Header Ads

RUFAA YA DPP,MAHALU HAKIELEWEKI



Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana ilijikuta ikishindwa kaanza kusikilia rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia na Grace Martin  kwa sababu mwenendo wa kesi hiyo iliyokuwa ikiendeshwa awali katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu haujawekwa kwenye jarada la rufaa ambalo linaanza kutumiwa na Mahakama Kuu kuendeshea rufaa hiyo.

Jaji John Utamwa alisema kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kaunza kusikilizwa lakini kwa bahati mbaya jarada la rufaa hiyo ndani yake haina rekodi ya kesi ya uhujumu uchumi iliyokuwa ikiwawakabili wajibu rufaa yaani (Mahalu na Grace), ambao
Agosti 9 mwaka jana  walishinda kesi hiyo ya uhujumu uchumi na wizi wa Euro zaidi ya milioni mbili.

Alisema sababu ya pili mawakili wa wajibu rufaa, Mabere Marando na Alex Mgongolwa wanaudhuru hivyo anaiarisha rufaa hiyo hadi Novemba 11 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya kusikilizwa.
Agosti 9 mwaka huu, Hakimu mkuu Mfawidhi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu , Ilvin Mugeta aliwaachilia huru Mahalu na Grace Martin kwa maelezo kuwa upande wa jamhuri umeshindwakuthibitisha kesi yao.Na muda mfupi baada ya hukumu hiyo kutolewa DPP hakulidhishwa na hukumu hiyo akakata rufaa Mahakama Kuu kupinga hukumu hiyo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Septemba 3 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.