Header Ads

MAKALLA awasaidia wanake Mvomero

Na Mwandishi Wetu, Mvomero
MBUNGE wa Jimbo la Mvomero Amos Makalla amekisaidia kikundi cha akinamama mshikamano group shingi milioni moja kwa ajili ya kukuza mtaji wa shughuli za uzalishaji mali.

Msaada huo umekabidhiwa juzi kwa kiongozi wa mshikamano group Bi Mariam Mdabwa ambaye alimshukuru sana mbunge kwa utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoa hivi karibuni baada ya kikundi kumsomea risala ya kuomba msaada huo“ndugu wana kikundi mmeona?wananchi mmeona?sh milioni moja na laki tano hizi hapa,makalla ni mkweli si mbabaishaji kama wanasiasa wengine yeye anatoa cash hatoi cheki feki”alisema bi mariam.

Kwa upande wake makalla aliwataka wanakikundi kutumia msaada huo kukuza mtaji na shughuli za uzalishaji mali“jamani hii ni mbegu ipandeni izae.

Aidha amewapongeza wanakikundi kwa kuanzisha kikundi na amewataka makundi mengine kuiga mfano wa mshikamano group na akawaakumbusha kuwa umoja ni nguvu utengeno ni udhaifu.“Ndugu zangu taasisi za fedha zinapenda kusaidia vikundi hivyo tukiungana ni rahisi taasisi hizo zinapotoa mikopo zaweza kutusaidia na sisi tulioungana”.

No comments:

Powered by Blogger.