Header Ads

JAJI AKWAMISHA UAMUZI KESI YA MBATI VS MDEE

Na Happiness Katabazi
JAJI wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam John Utamwa , jana ilishindwa kutoa uamuzi wa ama hati ya madai katika kesi ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 iliyofunguliwa na aliyekuwa Mgombea Ubunge(NCCR-Mageuzi) dhidi ya mbunge Jimbo hilo Halima Mdee(Chadema) ifanyiwe marekebisho au la kwa maelezo kuwa bado hajakamilisha kuandaa uamuzi huo.


Wakili wa Mbatia, Mohamed Tibanyendera aliikumbusha mahakama hiyo kuwa jana kesi hiyo ilikuja kwaajili ya mahakama kutoa uamuzi huo na kwamba pande zote mbili zipo tayari kwaajili ya kupokea uamuzi huo.

Hata hivyo kwa upande wake Jaji Utamwa alisema hataweza kutoa uamuzi huo jana kwasababu bado hajamaliza kuandaa uamuzi huo hivyo akaiarisha kesi hiyo ya uchaguzi hadi Septemba 29 mwaka huu, ambapo atakuja kuitolea uamuzi.

Hatua hiyo ya mahakama kutaka kutoa uamuzi kuhusu hati hiyo ya madai, kunafuatia pingamizi lilowasilishwa na wakili wa Mdee, Edson Mbogoro la kuiomba mahakama hiyo imwamuru mlalamikaji aifanyie marekebisho hati yake ya madai na kuyaondoa baadhi ya madai ambayo Mbatia anadai kuwa katika mikutano ya kampeni Mdee alimwita yeye kuwa ni Fataki anayefanya mapenzi na watoto wa shule, kibaraka wa CCM na kila wiki analipwa sh milioni 80 na CCM hivyo kuwataka wapiga kura wa jimbo la Kawe wasimchague Mbatia.

Mdee anadai tuhuma hizo zilizoelekezwa kwake na Mbatia ndani ya hati hiyo ya madai zinamletea kinamkera na hataweza kuziandalia utetetezi na kusisitiza kwa kuomba mahakama hiyo imwamuru Mbatia aondee hizo tuhuma kwenye hiyo hati ya madai.

Novemba 25 mwaka 2010 Mbatia alifungua kesi ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo hilo ambayo yalimtangaza Halima Mdee(CHADEMA) kuwa ndiye aliyeshinda na ataliongoza jimbo hilo kwa kipindi cha miaka mitano.

Chanzo:Chazeti la Tanzania Daima la Septemba 22 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.