Header Ads

KESI YA MAHALU YAPIGWA KALENDA

Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilishindwa kuendelea kusikiliza kesi ya uhujumu wa uchumi wa Euro zaidi ya milioni mbili inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Grace Martin kwasababu wakili wa washtakiwa hao Mabere Marando amefiwa na ndugu yake.


Kesi hiyo ambayo ilikuja jana kwaajili ya Profesa Mahalu kuendelea kujitetea lakini Kiongozi wa jopo la mawakili wa Mahalu, Marando mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi Mfawidhi Elvin Mugeta aliomba mahakama hiyo jana iairishe usikilizwaji wa kesi hiyo kwasababu amefiwa na ndugu yake na kwamba yeye ndiyo kiongozi wa msiba huyo.

Ombi hilo lilikubaliwa na Hakimu Mugeta na wakili wa serikali Ponsian Lukosi ambapo hakimu huyo aliairisha kesi hiyo hadi Septemba 26 ambapo kesi hiyo itakuja kwaajili ya kutajwa na Oktoba 18,19 na 20 mwaka huu, kesi hiyo itakuja kwaajili ya kuendelea kusikilizwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Agosti 27 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.