Header Ads

DK..BILAL ATUA BRAZIL KUSHIRKI RIO +20 JUMATANO

Na Happiness Katabazi,Brazil TANZANIA na mataifa mengine mbalimbali dunia Jumatano hii inaanza kuudhulia mkutano wa Rio+20 unaofanyika jijini Rio Je Neiro nchini Brazil. Mkutano huo ambao utamalizika Juni 22 mwaka huu na washiriki wa mkutano huo kutoa maazimio yao ya nini kifanyike kuhusu kuhusu uharibu wa misitu na mazingira kwa ujumla, unaudhuliwa na marais wa nchi,wawakilishi wa marais hao, wataalamu wa masuala ya mazingira duniani. Kwa upande wa Tanzania, makamu wa Rais Dk.Mohamed Gharib Bilal ambaye amefuatana na Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia mazingira, Teresa Uvisa, Mshauri Mwandamizi wa rais Jakaya Kikwete wa masuala ya Kidiplomasi, balozi Liberata Mulamula na maofisa wengine waandamizi wa serikali ndiye aitaiwakilisha nchi na tayari jana mchana aliwasili nchini hapa tayari kwaajili ya kuudhuria mkutano huo. Mwandishi wa habari hizi ambaye ni miongoni mwa waandishi wa habari anayeudhulia mkutano huo wa kihistoria ameshuhudia maofisa ubalozi wa Tanzania nchini hapa wakimlaki Dk.Bilal na pia kuwashuhudia baadhi ya wakuu wa mataifa mbalimbali duniani waliofuatana na watendaji wa serikali zao wakiwasili mjini hapa Rio de Jeneiro kwaajili ya kuudhulia mkutano huo. Pia mwandishi wa habari ambae ameweza kutembelea katikati ya mji wa Rio De Jeneiro ameishuhudia wananchi wa mataifa mbalimbali wakiwa wamekodi katika mahoteli hao kwaajili ya kuishi kwa muda wakati wakiidhulia mkutano. Katika mkutano huo wa mazingira duniani maarufu kama Rio +20 ,wanakusudia kujadili matatizo ya uharibu wa mazingira yaliyojitokeza kwa ghafla katika karne ya 21 kwani uharibu wa misitu utabakia kuwa ajenda ya juu ya mkutano huo wa mwaka huu 2012.

No comments:

Powered by Blogger.