Header Ads

KESI YA MAHALU,MWENZAKE YAPIGWA KALENDA

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kwa mara nyingine jana ilishindwa kuanza kusikiliza utetezi wa aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Grace Martin wanaokabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi wa zaidi ya Euro milioni mbili kwasababu mawakili wa utetezi walikuwa na udhuru.


Wakili Mwandamizi wa Serikali Ponsian Lukosi mbele ya Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Elvin Mugeta aliambia mahakama kesi hiyo ilikuja jana kwaajili ya washtakiwa hao kuanza kujitetea na kwamba upande wa jamhuri upo tayari kwaajili ya kuendelea na kesi hiyo.

Lakini wakili wa utetezi mmoja Beatus Malima aliambia mahakama hiyo kuwa upande wa utetezi jana haupo tayari kwaajili ya kuendelea na kesi hiyo kwasababu wakili kiongozi wa utetezi Mabere Marando yupo Mahakama ya Rufani kuudhulia kesi nyingine na Alex Mgongolwa anaugua hivyo wanaomba kesi hiyo iarishwe.

Ombi hilo lilikubaliwa na hakimu huyo ambaye aliairisha kesi hiyo hadi Agosti 5 ba 26 mwaka huu, ambapo washtakiwa hao watapanda kizimbani kutoa ushahidi wao.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi,Julai 9 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.