Header Ads

MNYIKA AMTOA JASHO NG'UMBI KORTINI

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeyakataa maombi ya aliyekuwa mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo(CCM), Hawa Ng’umbi yaliyokuwa yanaiomba mahakama itamke kuwa mbunge wa sasa wa jimbo hilo John Mnyika(Chadema) alijihusisha na vitendo vya uvunjifu wa sheria za uchaguzi wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.


Sambamba na uamuzi huo, Jaji Msuya alisema anamshangaa mlalamikaji(Ng’umbi) kwa kushindwa kwake kuyaondoa mapungufu hayo mapema hadi muda mrefu umepita sasa ndiyo mahakama inakuja kuyabaini mapungufu hayo jana.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Upendo Msuya wakati akitoa uamuzi wa kesi hiyo ya uchaguzi ambapo pia alisema anatupilia mbali ombi la mlalamikaji lilokuwa likiomba mahakama hiyo itamke kuwa matokeo yaliyomtangaza Mnyika ambaye jana alikuwepo mahakamani hapo kuwa mbunge hayakuwa halali.

Pia Jaji Msuya alitupilia mbali pingamizi la Ng’umbi liloomba mahakama itoe amri ya kumzuia Mnyika kushiriki uchaguzi wowote na lile liloomba mahakama hiyo itoe amri ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo wa huru na haki katika jimbo la Ubungo kwasababu amebaini maombi hayo hayanamsingi.

Jaji Msuya alisema amefikia uamuzi huo baada ya kukubaliana na hoja za wakili wa Mnyika (Edson Mbogoro) kuwa hati ya madai iliyofanyiwa marekebisho ina makosa kwani kuna baadhi ya haya hazifafanui tuhuma anazotuhumiwa na mdaiwa hali inayosababisha yeye kushindwa kuaanda utetezi wake.

“Baada ya kusikiliza hoja za pande zote mbili, nakubaliana na hoja za wakili wa mdaiwa(Mbogoro) kuwa hati ya madai haifafanui kwa uwazi tuhuma zinazomkabili mdaiwa hali ambayo imesababisha mahakama hii ione hati hiyo ina mapufungu na inaamuru hati hiyo iondolewe na ikafanyiwe marekebisho na kisha irejeshwe mahakamani hapa ndani ya siku 14 kuanzia leo”alisema Jaji Msuya.

Aidha Jaji Msuya alimtaka Ng’umbi aakikishe hati mpya atakayokuwa ameifanyia marekebisho aakishe anaifafanua kwa mapana tuhuma anayodai kuwa Tume ya Uchaguzi(NEC) ilishindwa kutimiza majukumu yake kwa mujibu wa sheria na kuwa akikishe analeta ufafanuzi kuhusu tuhuma alizomtuhumu Mnyika kuwa alitumia mikutano yake ya kampeni kumchafua kuwa yeye ni fisadi kwani aliuza nyumba za Jumuiya ya Umoja wa Wanawake(UWT).

Hata hivyo Jaji Msuya alimwamuru Ng’umbi awasilishe hati mpya iliyofanyiwa marekebisho mahakamani hapo Oktoba 11 , na wadaiwa wajibu Oktoba 25 na kesi hiyo itakuja kwaajili ya kutajwa Novemba mosi mwaka huu.
Agosti mwaka huu, wakili wa Mbogoro aliwasilisha mapingamizi yake yanayotaka mahakama hiyo iifute hati hiyo kwasababu katika marekebisho ya hati hiyo, mlalamikaji ameendelea kujitoa malalamiko ya jumla yenye utata, yasiyojibika na yenye mkanganyiko kisheria hali inayofanya mdaiwa hawezi kujitetea dhidi ya madai yanayomkabili.

Miongoni mwa madai katika kesi ya msingi ,Ng’umbi aliyoifungua Novemba mwaka jana,anadai Mnyika na au wasaidizi na mashabiki wake walifanya vitendo ambavyo ni ukiukwaji wa sheria kwa makusudi kwa madhumuni ya kushinda uchaguzi na kwamba kaisis wa Kanisa Katoliki Saranga Oktoba 3 mwaka jana aliwashawishi wahumini kupigia kura Mnyika na kuwataka wasipigie kura CCM kwa kuwa ni chama cha Mafisadi na Jaji Msuya alifuta dai hilo kwasababu haliwataji kwa majina viongozi wa makanisa hayo.

Na kwamba Mnyika mara kadhaa alitumia barua ya TANROADS, ya Machi 30 mwaka 2010 iliyotumwa kwa CCM kuwadanganya wakazi wa Kimara kwamba nyumba zao zitabolewa kama watamchagua Ng’umbi na kwamba Mnyika aliwanunulia pombe na kuwalipa sh 20,000 wananchi wa Kimara Saranga hili wampigie kura.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Septemba 28 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.