Header Ads

WAHITIMU UDSM WAHAMASISHWA KUSHIRIKI JUBILEE YA MIAKA 50


Na Happiness Katabazi

KITIVO cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimewataka waadhili wastaafu, wahitimu wa fani ya sheria waliowahi kuhitimu kozi ya cheti na shahada mbalimbali za fani ya sheria katika kitivo hicho kushiriki kwenye maadhimisho ya jubilee ya miaka 50 yatayofanyika Oktoba 25 mwaka huu, chuoni hapo.


Mkuu wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Paramaganda Kabudi alitoa wito huo jana katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jana chuoni hapo ambapo alisema lengo la mkutano huo wa waandishi wa habari ni kuitambulisha Kamati ya Maandalizi ya maazimisho ya miaka 50 ya kitivo hicho na jinsi maadhimisho hayo yatakavyoazimishwa.

Profesa Kabudi alisema Kitivo cha Sheria ndiyo kilikuwa kitivo cha kwanza kanzishwa katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati pia ndiyo kitivo cha kwanza kuanzishwa UDSM Oktoba 25 mwaka 1961 ambacho kuanzishwa kwa kitivo hic ambacho kuanzishwa kwa kitivo hicho ndiyo kikaja kusababisha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuzaliwa mwaka 1970.

Kabudi ambaye ni Mwenyekiti Mkuu wa Kamati ya Maandalizi ya maadhimisho hayo ya nusu karne alisema wiki ya maazimisho hayo yataanza rasmi Oktoba 17-25 mwaka huu, ambapo katika wiki hiyo ya maadhimisho kutafanyika kongamano mdahalo, kujadili mada ya Ukatiba na ujenzi wa Katiba mpya ya Tanzania, kusikiliza hotuba za wanafunzi 12 wa kwanza waliohitimu sheria katika kitivo hicho, pia hotuba zitakazotolewa waadhili wa kwanza wa kitivo hicho, pia wasomi wa sheria mbalimbali ambao wamewai kusomea fani hiyo katika chuo kikuu cha UDSM.

“Kitivo cha Sheria kimepata kutoa wasomi mbalimbali wa fani hiyo ambao leo hii wanafanyakazi katika ngazi mbalimbali duniani na Oktoba 25 mwaka huu, kitivo cha Sheria ndiyo kinatimiza miaka 50 tangu kilipoanzishwa na tunawataka umma utambue uanzishwaji wa kitivo hicho ni harama ya kwanza ya uhuru wa nchi yetu ambapo Desemba 9 mwaka huu, taifa linaazimisha miaka 50 ya uhuru hivyo utaona kitivo kilianza halafu miezi mitatu baadaye taifa likapata uhuru”alisema Profesa Kabudi.

Aidha alisema maandalizi ya maamizisho hayo ambayo yatausisha wasomi mbalimbali wa sheria toka pande zote za dunia yamekamilika na kwamba wanawaomba wasomi wa fani hiyo na umma kwa ujumla kujitokeza kwa wingi katika wiki kuudhulia maazimisho hayo kwani watajifunza mengi hasa ukizingatia kitivo hicho ndiyo kitivo cha kwanza kaunzishwa na kitivo hicho ndiyo kilichopelekea Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzishwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatatu, Julai 11 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.