Agustine Mwarija muda mfupi baada ya wakarimani wanne wa lugha za kigeni katika kesi hiyo kumaliza kutoa tafsiri ya hoja zilizowasilishwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali Biswalo Mganga na Prosper Mwangamila kumaliza kuwasilisha majumuisho yao ambayo yaliiomba mahakama hiyo iwaone washtakiwa wote wanakesi ya kujibu kwani wanaamini wameweza kuleta ushahidi thabiti ambao utaishawishi mahakama iwaone washtakiwa wanakesi ya kujibu.

“Nimesikiliza hoja za pande zote mbili zilizowasilishwa na mawakili wa pande zote mbili,hivyo naairisha kesi hii hadi Julai 14 mwaka huu ambapo siku hiyo nitakuja kutoa uamuzi wa kuwaona washtakiwa wana kesi ya kujibu au la”alisema Jaji Mwarija.

Juni 16 na 17 mwaka huu, mawakili wa utetezi Ibrahim Bendera na John Mapinduzi waliwasilisha majumuisho ya kesi hiyo ambayo waliiomba mahakama hiyo iwaone washtakiwa wote hawana kesi ya kujibu kwasababu upande wa Jamhuri umeleta ushahidi dhaifu na kwamba wakati wateja wao wanakamatwa Machi 7 mwaka 2009, Tanzania haikuwa na Sheria ya Uvuvi wa Samaki katika kina kirefu cha Bahari(The Deep Sea Fishing Authority Regulation, 2009).

Wakati Juni 20 na 21 mwaka huu, mawakili wa serikali Mganga na Mwangamila nao waliwasilisha majumuisho yao kwa njia ya mdomo ambao walijigamba kuwa wameweza kuthibitisha kesi na hivyo wanaiomba mahakama iwaone washtakiwa wote wanakesi ya kujibu.Ambapo jana wakarimani wanne wanaotafsiri yote yanayozungumzwa mahakamani hapo kwa lugha za washtakiwa hao walimaliza kutoa tafsri ya majumuisho hayo ya serikali.

Machi 2009 ilidaiwa na upande wa Jamhuri kuwa washtakiwa hao wanakabiliwa na makosa matatu ambayo kufanya uvuvi katika bahari ya Hindi ukanda wa Tanzania bila leseni na pia kufanya uharibifu wa mazingira katika eneo la ukanda huo.

Chanzo:Happiness Katabazi Juni 25 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.