Header Ads

NG'UMBI AKIMBILIA MAHAKAMA YA RUFAA

Na Happiness Katabazi ALIYEKUWA mgombea Ubunge jimbo la Ubungo kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi(CCM), Hawa Ng’umbi amewasilisha hati ya kusudio la nia ya kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa nchini, akipinga hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ambayo ilitupilia mbali kesi yake ya uchaguzi ambayo ilikuwa ikipinga ubunge wa mbunge wa jimbo hilo John Mnyika(Chadema). Nia hiyo iliwasilishwa Mahakama ya Rufaa na wakili wa Ng’umbi , Issa Maige kwa njia ya maandishi ikiwa ni siku chache baada ya Jaji wa Mahakama Kuu Upendo Msuya kutupilia mbali kesi ya uchaguzi Na.107 ya mwaka 2010 iliyofunguliwa na Ng’umbi dhidi ya Mnyika. Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima jana, Ng’umbi alithibitisha kuwasilisha kusudio hilo la kukata rufaa na kwamba tayari nakala ya kusudio hilo imeishapelekewa Mnyika. Mei 24 mwaka huu, jaji Msuya alitoa hukumu ya kesi ya kupinga ushindi wa Mnyika iliyofunguliwa na Ng’umbi ambapo jaji huyo aliitupilia mbali kesi hiyo kwa maelezo kuwa madai ya Ng’umbi dhidi ya Mnyika ambayo yalikuwa ni kuiomba mahakama itamke kuwa uchaguzi wa Jimbo la Ubungo ulikuwa ni batiri kwasababu haukuwa huru na haki, taratibu za uchaguzi zilikiukwa kwani kuna baadhi ya fomu hazikujumlisha matokeo, pia Mnyika aliingiza Laptop kwenye chumba cha kuhesabia kura na kwamba alizitumia laptop hizo kujiongezea kula, Mnyika aliingiza watu watano katika chumba cha kujumlishia kura wakati watu hao hawakuwa na kibali cha kuingia ndani ya chumba hicho,pia Mnyika alimtolea maneno ya alimkashifu kwa kumita fisadi kwani alipokuwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake(CWT) Kinondoni, aliuza kifisadi nyumba za jumuiya hiyo na kwamba kuna baadhi ya kula zimeongezeka, halishindwa kuleta ushahidi wa kuthibitisha. Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Juni 14 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.