Header Ads

MASAWE,BENDERA WAPONGEZWA NA WADAU WA MICHEZO

Na Happiness Katabazi
CLUB ya Tanzania Youth Athletics yenye maskani yake Holili Mkoani Kilimanjaro imempongeza Mkuu mkoa wa Kagera Mteule, Kanali Mstaafu, Fabiani Masawe kwa kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete juzi kushika wadhifa huo.


Akizungumza na gazeti hilo kwa njia ya simu jana Mwenyekiti wa Club hiyo, Dominic Rwezaula na Nahodha wa timu Nelson Brighton alisema kwaniaba ya klabu yake ambayo imeanzishwa kwaajili ya kuinua vipaji vya riadha mkoa wa Kagera anampongeza Masawe ambaye awali alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Karagwe kwa kuteuliwa kwake juzi na Rais Kikwete kuwa mkuu wa Mkoa wa Kagera.

“Pongezi hizi zinatokana na Masawe mwenye kuwa ni mdau sana wa michezo na kuamini club ya riadha iliyoanzishwa itaendelezwa na kuibua vipaji vyavya riadha mkoa wa Kagera na tunaimani chini ya wadhifa wake mpya wa ukuu wa mkoa huo ,ataiendeleza michezo sambamba na kuwaunganisha wakazi wa mkoa huo kwaajili ya kujiletea maendeleo”alisema Rwezaula.

Wakati huo huo wadau mbalimbali wamepongeza hatua ya Rais Kikwete kumteua Joel Bendera kuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwasababu Bendera naye ni mdau wa sekta ya michezo hapa nchini na waimani kuwa atakapokuwa Morogoro pia ataweza kukukuza michezo katika mikoa hiyo na kwamba wamefurahishwa kwa hatua hiyo ya rais Kikwete kuwateua wakuu wa mikoa ambao ni wadau wakubwa wa michezo.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Septemba 16 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.