Header Ads

KESI YA 'HASSANOO' YAPIGWA KALENDA

Na Happiness Katabazi
KESI ya kula njama na kuiba tani 26 za Shaba zenye thamani ya Sh milioni 400 mali ya kampuni ya Liberty Express Ltd ya Dar es Salaam inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Hassan Othman ‘Hassanoo’ na wenzake watatu,jana ilitajwa na kuairishwa mahakamani hapo.


Wakili wa Serikali Komanya mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa alieleza mahakama kuwa kesi hiyo jana ilikuja kwaajili ya kutajwa na kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kwamba wanaomba iairishwe hadi tarehe nyingine ili siku hiyo waje kuona kama upelelezi umekamilika.

Ombi hilo lilikubaliwa na Hakimu Nongwa ambaye aliairisha hadi Oktoba 12 mwaka huu,ambapo mahakama itakuja kuona kama upelelezi wa shauri hilo kama umekamilika.

Septemba 2 mwaka huu, mawakili wa serikali Andrew Rugarabamu na Aneth Kaganda,walidai mbele mahakamani hapo kuwa Agosti 26, mwaka huu ,maeneo ya Bahari Beach jijini Dar es Salaam, washitakiwa walikula njama na kuiba mali hiyo kwenye gari namba T 821 BCL iliyokuwa inasafirishwa kwenda Zambia.

Wakili Rugarabamu alidai katika kosa la nne, washitakiwa hao wanadaiwa kupokea tani hizo za shaba kinyume cha sheria huku wakijua wazi mali hiyo iliibwa
Mbali na Hassanor washtakiwa wengine ni Wambura Kisiroti (32), Najim Msenga (50) na Salim Shekibula (29) ambao wanatetewa na wakili wa kujitegemea Majura Magafu.

Chanz:Gazeti la Tanzania Daima la Septemba 21 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.