Header Ads

UB ILIVYOJITOA KUWAFUNDA WATETEZI HAKI ZA BINADAMU






Na Happiness Katabazi

NENO ‘watetezi wa haki za binadamu’ bila shaka siyo neno geni kwa masikioni mwa watu. Neno hilo limekuwepo kwasababu linatumiwa na watu wanaojitambulisha kuwa wao ni watetezi wa haki za binadamu ndani na nje ya Tanzania.

Kwa upande fulani watetezi hao wa haki za binadamu wamekuwa wakifanyakazi nzuri ya kuwaelekeza wananchi wasiyojua haki zao jinsi ya kuzidai kwa kufuata utaratibu na mwisho wa siku wanancho hao wanaozingatia ushauri wa watetezi hao wa haki za binadamu wamekuwa wakifanikiwa.

Lakini kwa upande mwingine kuna makundi ya watu wanaojitambulisha kuwa ni watetezi wa haki za binadamu kwanza hawana hata elimu ya kujua haki za binadamu ni zipi, zinadaiwa kwa njia zipi na wengine wamekuwa wakijifanya watetezi wa haki za binadamu kumbe wanatumia ngao hiyo kujificha kumbe ni wanachama wa vyama vya siasa na wakati wakiamasisha watu kudai haki zao wamekuwa wakipenyeza ajenda zao za kiitikadi jambo ambalo siyo sahii.

Hili kuondokana na wimbi la wanaharakati ucharwa ambao kadri siku zinavyozidi kusonga mbele hapa nchini linazidi kushamili,na ambapo kama wimbi hilo halitadhibitiwa Tanzania inaweza kujikuta inaingia kwenye machafuko kwa kisingizio cha baadhi ya wanaharakati wasiyo na elimu za ki uhanarakati kila kukicha kutoa matamko katika jamii ambayo wakati mwingine matamko hayo yanapotosha jamii na kuleta mivutano baina ya wananchi na serikali,  Chuo Kikuu cha Bagamoyo Dar es Salaam (UB), kinachoongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo Profesa Costa Ricky Mahalu kwa kushirikiana na Taasisi isiyoyakiserikali ya nchini Kenya , Akiba Uhaki imezindua mafunzo ya kuwanoa wale wote wanaojiita wanaharakati na wale wanye ndoto ya kuwa wanaharakati yatakayo chukua miezi sita chuoni hapo kwaajili ya kuwafundisha watetezi hao wa haki za binadamu kwanza kuzifahamu haki hizo za binadamu ni zipi, zinadaiwaje, na kisha waende kwenye jamii kuielimisha jamii jinsi ya kuzidai haki hizo kwa njia ya amani na utulivu na siyo maandamano yasiyo na vibali wala ghasia.

Tumeshuhudia baadhi ya watu wanaojiita wanaharakati wakiwachochea wananchi kudai haki kile wanachoona ni haki yao kwa kuamua kupambana na vyombo vya dola na mwisho wa siku wananchi hao wanajikuta wakiambulia kupata madhara ya kupata vigipo au kufikishwa mahakamani kwa makosa mbalimbali yakiwemo ya maandamano haramu,kuzuia polisi wasifanyekazi yao na kufanya mikusanyiko haramu.Na wananchi hao wakipata madhara hayo,wale watu watu wanaojiita ni wanaharakati ambao walikuwa wakiwatuma kufanya hivyo, wao ukaa pembeni.
  
Mbali na maelezo , mwandishi wa makala hii anasimulia hotuba zilizotolewa katika uzinduzi wa program ya Akiba Uhaki inayotolewa na Chuo Kikuu cha Bagamoyo kwaajili ya kuwaonea watetezi wa haki za binadamu siku ya uzinduzi wa program hiyo uliofanyika Jumatatu usiku katika chuo hicho kilichopo Kawe Beach Dar es Salaam , ambapo Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mercy Sila alitoa hotuba yake kwaniaba ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza.

Sila alisema serikali inakipongeza  Chuo Kikuu cha Bagamoyo(UB), kwa uamuzi  wake wa kuanzisha kozi ya kuwanoa watu wanaojitambulisha kuwa wao ni watetezi wa haki za binadamu katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kwasababu kozi hiyo itasaidia  watetezi wa haki za binadamu kufahamu wanachokifanya katika jamii na kwamba kozi hiyo inakuwa ni ya kwanza kutolewa hapa nchini.


Sila alisema program hiyo inaendeshwa na Chuo Kikuu cha Bagamoyo (UB) na kufadhiliwa taasisi ya kiraia ya  Haki Uhaki yenye makao makuu yake nchini Kenya, tayari imeishapata wanafunzi kumi  toka nchi za Tanzania,Kenya,Uganda,Rwanda,Burundi  na kwamba masomo hayo yatakuwa yakitolewa kwa miezi sita na kuwataka wale wote wanaojiita wanaharakati hapa nchini wafike katika chuo hicho ili waweze kufundishwa kwanza jinsi ya kufahamu haki za binadamu ni zipi ,na haki za kijamii ni zipi na hao wanadamu wanatakiwa wazitii sheria za nchi wakati wakizidai hizo haki zao bila shuruti.

“Tumeona katika mataifa ya wenzetu vurugu kila kukicha na hata hapa nchini kuna baadhi ya watu wanaojiita ni watetezi wa haki za binadamu na wamekuwa wakitumia kinga hiyo kupotosha ukweli wa mambo ambayo yanafanywa na serikali zao kwa kisingizio kuwa wa ni watetezi wa haki za binadamu wakati hata elimu ya kutetea hizo haki za binadamu hawana …leo serikali inapenda kupongeza program hii kwani itasaidia sana kuondoa mivutano na malumbano baina ya watetezi wa haki za binadamu na serikali kwani  mtu atakayepata elimu hii atakuwa ameelimika na kufahamu haki za binadamu zinapaswa zidaiwe kwa kutumia amani”alisema Sila.

Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo, Profesa Costa Ricky Mahalu aliishukuru serikali kwa kukubali kuja kuzindua program hiyo kwani programu ni yakwanza kutolewa katika vyuo vya hapa nchini na program hiyo itawezesha kuondoa malumbano baina ya serikali na watetezi wa haki za binadamu kwani ni wazi hivi sasa kumeibuka watu wanaojitambulisha kuwa ni watetezi wa haki za binadamu wakati hawana hata elimu ya huo utetezi wa haki za binadamu na wamekuwa wakitoa baadhi ya matamko ambayo  hayana mantiki katika suala zima la utetezi wa haki za binadamu hali ambayo alisema ikiachwa iendelee italeta madhara katika jamii.

“UB inaamini katika elimu zaidi…hivyo UB imeona ni jambo jema kuanzisha program hiyo ya mafunzo ya muda mfupi kwa wale wote wanaotaka na wanajiita watetezi wa haki za binadamu waje kufundishwa masuala hayo na waadhiri waliobobea katika eneo hilo la masuala ya haki za binadamu”alisema Profesa Mahalu.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Bagamoyo  Dk.Natujwa Mvungi ambayo program hiyo ya Akiba uhaki inatolewa chini ya kitivo chake alisema   jumla ya wanafunzi 10 toka katika nchi tano za jumuiya ya Afrika Mashariki  wa kozi ya Akiba Uhaki ,wameishafika hapa nchini na wanaanza mafunzo hayo kwa muda wa miezi sita kuanzia wiki hii chuo hapo na kwamba wanafunzi hao wamefadhiliwa ada ya kusoma kozi hiyo na taasisi isiyo ya kiserikali yenye makao makuu yake nchini Kenya ya Akiba uhaki na kuwataka wale wote wanaojiita ni watetezi wa haki za binadamu  wakati hawana elimu ya kuonyesha wamefudhu kozi hiyo,wasisite kuja kupata elimu hiyo chuo hapo.

Aidha Mratibu wa Programu hiyo toka Taasisi ya Akiba Uhaki ya nchini Kenya, Kempta Ombati alishukuru chuo cha UB, kukubali kushirikiano nao kutoa mafunzo hayo ambayo yasaidia nchi za Afrika Mashariki kuondokana na watu wanaojiita kuwa ni wanaharakati wakati hawana elimu ya kuzijua haki wanazozitetea na wajibu na kwamba taasisi yake ndiyo imetoa ufadhili kwa wanafunzi hao kumi wanaotoka nchi zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki kuja kuudhulia kozi hiyo  katika chuo Kikuu cha Bagamoyo na kwamba mafunzo hayo ni ya kwanza kutolewa katika vyuo vya hapa nchini na kwamba taasisi yao itaendelea kutoa ufadhili.

 0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumapili , Septemba 22 mwaka 2013.


No comments:

Powered by Blogger.