Header Ads

HAKIMU AGOMA KUJITOA KESI YA MARANDA

Na Happiness Katabazi

JOPO la Mahakimu Wakazi watatu wanaosikiliza kesi ya wizi wa Sh bilioni 3.3 katika Akaunti ya Madeni ya Nje(EPA) inayomkabili Rajabu Maranda na wenzake wanne katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam,limetupilia mbali ombi la washtakiwa wawili Maranda na Farijala Hussein lilokuwa likiomba Hakimu Mkuu Mfawidhi Elvin Mugeta anayeunda jopo hilo ajitoe kwenye kesi hiyo.


Wanaounda jopo hilo ni Jaji Beatrice Mutungi, Jaji Karua na Hakimu Mkazi Mugeta.

Uamuzi huo ulitolewa jana na jopo hilo ambalo lilisema uamuzi huo unatokana na ombi lilowasilishwa juzi na wakili wa washtakiwa hao Majura Magafu ambaye ambalo lilimwomba Mugeta ajitoe kwenye kesi hiyo kwani hatatenda haki kwakuwa Mugeta ndiye aliyekuwa akiunda jopo la mahakimu wakazi Saul Kinemela na Focus Bampikya ambao Mei 25 mwaka huu, walihukumu washtakiwa hao Maranda, Farijala kifungo cha miaka mitano jela baada ya kupatikana na hatia kujipatia sh bilioni 1.8 kwa njia ya udanganyifu kutoka Benki Kuu na kwamba mashahidi waliotoa ushahidi kwenye kesi ya awali ndiyo wanaokuja kutoa ushahidi kwenye kesi hiyo ya sasa.

Jaji Karua alisema wamefikia uamuzi huo kwasababu ombi hilo halina msingi wa kisheria kwani kesi hiyo inaendesha kwa mtindo wa jopo hivyo Hakimu Mugeta peke yake hawezi kulishawishi jopo hilo kutoa uamuzi anaoutaka yeye bila kukubaliana na jopo hilo na hivyo akaiarisha kesi hiyo hadi Novemba 25 itakapokuja kwaajili ya kutajwa na itakuja kwaajili Februali 13-17 mwaka 2011 kwaajili ya kuendelea kusikilizwa.

Mbali na Maranda na Farijala washtakiwa wengine ni maofisa wa BoT, Sophia Lalila na Iman Mwakosya, Ester Komu na mfanyabiashara Ajay Somani ambao wanadai wakula njama na kuibia BoT jumla ya Sh bilioni 3.3.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Oktoba 26 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.