Header Ads

MAHAKAMA INA NINI NA KESI YA MRAMBA?


Na Happiness Katabazi

JANUARI 20 mwaka huu, upande wa Jamhuri katika kesi ya matumuzi mabaya na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 11.7 inayomkabili Waziri wa Fedha wazamani, Basil Mramba na Waziri wa Nishati na Madini na Nishati wa zamani Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonja,walifunga kesi yao.

Washtakiwa hao wanatetewa na mawakili wa kujitegemea Hurbet Nyange, Elisa Msuya ,Peter Swai na Profesa Leonard Shaidi.Wakati upande wa Jamhuri unawakilishwa na Wakili Kiongozi wa Serikali Stanslaus Boniface anayesaidiwa na Fredrick Manyanda na Ben Lincolin.

Kesi hiyo ambayo inasikilizwa kwa mtindo wa jopo.Jaji John Utamwa ndiye anaongoza jopo la Mahakimu wakazi kusikiliza kesi hiyo ambapo anasaidiwa na Sam Rumanyika na Saul Kinemela.

Binafsi mimi nimiongoni mwa waandishi wa habari wachache hapa nchini ambao nimezama katika kuripoti habari za mahakamani kikamilifu.Hivyo kuhusu kesi hii ya Mramba nadiriki kusema nimepata fursa ya kuudhulia kesi hii tangu ilipofunguliwa rasmi Novemba 25 mwaka 2008 .

Ambapo Mramba na Yona ndiyo walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mara ya kwanza kwa pamoja kwa mbwembwe na makachero wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(Takukuru) zilizochagizwa na vyombo vya habari wakikabiliwa na makosa hayo lakini hata hivyo siku hiyo walishindwa kutimiza masharti ya dhamana na hivyo kuamliwa kwenda gerezani hadi siku watakapotimiza masharti ya dhamana.

Kisha Desemba 15 mwaka 2008 majira ya mchana ndipo Mgonja alifikishwa peke yake hapo mahakamani na makachero wa Takukuru ambapo naye alisomewa mashtaka yale yale yanayofana na kesi ya Mramba na Yona na

Lakini ilipofika Januari 2 mwaka 2009 Jamhuri iliibadilisha hati ya mashtaka ya kesi iliyokuwa ikimkabibili Mramba na Yona kwa kumuunganisha Mgonja katika kesi hiyo hivyo kufanya kesi hiyo kuwa na jumla ya washtakiwa watatu na ile kesi iliyokuwa ikimkabili Mgonja peke yake kufutwa.

Na mwisho wangu kuudhulia kesi ya washtakiwa hao ambao ni watumishi wa muda mrefu serikali na Bungeni ni Oktoba 19 mwaka huu, ambapo kesi hiyo siku hiyo ilikuja mbele ya kwa Hakimu Mkazi Sundi Fimbo kwaajili ya kutajwa na jopo la mahakimu wakazi wanaosikiliza kesi hiyo yaani Jaji Utamwa, Rumanyika na Kinemela kuwagawia mwenendo wa kesi hiyo pande mbili za kesi hiyo yaani upande wa Jamhuri na ule wa utetezi ili kila upande uende kuaandaa sababu ambazo mwisho wa siku upande wa Jamhuri utaleta sababu zake za kuiomba Jamhuri iwaone washtakiwa hao wanakesi ya kujibu na upande wa utetezi utaiomba mahakama iwaone wateja wao hawana kesi ya kujibu na baada ya pande hizo kuwasilisha mahakamani maombi hao, ndipo kisheria mahakama inabaki na jukumu ya kuyapitia kwa kina maombi hayo ya pande hizo mbili na kisha mahakama hiyo inapanga tarehe yake ya kuja kutoa uamuzi utakaowaona washtakiwa hao ama wana kesi ya kujibu au wanakesi ya kujibu.

Na endapo mahakama itafikia uamuzi wa kuwaona washtakiwa wana kesi ya kujibu, hivyo washtakiwa watalazimika kupanda kizimbani kujitetea.

Lakini katika kesi hii ya Mramba, Yona na Mgonja, upande wa Jamhuri ilijitahidi kadri ya uwezo wake kuleta jumla ya mashahidi 13 ambao walifika mahakamani hapo na kutoa ushahidi wao na kisha ilipofika Januari 20 mwaka huu, ndipo upande wa Jamhuri uliambia mahakama hiyo kuwa wamefunga kesi yao.

Nakumbuka siku hiyo baada ya wakili wa serikali Boniface kuieleza mahakama kuwa wamefunga kesi yao, Jaji Utamwa jopo lake linaueleza uongozi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu chini ya Hakimu Mkuu Mfawidhi Elvin Mugeta uuchape mwenendo mzima wa kesi hiyo(Procedings) na ukimaliza kuuchapa mwenendo huo watapewa wanajopo hili waweze kuhuhakiki na wakishamaliza kuhakiki ndipo panede hizo mbili zitapewa mwenendo huo.

Tangu Jaji Utamwa atoe ahadi hiyo ambayo kweli ilitekelezwa kwa vitendo na uongozi wa Mahakama ya Kisutu licha mahakama ilikuwa ikikabiliwa na tatizo la mgao wa umeme ,ikauchapa mwenendo huo na ukaugawa mwenendo huo wa wanajopo hao na tangu kipindi hicho cha Januari 20 mwaka huu, washtakiwa na mawakili wa pande zote na waandishi wa habari za mahakamani wamekuwa wakifika mahakamani hapo kwa terehe zilizokuwa zikipangwa ambapo kesi hiyo imekuwa ikija kwaajili ya kutajwa huku mahakimu wanaoarisha kesi hizo ambazo siyo wanajopo wakihitimisha kuairisha kesi hiyo kwa kibwagizo kisemacho ‘jopo linalosikiliza kesi hiyo bado linaendelea na uhakiki wa mwenendo”.

Nakumbuka wakati mashahidi wa Jamhuri wanatoa ushahidi wao, kuna mwandishi mmoja aliripoti habari isiyosahihi kuhusu ushahidi huo hali iliyosababisha mawakili wa washtakiwa hao kugeuka mbogo na kuliomba jopo linalosikiliza kesi hiyo kulichukulia hatua gazeti hilo(siyo Tanzania Daima), lakini kiongozi wa jopo hilo Jaji Utamwa akitoleoa uamuzi ombi hilo alisema hawezi kutolea uamuzi ombi la mawakili hao kwasababu vyombo vya habari siyo sehemu ya kesi hiyo.Sehemu ya kesi hiyo ni upande wa Jamhuri na Utetezi.Nakubaliana na uamuzi huo.

Lakini sisi wanahabari tunawajibu wa ujulisha umma taarifa mbalimbali ikiwemo kesi mbalimbali zinavyoendelea mahakamani ikiwemo kesi hii ya Mramba.

Napenda ieleweke wazi kuwa kutokana na jopo hilo la mahakimu wakazi kuchukua muda mrefu bila kuzipatia pande mbili katika kes hizo ule mwenendo wa kesi hiyo, umezua minong’ono na hisia tofauti ambazo zinaendelea kusambaa chini chini kwa wananchi wenyewe, viongozi wa serikali, hata kwa mawakili wa pande hizo wamekuwa wakijiuliza nje ya mahakama kuwa kuna nini kilichojificha ambacho kinasababisha jopo hilo la mahakimu wakazi lichukue muda mrefu kuwapatia mwenendo huo?

Kwa wale tuliokuwa tukiudhulia kesi hii tunaweza kusema kesi hii ni miongoni mwa kesi chache za upande wa Jamhuri ambazo upande wa Jamhuri umejitahidi kuleta mashahidi wake kadri ya inavyoweza lakini cha kushangaza ni jopo hilo hadi kufikia leo inakaribia kumalizika mwaka mmoja inashindwa kutoa mwenendo huo wa kesi hiyo kwa pande hizo mbali hali inayosababisha kuibua maswali mengi kuliko majibu nje ya mahakama?

Ni rai yangu kwa jopo hilo linaloongozwa na Jaji Utamwa kwamba tayari kitendo cha jopo lake kuchukua muda mrefu licha jopo hilo lina haki ya kisheria kujitetea kuwa halikutoa muda kuwa kipindi fulani kitakuwa kimemaliza kuuhakiki mwenendo na kitakuwa kimeishazipatia pande pande hizo nyaraka, kimeanza kulalamikiwa chini chini na kuhusishwa na hisia mbaya na wafuatiliaji wa kesi hiyo na pia limesababisha sisi waandishi wa habari za mahakamani kuanza kujiuliza kuwa mahakama ina nini na kesi ya Mramba?.

Tunaamini jopo la mahakimu hao ni jopo la mahakimu wakazi wenye uweledi na uzoefu katika taaluma hiyo ya sheria.Na ninafahamu pia mahakama haifanyi kazi kwa hisia wala minongono ya watu waliopo nje ya mahakama lakini, ni vyema pia jopo hilo kuanzia sasa likaona ni vyema kukomesha hisia hizo mbaya ambazo hazina ushahidi zinazoelekezwa kwao na hivyo likaharakisha kuzipatia pande hizo mbili mwenendo huo ili taratibu zingine za kisheria kuhusu kesi hizo ziendelee.

Ieleweke wazi kesi hiyo inawahusu washtakiwa hao ambao walishatoa mchango mkubwa wa utumushi katika taifa letu hivyo wanamajukumu mengine yakufanya, pia nao mawakili wa serikali na mawakili wa kujitegemea nao wanamajukumu mengine, sasa kitendo cha kesi hiyo ambayo hivi sasa inakaribia kufikia mwaka mmoja , inakuja kwaajili ya kutajwa tu , ni wazi kabisa hao mawakili, washtakiwa na ndugu wawashtakiwa na sisi waandishi wa habari tunashindwa kwenda kufanya shughuli nyingine za ujenzi wa taifa tunakuja kuudhulia kesi hiyo ambayo inaairishwa kila kukicha na mbaya zaidi inaarishwa kwa mahakimu ambao hawasikilizi kesi hiyo, huku jopo hilo la mahakimu wakazi halifiki katika viwanja vya mahakama ya Kisutu kuarisha kesi hiyo.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Oktoba 27 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.