Header Ads

HATI YA KESI YA NG'UMBI INA MAKOSA

Na Happiness Katabazi
ALIYEKUWA mgombea ubunge wa Jimbo la Ubunge(CCM), Hawa Ng’umbi ambaye ni ndiye mlalamikaji katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 yaliyomtangaza John Mnyika kuwa mbunge wa jimbo hilo, amekiri kuwa hati yake ya madai aliyoifanyia marekebisho ina makosa ya kisheria na anaiomba mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imruhusu aende kuifanyia marekebisho.


Ng’umbi aliyasema hayo kupitia majimbu yake yaliyowasilishwa kwaniaba yake na wakili wake Issa Maige kwa Jaji Upendo Msuya ambapo alidai anakubaliana na baadhi ya mapingamizi aliyowekewa na Mnyika yanayotaka hati hiyo ifutwe kwasababu ina makosa ya kisheria yanayosababisha wadaiwa ambao ni Mnyika, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo washindwe kuandaa utetezi wao.

Hati hiyo ya madai iliyofanyiwa marekebisho na Ng’umbi iliwasilishwa mahakamani hapo kufuatia amri ya Jaji Msuya aliyoitoa Julai 18 mwaka huu, ya kuleta mabadiliko hayo baada ya lalamiko la mlalamikaji la awali kupingwa na Mnyika.

Baada ya kuwasilishwa kwa hati hiyo iliyofanyiwa marekebisho, Mnyika anayetetewa na wakili Edson Mbogoro naye aliwasilishwa mapingamizi yake yanayotaka mahakama hiyo iifute hati hiyo kwasababu katika marekebisho ya hati hiyo, mlalamikaji ameendelea kujitoa malalamiko ya jumla yenye utata, yasiyojibika na yenye mkanganyiko kisheria hali inayofanya mdaiwa hawezi kujitetea dhidi ya madai yanayomkabili.

“Katika hati yake ya madai, mlalamikiaji anadai hukiukukwaji wa sheria, Kanuni na taratibu za uchaguzi ulifanywa na mimi wakati wa kampeni za uchaguzi ,pamoja na mambo mengine …kwa makosa hayo makubwa ya kisheria ambayo ni mdaiwa mwenyewe amekiri kuwa hati yake inadosari tunaomba mahakama hii itoea amri ya kuifuta hati hiyo ili mahakama iendelee na taratibu nyingine”alidai Mnyika.

Miongoni mwa madai katika kesi ya msingi ,Ng’umbi aliyoifungua Novemba mwaka jana,anadai Mnyika na au wasaidizi na mashabiki wake walifanya vitendo ambavyo ni ukiukwaji wa sheria kwa makusudi kwa madhumuni ya kushinda uchaguzi na kwamba kaisis wa Kanisa Katoliki Saranga Oktoba 3 mwaka jana aliwashawishi wahumini kupigia kura Mnyikka na kuwataka wasipigie kura CCM kwa kuwa ni chama cha Mafisadi.

Na kwamba Mnyika mara kadhaa alitumia barua ya TANROADS, ya Machi 30 mwaka 2010 iliyotumwa kwa CCM kuwadanganya wakazi wa KImara kwamba nyumba zao zitabolewa kama watamchagua Ng’umbi na kwamba Mnyika aliwanunulia pombe na kuwalipa sh 20,000 wananchi wa Kimara Saranga hili wampigie kura.
Hata hivyo Jaji Msuya alisema uamuzi wa maombi hayo atautoa Septemba 27 mwaka huu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Septemba 21 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.