Header Ads

MAHALU HANA HATIA-MAWAKILI

Na Happiness Katabazi ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania nchini Italia Profesa Costa Mahalu na Meneja Utawala na Fedha, Grace Martin wameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, isiwaone wanahatia katika kesi ya wizi wa Euro Milioni tatu kwasababu upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi wa kutenda makosa hayo. Balozi Mahalu aliwasilisha maombi hayo ya jana mchana kupitia mawakili wake Mabere Marando, Beatus Malima ,Alex Mgongolwa na Cuthbert Tenga kwa njia ya maandishi mahakamani hapo kama walivyoamriwa kufanya hiyo na Hakimu Mfawidhi Ilvin Mugeta Mei 16 mwaka huu, ambapo hakimu huyo alizitaka pande zote kuwasilisha jana majumuisho hayo ya kuiomba mahakama iwaone washtakiwa wana hatia au la. Kwa mujibu wa maombi hayo ya Mahalu ambapo Tanzania Daima ina nakala yake, mawakili wamewaanza kuikumbusha mahakama kuwa washtakiwa hao wanakabuliwa na makosa sita likiwemo kosa lakula njama, wizi wa Euro milioni mbili ,kugushi vocha za manunuzi ya jengo la Ubalozi,kutumia risiti za manunuzi kuidanganya serikali,kuisababishia serikali hasara ya Euro milioni tatu. Kwa mujibu wa hoja zao tano muhimu ambazo wamezitumia kuwasilisha ombi hilo, hoja ya kwanza mawakili hao wa utetezi Serikali ya Tanzania ilimruhusu Mahalu kununua jengo la ubalozi kwa njia ya mikataba miwili kwa bei ya Euro 3,098,741.58 na kwamba Mahalu alileta vielelezo kadhaa ambavyo viliweza kuithibitishia mahakama hiyo kuwa serikali ililidhia jengo hilo linunuliwe kwa njia ya mikataba miwili na kwa thamani hiyo…na kwamba hakuna ushahidi wowote ulioletwa na upande wa Jamhuri kuwa washtakiwa walifanya siri na kutenda kosa la wizi”alidai wakili Marando. Hoja ya pili, mawakili hao wanadai kuwa upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi unaonyesha muuzaji wa jengo hilo la ubalozi hakupokea fedha za manunuzi ya jengo hilo ambazo ni Euro milioni tatu..na kwamba wameshindwa kuleta ushahidi ambao ungethibitisha muuzaji huyo wa jengo hakulipwa kiasi hicho cha fedha na washtakiwa. Aidha hoja ya tatu ni kwamba ripoti tatu za thamani ya majengo zilizoandaliwa na Wizara ya Ujenzi, muuzaji na ubalozi wa Tanzania nchini Rome hazikuandika jengo hilo lilikuwa na thamani ya chini ya Euri milioni tatu, kwani ripoti zote ziliandika jengo hilo lilikuwa na thamani ya zaidi ya Euro milioni tatu na kwamba upande wa jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi unaonyesha unaonyesha wakati huo jengo linanunuliwa lilikuwa na thamani ya kiasi gani na kwa maana hiyo jamhuri ilikuwa haifahamu thamani ya jengo hilo wakati serikali inalinunua. “Hoja ya tano sisi tunadai kuwa upande wa Jamhuri umeshindwa kuleta ushahidi ambao ungeonyesha nani ni mmiliki wa akaunti mbili ambazo Euro milioni tatu ambazo zilitumwa na ubalozi wa tanzania nchini Rome kwenye akaunti hizo: “Kwa hoja hizo tano tulizozitaja hapo juu, tunaiomba mahakama hii iwaone washtakiwa hawana hatia kwasababu upande wa jamhuri wameshindwa kuleta ushahidi ambao utaishawishi mahakama iwaone washtakiwa hao wana hatia katika makosa wanashitakiwa nayo” alidai wakili Marando. Hata hivyo mahakama hiyo Julai 11 mwaka huu, ndiyo itakuja kutoa hukumu katika kesi hii ambayo ilifunguliwa rasmi mwaka 2007. Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Julai 12 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.