Header Ads

MWENENDO KESI YA MRAMBA WAKAMILIKA

Na Happiness Katabazi
HATIMAYE Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, imesema kuwa mwenendo wa kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya Sh bilinioni 11.7 inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba na wenzake umeishachapwa na hivi sasa unafanyiwa uhakiki na jopo la mahakimu wanaoisikiliza.


Hayo yalisemwa jana na Hakimu Mkazi Frank Moshi wakati kesi hiyo ilipokuja jana kwaajili ya kutajwa na kuangalia kama mwenendo huo wa kesi umeishakamilika ili pande zote katika kesi hizo uwe kupatiwa kwaajili ya kwenda kujiaanda na majumuisho ya kuwaona washtakiwa wanakesi ya kujibu au la.

Hakimu Moshi alisema taarifa alizopewa ni kwamba tayari mwenendo huo umeishachapwa na kwamba kinachofanywa na mahakimu wanaosikiliza kesi hiyo ni kuuhakiki mwenendo huo na kusema kuwa anaairisha kesi hiyo hadi Oktoba 5 mwaka huu, ambapo siku hiyo uhakiki utakuwa umeishakamilika nakala za mwenendo huo wa kesi utatolewa kwa pande zote.

Mbali na Mramba washtakiwa wengine ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona na Katibu Mkuu Mstaafu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Gray Mgonjwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania la Jumanne, Septemba 6 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.