Header Ads

KATIBU BAKWATA AMRUKA PONDA





Na Happiness Katabazi

KATIBU Mkuu wa Baraza la Kuu la Waislamu(BAKWATA), Suleman Said Lolila(61),amekanusha madai yaliyotolewa na  Katibu wa  Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49 wanaokabiliwa na kesi  uchochezi na wizi wa Sh milioni 59  katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kuwa Baraza Kuu la Waislamu nchini(BAKWATA), siyo chombo cha kuwakilisha waislamu wote hapa nchini.

Sambamba na waandishi wa habari  za mahakamani walipongeza hatua iliyochukuliwa na wana usalama ya jana kuzuia umati wa wafuasi wa Ponda kuingia ndani ya chumba kinachoendeshewa kesi kwani hapo awali wafuasi hao walikuwa wakifurika hali iliyosababisha waandishi wa habari,wanausalama kushindwa kufanyakazi yao kwa nafasi na kupata hewa ya kutosha kwani kesi hiyo kwanza ina washtakiwa wengi  ambao ni 50.
Suleiman ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa jamhuri katika kesi hiyo, alitoa maelezo hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Victoria Nongwa wakati akiongozwa na wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka kumuongoza kutoa ushahidi ambapo jana shahidi huyo alimaliza kutoa ushahidi wake.
Itakumbukwa kuwa Novemba 15 mwaka huu, wakili Mwandamizi wa Serikali Tumaini Kweka aliwasomea maelezo ya awali washtakiwa hao ambapo alidai Bakwata ni chombo ambacho kinawawakilisha waislamu wote, lakini Ponda na wenzake walikanusha madai yao na kusema kuwa Bakwata haipo kwaajili ya kuwawakilisha waislamu wote.
Suleiman alitoa maelezo hayo baada ya kuulizwa swali na wakili Kweka kuwa BAKWATA ni chombo gani?kipo kwaajii ya waumini wa dini gani?Mali za waislamu zinamilikiwa na nani kwa niaba yao?Na na ninani hivi sasa ni mmilikiwa wa kiwanja  kiwanja Kitalu 311/3/4 Block  T ,kilichopo eneo la Chang’ombe Markas jijini Dar es Salaam?
Akijibu maswali hayo shahidi huyo ambaye alidai yeye ndiye mtendaji mkuu wa BAKWATA alieleza kama ifuatavyo:
“BAKWATA ni chombo kilichoundwa kwa Korani  na Sunaa na imesajiliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani, na Bakwata ni chombo kilichoanzishwa kwa kwaajili ya kuwawakilisha waumini wa dini ya Kiislamu hapa nchini  na mali za waislamu zinamilikiwa kwa niaba yao na Bodi ya Wadhamini ya Bakwata ;
“Na mmiliki halali wa kiwanja hicho hivi sasa ni kampuni ya Agritanza Ltd , kwani Serikali ya Misri ilitoa wazo ya kuwasaidia waislamu wa Tanzania kielimu na ikafanya mazungumzo na viongozi wa serikali ya Tanzania ,serikali ya Tanzania ikaipatia serikali ya Misri eneo hilo la Chang’ombe Markas kiwanja hicho ili kiweze kujenga chuo kikuu cha Waislamu lakini baadaye serikali ikaja kuwagawai baadhi ya maeneo taasisi ya YCC na mfanyabashara Yusuf Manji:

“Ikabakia eneo jingine ambalo mwisho wa siku BAKWATA ikiaamua eneo hilo wabadilishane na kampuni ya Agritanza Ltd kwa mikataba halali kisheria , hivyo makubaliano yalifikishwa tena kwa maandishi BAKWATA ikaridhia kubadilisha na kampuni hiyo hivyo Agritanza hivi sasa ndiye mmiliki halali wa kiwanja hicho na si vinginevyo na alipata Baraka zote za Bakwata ambayo ni chombo kinachosimamia mali na waislamu wote’alidai shahidi huyo.

Kwa upande wake wakili utetezi Nassor Mansoor akimhoji shahidi huyo alimuuliza kama  anafahamu  alikuwa akifahamu hati ya umiliki wa kwanza wa kiwanja hicho ulikuwa ukimilikiwa na nani na kwamba kabla ya kiwanja hicho kugawiwa kwa baadhi ya watu kilikuwa na ukubwa gani na kwamba kama alikuwa akiwafahamu washtakiwa .
Akijibu maswali hayo alidai yeye hafahamu awali kiwanja hicho kilikuwa kikimilikiwa na nani na kilikuwa na ukubwa gani na kuhusu kuwafahamu washtakiwa alidai anamfahamu Sheikh Ponda kwani amekuwa akimuona kupitia vyombo vya habari na kisha shahidi huyo akainuka akawasalimia washtakiwa na kusema “Asalmayek nao washtakiwa wakamjibu kwa sauti Alykmsalamu hali iliyosababisha Hakimu Mkazi Victoria Nongwa kumwaleza shahidi kuwa mahakamani hapo watu huwa hawasalimiani na kusababisha watu kuangua vicheko.

Baada ya Shahidi huyo kumaliza kutoa ushahidi wake, Hakimu Nongwa alisema anaiarisha kesi hiyo hadi Desemba 13 mwaka huu, itakapokuja kwaajili ya shahidi wa pili kuja kuanza kutoa ushahidi wake na akamuamuru mshtakiwa wa kwanza Ponda na Mukadam Abdal Swalehe(45) ambaye ni mshtakiwa wa   tano katika kesi hiyo ya jinai Na.245/2012 warudishwe gerezani kwasababu bado Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi hajaiondoa hati yake aliyoiwasilisha   ambayo  imefunga dhamana za washtakiwa hao wawili.

Baada ya hakimu Nongwa kuarisha kesi hiyo, ndugu na jamaa na washtakiwa ambao wapo nje kwa dhamana walijipanga katika viunga vya mahakama hiyo na kumpungia mkono Mukadam na Ponda ambao walikuwa wamepandishwa kwenye gazeti la Jeshi la Magereza lilokuwa likilindwa na kuongozwa na msafara wa magari ya ina ya  Defenda za jeshi la Polisi na gari mmoja lililokuwa limebebeba maji ya kuwasha ‘kikojozi’ na kuanza safari ya kumrejesha katika gereza la Segerea na wafuasi hao ambao kadri siku zinavyozidi kusonga mbele wanapungua kuja mahakamani kuudhulia kesi hiyo walisikika wakisema ‘Takbiri,Takbir’ huku wakiwapungia mkono Ponda na Mukadam ambao walikuwa wakiondoshwa kwenye eneo hilo la Mahakama kupelekwa gereza  la Segerea.

Awali Oktoba 18 mwaka huu, ilidaiwa na wakili Kweka kuwa kosa la kwanza alidai ni la kula njama ambalo linawakabili washitakiwa wote,kosa la pili ni kwaajili ya washitakiwa wote ambalo ni la  kuingia kwa nguvu  kwa nia ya kutenda kosa kinyume na kifungu cha  85 na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002, kuwa Oktoba 12 mwaka huu huko Chang’ombe Markas, wasipokuwa na sababu za msingi waliingia kwa jinai kwenye kiwanja kinachomilikiwa na kampuni ya Agritanza Ltd, kujimilikisha kiwanja hicho kwa njia ya iloyopelekea uvunjifu wa amani,wizi ambapo baada ya kuvamia waliiba vifaa na malighafi ikiwemo nondo, kokoto zenye jumla ya thamani ya Sh. 59,650,000 mali ya kampuni ya Agritanza na kosa la tano ni la uchochezi kinyume na kifungu cha 390 na 35 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, ambalo sasa kosa hili la uchochezi litamkabili Mukadamu na Ponda peke yao  kuwa wakiwa ni viongozi wa jumuiya hiyo , Oktoba 12 mwaka huu ,waliwashawishi wafuasi wao watende makosa hayo hata hivyo walikanusha mashtaka yote.

 Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Novemba 30 mwaka 2012

   

6 comments:

Anonymous said...

If yοu ωish for tο obtain a grеat deal from
this ρiece of writing then you have tо аρplу suсh strategies to your
ωοn weblοg.http://greysanatomyѕ9e7hԁfrеe.

educatοграges.com
My web site :: Grey's Anatomy Season 9 Episode 7 I Was Made For Lovin You

Anonymous said...

Good info. Lucky mе I fοund your site by accіdent (stumblеupon).
I've book-marked it for later!Watch Beauty and the Beast Season 1 Episode 7
Here is my blog ... Watch Beauty and the Beast Season 1 Episode 7

Anonymous said...

Undеniably belіeve thаt whіch уou
said. Your favorite reason seemed to be on the internet the simplest thing
to be aware of. I ѕay to you, I certainly get annoyеd ωhile peoplе think about worrіes thаt thеy juѕt don't know about. You managed to hit the nail upon the top and also defined out the whole thing without having side-effects , people could take a signal. Will likely be back to get more. ThanksLast Resort Season 1 Episode 8
my site > Last Resort Season 1 Episode 8

Anonymous said...

Ні thегe, just becаme awarе οf your blog through
Google, anԁ founԁ thаt іt is trulу іnfοrmativе.
I am going to ωatсh out for bгusselѕ.
I will bе grateful if you continue this in futurе.

A lot of people will bе benefiteԁ from уouг wrіting.
Cheеrs!Glee Season 4 Episode 8 Free Stream
my site :: Glee Season 4 Episode 8 Free Stream

Anonymous said...

After checkіng out a hаndful of the blog ρosts оn your web page, I tгuly appreciate your ωаy of writing a blog.
ӏ bοoκ-markеd it tο my bookmaгk site
list and will be chеckіng back soоn. Please νisit my ωeb ѕite too
and lеt me know what you think.http://thebigbangtheorys6e9hdfr.
eԁucatorpagеs.com
Here is my weblog - The Big Bang Theory Season 6 Episode 9

Anonymous said...

Heya just wanted to give yоu a quicκ headѕ
up and let yоu knoω a fеw of the ρicturеs aren't loading correctly. I'm
not ѕure why but I think its a linκing
iѕsue. I've tried it in two different web browsers and both show the same results.http://jerseyshores6e10hdfree.educatorpages.com
Also see my website :: Watch Jersey Shore Season 6 Episode 10 Shore Shower Online Free Stream

Powered by Blogger.