Header Ads

HUKUMU YA RUFAA YA WAFUASI WA PONDA YAWEKWA KIPORO

 
Na Happiness Katabazi
 
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana ilishindwa kutoa hukumu ya rufaa iliyokatwa na wafuasi  52 wa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu ,Sheikh Issa Ponda Issa, ambapo Machi 21  mwaka huu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, iliwahukumu adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja jela, wameiomba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kwa maelezo kuwa bado haijaiandaa hukumu hiyo.
 
Jaji Salvatory Bongole alisema ni kweli rufaa hiyo ilikuja jana kwaajili ya yeye kuitolea hukumu lakini ameshindwa kutoa hukumu hiyo kwasababu tangu Septemba 2 hadi Oktoba 4 mwaka huu, anasikiliza vikao vya kesi ya mauji hivyo ameshindwa kuandaa hukumu hiyo na badala yake anaiarisha kesi hiyo hadi Oktoba 21 mwaka huu ambapo siku hiyo atakuja kuitolea hukumu na akaamuru waomba rufaa warejeshwe gerezani.
 
Agosti 12 mwaka huu, rufaa hiyo ilianza kusikilizwa rasmi na jaji huyo ambapo wakili wa waomba rufaa   Mohammed Tibanyendera  aliomba ,mahakama hiyo iwachilie huru Salum Bakari Makame na wenzake 51 na itengue hukumu iliyotolewa na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Sundi Fimbo baada ya kuwakuta na hatia ya makosa ya matatu ya kula njama,kufanya mkusanyiko haramu  na kukaidi amri ya jeshi la polisi  iliyowataka wasiaandamane kwenda ofisini kwa Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi kushinikiza ampatie dhamana Ponda ambaye alikuwa akikabiliwa na kesi ya wizi wa malighafi zenye thamani ya Sh.milioni 59 ambaye alihukumu kifungo cha mwaka mmoja jela.
 
Tibanyendela alidai kuhusu kosa la kwanza la kula njama kwa mujibu wa rekodi ya hukumu, ile hakuna ushahidi unaonyesha washitakiwa walikutana mahali kokote kupanga njama ya kutenda kosa hilo lakini wanashangazwa na Hakimu Fimbo kuwatia hatiani kwa kosa hilo kwa shahidi kwanza hadi wa 10 ambao ni maofisa wa polisi walieleza mahakama kuwa waliwakamata washitakiwa hao katika maeneo tofauti jijini Dar es Salaam Februali 15 mwaka huu.
 
Wakili Tibanyendera alikilichambua kosa la kula njama kutenda kosa kinyume na kifungu 384 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, kosa la pili ni la kufanya mkusanyiko haramu kinyume na kifungu cha 74 na 75 cha sheria hiyo  ambavyo vinasomwa pamoja na kifungu cha 43(2)(4) na 46 cha Sheria ya Jeshi la Polisi ya mwaka 2002.
 
‘Kwa masikitiko makubwa tu   nasema kosa la kula njama halikuthibitika, na hakimu Fimbo alikosea kuwatia hatiani kwa kosa la kula njama kwa kutumia kifungu hicho cha 384 cha sheria ya Kanuni ya adhabu. Na kwa mujibu wa kifungu cha 46 cha Sheria ya Jeshi la Polisi ya mwaka 2002,inasema wazi kabisa mtu anayekutwa a hatia ya kutenda kosa la mkusanyiko haramu atapaswa alipe faini ya Sh.50,000 au kwenda jela miezi mitatu au vyote pamoja:
 
‘Lakini tunashangaa huyu hakimu Fimbo ameto adhabu ya juu kabisa ya mwaka mmoja jela..sijui hiyo sheria ameipata wapi?Tunaomba mahakama hii itengue hukumu hiyo kwani inadosari nyingi za kisheria na hakukuwa na ushahidi wowote wakuweza kuishawishi mahakama hiyo iwatie hatiani waomba rufaa”alidai wakili Tibanyendera.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Septemba 21 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.