Header Ads

KORTI YAAMURU RAMA AKAPIMWE AKILI

MAHAKAMA Kuu Dar es Slaam imeamuru mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya mauaji ya kukusudia, Ramadhani Selemani, aliyekutwa akitafuna kichwa cha mtoto eneo la Hospitali ya Taifa Muhimbili, akapimwe akili.

Ramadhani na mama yake mzazi Hadija Ally wanashtakiwa kwa kosa la mauaji ya kukusudia ya mtoto Salome Yohana (3) eneo la Tabata jijini Dar es Salaam.
Kesi hiyo ilitarajiwa kuanza kusikilizwa kwa washtakiwa kusomewa maelezo ya awali ya mashtaka yao (PH) lakini ilishindikana baada ya wakili wa washtakiwa hao Yusufu Shehe kuiomba mahakama iamuru mshtakiwa huyo akapimwe akili.

Mheshimiwa Jaji, kulingana na ushahidi wa kesi hii, chini ya kifungu cha 219 (1) Sura ya 20 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), inaiomba mahakama yako iruhusu mshtakiwa wa kwanza akapimwe akili zake kwanza.

Alisema ameamua kutoa ombi hilo ili kujiridhisha na utimamu wa akili za mshtakiwa kwanza kabla ya kuanza usikilizwaji wa kesi hiyo kulingana na kumbukumbu za maelezo ya ushahidi ulioko.

Hata Hivyo Wakili Shehe alibainisha kuwa anakusudia mshtakiwa huyo apimwe akili kwa wakati ule tu aliotenda kosa analoshtakiwa kwalo na si kwa wakati mwingine wowote.
Wakili wa upande Jamhuri (mashtaka) Dionisia Saiga akisaidia na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga, alisema kuwa kulingana na ushahidi wa kesi hiyo hata wao hawana pinagmizi dhidi ya ombi la wakili wa utetezi kwa mshtakiwa huyo kupimwa akili.

Baada ya kusikiliza pande zote Jaji Karua alikubaliana na ombi hilo la wakili wa utetezi na kutoa amrim rasmi mshtakiwa huyo akapimwe akili kabla ya kuendelea na usikilizwaji wa kesi hiyo.

Hivyo Jaji Karua aliahirisha kesi hiyo hadi itakapopangwa tarehe nyingine ya kuendelea nayo katika awamu nyingine ya vikao vya mahakama vya kesi za jinai.
Kabla ya kutoa ombi la mshtakiwa kupimwa akili, Wakili Shehe aliomba mahakama iliamuru atafutwe wakili mwingine kwa ajili ya kumtetea mmoja wa washtakiwa katika kesi hiyo.
Wakili Shehe ambaye alikuwa akiwatete washtakiwa wote wawili katika kesi hiyo alisema kwa mazingira ya kesi hiyo na ushahidi yakiwemo maelezo ya washtakiwa asingeweza kuendelea kuwatetea wote.
Moja ya maelezo ambayo yalimsukuma Wakili Shehe aombe atafutwe wakili mwingine kwa ajili ya kumtetea mmoja wa watuhumiwa hao, ni yale ya mshtakiwa wa kwanza, Ramadhani kumsukumia mama yake mzigo kuwa ndiye aliyefanya mauaji hayo.

Hata hivyo mama yake Ramadhani naye anakana tuhuma hizo akidai kuwa siyo yeye aliyemuua mtoto huyo, maelezo ambayo pia yanaashiria kuwa anamwachia mzigo huo mwanaye Ramadhani, aliyekutwa na kicha cha mtoto huyo.

Mahakama ilikubaliana na ombi hilo la wakili wa utetezi na kuamuru atafutwe wakili mwingine kwa ajili ya kumtetea mshtakiwa mwingine, kabla ya kesi hiyo haijapangiwa tarehe nyingine ya kuanza kusikilizwa.

Washtakiwa hao wanadaiwa kutenda kosa hilo
Ramadhan alikamatwa na mlinzi wa Hospiltali ya Muhimbili Furgence Michael akiwa na kichwa cha mtoto huyo kikiwa kimesukwa nywele, April 26, 2008, akidai kuwa alikuwa anampelekea zawadi muuguzi mmoja wa hospitali hiyo.Kichwa hicho kilikuwa ndani ya mfuko wa nailoni aina ya Rambo huku akikitafuna hadharani huku akidai kuwa alikuwa amezoea kula nyama za watu yeye na bibi yake.

Tukio hilo liliwafanya wafanyakazi wa hospitali hiyo na watu wengine waliofika hospilatini hapo kwa sababu mbalimbali kuacha shughuli zao na kwenda kumshuhudia kijana huyo akitafuna kichwa hicho

Hata hivyo walimweka chini ya ulinzi mkali, na kutoa taarifa polisi ambapo baada ya polisi kufika walimuhoji akadai kuwa alikuja na bibi yake anayeishi makaburi ya Jeti Lumo na kwa bahati mbaya wamemuacha na wao wamepaa na ungo.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Kanda Maalum Dar es Salaam, Faustine Shilogile alisema kuwa Ramadhan amekuwa akipatikana kwenye matukio tofauti ya ajabu na wanaendelea kumchunguza kutokana na matukio hayo.
Kabla ya mwili na kichwa chake kupatikana mahali tofautotofauti mtoto Salome alipotea muda wa saa 2 usiku April 25 akiwa nyumbani kwa shangazi yake Furaha Majani (28), anayeishi Segerea kwa Bibi.

Mtoto huyo alifika kwa shangazi yake hapo akiwa na wazazi wake, baba yake Yohana Majani na mama yake Upendo Datsun, wakazi wa Kimara, kwa ajili ya kumtembelea shangazi yake huyo.Baada ya kubaini kuwa mtoto huyo alikuwa amepotea katika mazingira ya kutatanisha walitoa taarifa kituo cha polisi baada ya kumtafuta kwa ndugu na jamaa bila mafanikio.Baadaye kiwiliwili cha mtoto huyo kiliokotwa ndani ya shimo la choo kikiwa kimekatwa kichwa na wazazi walitambua kuwa ni kiwiliwili cha mtoto wao.Baada yakupata taarifa za Ramadhani kukamatwa Muhimbili akiwa na kichwa cha mtoto, wazazi hao walifika hospitalini hapo na walikitambua kichwa hicho kuwa ni cha mtoto wao.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima Daima, Oktoba 5 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.