Header Ads

WAZIRI MKANGARA UMESEMA KWELI

Na Happiness Katabazi MAPEMA wiki hii Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na MIchezo Dk.Fenella Mkangara aliwataka maafisa Habari wa serikali kuachana na tabia ya kuficha habari za serikali kwasababu kufanya hivyo ni kuwanyima wananchi haki ya Kikatiba ya kupata habari. Dk.Mkangara aliyasema hayo katika ufunguzi wa mkutano wa maafisa habari wa serikali ambapo alisema kitendo pia kinasababisha serikali ionekane haifanyi kazi kwasababu wao wanashindwa kuwapatia taarifa za shughuli za kimaendeleo zilizofanywa na serikali kwa wananchi. Binafsi nilimshuhudia Dk.Mkangara akitoa maneno hayo kupitia Televisheni na lilinufurahisha mno kwasababu ameongea ukweli mtu bila kuwaonea haya maofisa habari ambao wengi wao kadri siku zinavyozidi kwenda tunawaona wameishasahau majukumu yao kitaalum. Awali ya yote naomba ieleweke kuwa siyo kila taarifa za serikali zinapaswa kutolewa kwa umma.Kuna baadhi ya mambo yanayofanywa na serikali kwa maslahi ya taifa yetu hayapaswi kuwekwa adharani kwasababu ya unyeti wake na ndiyo lakini kuna baadhi ya mambo yanatakiwa umma uelewezwe. Lakini hayo mambo ambayo umma unatakiwa uelezwe na serikali kupitia maofisa habari hao, wamekuwa hawayaelezi kila wakati kama wanavyotakiwa wafanye hivyo. Ni maofisa Habari wachache sana wa serikali wamekuwa wakijiamini na kutekeleza moja ya jukumu hilo la kuubadilisha umma bila ugumu wowote.Lakini maofisa habari wengi wa serikali hapa nchini wamekuwa ni wazito kutoa taarifa mbalimbali kwa umma kwa kisingio kuwa mawaziri ,wakuu wa wilaya,makatibu wakuu, wakuu wa mikoa wamekuwa wakiwazuia kichinichini kutoa taarifa kwa umma na matokeo yake maofisa habari hao wameamu kukaa kimya. Minajiuliza hivi ofisa habari ambaye alisoma vizuri chuoni ni lazima atakuwa anaifahamu vyema kazi yake na kamwe hatakubali kuyumbishwa na mtu ambaye hana taaluma ya habari. Lakini cha kushangaza baadhi ya maofisa wa habari wa serikali hawako hivyo kabisa na uenda labda ni kwasababu waliajiriwa moja kwa katika nafasi hizo bila kwanza kufanyakazi katika vyumba vya habari? Lakini mwandishi wa habari ufanyakazi kwenye vyombo vya habari kwanza inaweza isiwe sababu ya msingi ya kusababisha afisa wa habari wa serikali kushindwa kutoa taarifa kwa umma, kwani kuna baadhi ya maofisa habari wa serikali leo hii hapo nyuma walishawahi kuwa waandishi wa habari katika vyumba kadhaa vya habari lakini waliteuliwa au walivyoajiriwa kuwa maofisa wa habari wa serikali ndiyo wamekuwa mstari wa mbele leo hii kushindwa kutoa taarifa za serikali kwa umma, kubagua vyombo vya habari katika kuvipa taarifa, wameshindwa kuwabunifu katika ofisi zao za habari huko serikalini. Ieleweke kuwa hivi sasa hapa ulimwengu umuhimu wa watu kupashana habari za aina yoyote unazidi kuongezeka na hali hiyo isaidia wananchi kujua nini kinaendelea hapa nchini na duniani kwa ujumla. Ndiyo maana makala yangu ya leo nimelazimika kuunga mkono hoja ya Waziri Mkangara ya kuwasema wazi wazi maofisa hao waache tabia ya kuficha habari bila sababu za msingi. Bila serikali kutoa taariza zake kwa umma ni wazi wananchi walioiweka serikali hiyo madarakani wataishia kulalamika kila siku kuwa serikali yao haiwatimizii matakwa yao na ushahidi wa hilo ni hivi sasa wananchi wengi wamekuwa wakiishutumu serikali kuwa haijawafanyia lolote jambo ambalo si kweli kwani kuna baadhi ya mambo ya kimaendeleo ikiwemo ujenzi wa barabara, nafuu ya upatikanaji wa umeme ukilinganisha na miaka mitatu nyuma hapo taifa lilikuwa likikabiliwa na mgao wa umeme, sera ya watoto wa chini ya miaka mitano kutibiwa bure katika hospitali za serikali na mambo mengine mengi lakini mambo hayo ya kimaendeleo hayasemwi kwa mapana na maofisa habari hao. Ukiachilia mbali hilo pia kuna baadhi ya maofisa habari wa serikali wamekuwa na kasumba mbaya ya kubagua vyombo vya habari vya kuvipatia taarifa bila sababu za msingi jambo ambalo linatufanya sisi waandishi wa jeuri tukiwa na shida ya kupata taarifa za taasisi fulani kuamua kwenda moja kwa moja ama kwa waziri,wakurugenzi, mkuu wa wilaya au wakuu wa mikoa watupatie hizo hizo kwa maslahi ya nchi. Na maofisa wa habari wenye tabia hii waache hiyo tabia kwani wakae wakijua cheo ni dhamana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, inakataza ubaguzi wa aina yoyote ile. Ina kera sana tabia hiyo kwani wakati mwingine mwandishi wa habari anataka kuandika habari au makala kuhusu eneo fulani anaitaji kupatia taarifa za kiserikali kutoka kwa maofisa habari lakini cha kusikitisha hapewi ushirikiano na baadhi ya maofisa hao wa serikali hali inayosababisha baadhi ya waandishi wa habari wanaofanya kazi katika vyombo vya habari kuandika taarifa au makala isiyokuwa na taarifa rasmi za kiserikali au mwandishi mwingine anaamua kuachakuandika makala au habari ya eneo lile alilokuwa amekusudia kuliandikia ili aweze kuubadilisha umma. Nimalizie kwa kuwataka hao maofisa habari wanaokalia habari waache tabia hiyo, wabadilike na waige mfano maofisa habari wenzao ambao ni Shy Rose Banji wa Benki ya Makabwera(NMB), na Badra Masoud wa Tanesco na wengine wachache ambao kwakweli hawa ni maofisa habari hao ni wachapakazi, wanajiamini kitaaluma na katika ofisi zozote wanapoenda kufanyakazi mchango wao unaonekana hata kwa watu wasio na taaluma ya habari. Mfano hai ni kipindi kile Banji na Badra katika nyakati tofauti walivyowai kushika wadhifa wa Afisa Uhusiano wa DAWASCO , sote tuliwashuhudia maofisa hao walivyokuwa wakichapakazi yao na kutoa taarifa za kwa umma bila upendeleo na hadi sasa wamekuwa wakifanya hivyo.Igeni mfano wao. Nimalizie kwa kuwaasa wale maofisa habari wanaokalia habari na wasiotaka kutoa ushirikiano ,wazingatie funzo walilopewa na Dk.Mkangara kwani kama wasipotaka kubadilika ipo siku viongozi wao ambao wanataka umma upewe taarifa watawachoka na watawaondoa kwenye hizo nafasi na kuwaweka maofisa habari wasiowababaishaji ili waweze kushika nyadhifa hizo. Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika 0716 774494 www.katabazihappy.blogspot.com Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamisi, Juni 14 mwaka 2012.

No comments:

Powered by Blogger.