Header Ads

MKUTANO WA MAZINGIRA UTUBADILISHE TABIA

Na Happiness Katabazi MAKAMU wa Rais wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal ataliwakilisha taifa katika mkutano wa dunia wa mazingira utakaofanyika Rio De Jeneiro nchini Brazil kuanzia Juni 20-22 mwaka huu. Wataalamu wa masuala ya Geographia wanaeleza mkutano huo maarufu kama mkutano huo , utatoa fiursa kwa viongozi wa mataifa mbali mbali kujadili na kufikia muafaka kuhusu masuala ya mazingira na kutoa dira ya nini kifanyike baada ya mkutano huo kumalizika kufanyika. Itakumbukwa kuwa Juni 5 kila mwaka Watanzania huungana na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, na kwa mwaka huu tayari Tanzania ilishazindua maazimisho hayo katika mikoa mbalimbali. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Terezya Huvisa,hivi karibuni alinukuliwa akisema maadhimisho hayo ni kumbukumbu ya mkutano wa kwanza wa Umoja wa Mataifa kuhusu mazingira uliofanyika mwaka 1972 mjini Stockholm, Sweden. Dk.Huvisa alisema kaulimbiu ya maadhimisho hayo kwa mwaka huu ni ‘Uchumi Kijani; Unakuhusu’. Anasema ujumbe huu unahimiza kuwajibika katika uzalishaji endelevu kwa kupunguza uzalishaji wa gesijoto hususani gesi ,mkaa na matumizi bora ya rasilimali. Anasema kitaifa ujumbe unaoongoza maadhimisho hayo ni hifadhi ‘Hifadhi Mazingira; jikite kwenye uzalishaji endelevu’. Kwa mujibu wa waziri huyo wa mazingira, changamoto za mazingira zinazoikabili nchi ni nyingi, mojawapo ni zaidi ya asilimia 60 ya nchi inakabiliwa na hali ya jangwa na ukame. Anasema changamoto nyingine ni kwamba takriban hekta 220,000 za misitu huangamia kila mwaka kwa mahitaji ya nishati, kilimo kisicho endelevu na kwa mahitaji ya ujenzi, uwezo wa malisho katika mikoa mingi umezidiwa na wingi wa mifugo hivyo kusababisha uharibifu mkubwa wa mazingira pamoja na uvamizi katika vyanzo vya maji. Kwa maelezo hayo hapo juu, kwanza nampongeza Dk.Huvisa uthubutu wake wa kuanika ukweli wa vyanzo vya uharibu wa mazingira unavyoathiri maeneo fulani katika taifa letu na kushauri nini kifanyike. Hakuna ubishi kuwa kadri siku zinavyozidi kwenda uhalifu wa mazingira umekuwa ukishika kasi hapa nchini kana kwamba waliopewa dhamana ya kuakikisha wanawathibiti wahalifu hao wameacha kazi, au wale wanaojihusisha na vitendo vya uharibu huo wa mazingira wanafikiri madhara ya uharibu wa mazingira hautakuja kuwaathiri kwa nanma yoyote ile. Ukitembelea baadhi ya maeneo ya mikoa ya nchi hii hivi sasa na ukilinganisha na miaka iliyopita utabaini kuwa tayari kuna wananchi au viwanda vimejihusisha na utendaji kazi katika maeneo hayo ambayo matokeo yake yanasababisha ukame, mikiti kukaukwa na kukatwa kwasababu ya shughuli hizo za binadamu ambazo zimesababisha uharibifu wa mazingira. Ukitembelea mito inayotililisha maji hapa jijini na mfano mzuri ni Mto Ng’ombe ,Bonde la Mto Msimbazi na mingine utaona kuna baadhi ya watu wamejenga makazi yao kando kando ya mito hiyo na wengine wamekuwa wakitupa takataka katika maeneo hayo na wengine wametililisha mabomba ya maji machafu yanayotoka kwenye vyoo vyao kuingia kwenye mito hiyo ili kuweza kuhebuka gharama za kulipia magari ya kuja kuchonya maji taka katika majumba yao. Hali hiyo imekuwa ikisabisha nyakati za mvua , mito hiyo kufurika sana na maji yanayopita kwenye mito hiyo ulazimika kupita kwa shida hali inayosababisha maji hayo kupita kwenye mkondo wake maji ambapo mkondo huo mara nyingine ndiyo nyumba za watu waliojenga mabondeni na mwisho wa siku Desemba 21 na 22 mwaka huu, nyumba za watu na wananchi kadhaa kupoteza maisha kwa kutoka na mvua kubwa iliyonyesha. Hivyo mkutano huo wa mazingira , Tanzania inayoenda kuwakilishwa na Dk.Bilal tuutumie vizuri kwa kuwasilisha hoja mathubutu na kuibua mjadala wenye mashiko sambamba na kila mwananchi kuanza kuchukia kutenda matendo yanayoleta uharibu wa mazingira. Hivi sasa kunazana ya kijinga iliyotawala katika vichwa vya baadhi ya watu hapa nchini kwamba kutunza mazingira ni kwa wale waliojariwa kuwa na vipato vikubwa kutengeneza bustani za mauwa ya kila aina majumbani kwao. Kwani Taifa hili na dunia hii ni yetu sote hivyo yanapotokea madhara ya uhalifu wa mazingira,anga tunaoathirika ni sisi binadamu tunaondelea kuishia humu duniani na vizazi vyetu. Na mataifa maskini pia yatumie mkutano wa Rio De Jeneiro kuakiskisha yanasimama kidete kuyakemea mataifa tajiri ambayo yamekuwa yakituhumiwa kuwa ni chanzo cha kusabisha uhalifu wa mazingira katika anga kwani kila kukicha yamekuwa yakitengeneza vifaa na kemikali ambazo wataalumu wa masuala ya mazingira wamedai yanasababisha mabadiliko ya tabia ya nchi. Nimalizie kwa kuwauliza wasomi wa masuala ya Geografia na wadau wa mazingira na taifa kwa ujumla wamejipangaje na mkutano wa mazingira duniani wa Rio De Jeneiro-Brazil ? Naomba kutoa hoja. Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania 0716 774494 www.katabazihappy.blogspot.com Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Juni 10 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.