Header Ads

DPP AMCHELEWESHA ZOMBE



Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana ilijikuta ikishindwa kuanza kusikiliza ombi la kuomba kuomba kuongezewa muda wa kukata rufaa lililowasilishwa na Mkurugenzi wa Mashitaka(DPP), Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam, Abdallah Zombe na wenzake kwasababu DPP halikuwa hajaupatia upande wa utetezi nakala ya ombi hilo.

Jaji Alocye Mujulisi  alisema shauri ilo lilikuja jana mbele yake kwaajili ya kuanza kusikiliza ombi hilo la DPP, lakini mahakama yake inalazimika kualisha usikilizwaji wa shauri hilo kwasababu mawakili wa upande wa utetezi wanaoongozwa na wakili wa kujitegemea Richard Rweyongeza waliomba shauri hilo lisikilizwe  kwasababu upande wa jamhuri jana  ulikuwa haujaupatia nyaraka hiyo upande wa utetezi na hivyo kusababisha mawakili wa utetezi kushindwa kujiandaa.

“Kwa sababu hiyo naairisha usikilizwa wa ombi hili la DPP hadi Septemba 5 mwaka huu, na ninaamuru upande wa jamhuri uwapatie nyaraka hiyo upande wa utetezi  na upande wa utezi ujibu  kisha tukutane hapa tarehe hiyo kwaajlili ya usikilizwaji wa ombi hili “alisema Jaji Mujulisi.

Mei 8 mwaka huu, Mahakama ya Rufani nchini iliifuta  rufaa  iliyokuwa imekatwa na DPP ya kupinga hukumu ya kesi ya mauji ya  Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam,iliyomwachilia huru  Zombe na wenzake baada ya kubaini kuwepo kwa dosari katika hati ya kukatia rufaa hiyo.

Uamuzi huo ulitolewa jana na jopo la majaji wa tatu  Edward Rutakangwa,Mbarouk Mbarouk na  Bethek Mila.Uamuzi huo ulitokana  na jopo hilo Aprili 22 mwaka huu, iliposhindwa kuanza kusikiliza rufaa hiyo Na.254/2009  baada ya jopo hilo kubaini dosari katika hati hiyo   ambapo mawakili wa mwomba rufaa Timon Vitalis na Richard Rweyongeza walikiri dosari hiyo na wakaiomba mahakama iwapatie muda wa kwenda kuifanyia marekebisho hati hiyo ya kukatia rufaa.

Jaji Mbarouk siku hiyo ndiyo aliyeibaini dosari hiyo ambayo dosari yenyewe ni kwamba katika hati ya kukataa rufaa, DPP alisema anapinga hukumu ya kesi ya mauji Na. 26/2006 iliyokuwa ikimkabili Zombe na wenzake kuwa ilitolewa na Jaji wa Mahakama ya Rufaa Salum Massati. Wakati DPP alipaswa kuandika Jaji Salum Massati ambaye wakati akisikiliza kesi hiyo alikuwa  ni  Jaji wa Mahakama Kuu  na wakati akiendelea kusikiliza kesi hiyo aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufaa , hivyo DPP katika hati yake ya kukata rufaa alipaswa amtambulishe kuwa hukumu ile ilitolewa na Jaji wa Mahakama Kuu Massati na siyo jaji wa mahakama ya rufaa.

Akitoa uamuzi huo, jopo hilo lilisema kuwa ibara ya  119 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inasomeka kama ifuatavyo:

“Jaji yoyote  wa Mahahakama ya Rufani hatakuwa na mamlaka  ya kusikiliza shauri lolote katika Mahakama Kuu  au katika mahakama ya hakimu  ya ngazi yoyote.:
“Isipokuwa kwamba iwapo jaji yeyote wa mahakama kuu atateuliwa  kuwa Jaji Mahakama ya rufaa, basi hata baaa ya kuteuliwa kwake kuwa jaji wa mahakama ya rufani,jaji huyo  aweza kuendelea kufanyakazi kazi zake katika mahakama kuu mpaka amalize  kutayarisha  na kutoa hukumu  au mpaka akamilishe shughuli nyingine yoyote  inayohusika na mashauri  ambayo yalikwisha anza kuyasikiliza kabla kabla  hajateuliwa  kuwa jaji  wa mahakama rufani, na kwamba ajili hivyo itakuwa  halali kwake  kutoa hukumu  au uamuzi  mwingine wowote unaohusika kwa kutumia  kutumia au  kutaja madaraka  aliyoshika kabla  ya kutueliwa  kuwa jaji wa mahakama ya rufani,  lakini endapo hatimaye hukumu hiyo au uamuzi  mwingine utapingwa kwa njia  ya rufaa itayofikishwa mbele ya  mahakama ya rufani,basi katika hali  hiyo jaji  huyo  wa mahakama ya rufani,hatakuwa  na mamlakaya kusikiliza  rufaa hiyo:inasomeka ibara hiyo.

Jaji Rutakangwa alisema kwa mujibu wa matakwa ya ibara hiyo, na kwakuwa wakili Vitalis alikiri dosari hiyo, mahakama yake imefikia uamuzi wa kuona hati ya rufaa ina dosari na kwa dosari hiyo mahakama yake imeona hakuna rufaa mbele yake na hivyo imefikia uamuzi wa kuifuta ombi hilo la rufaa iliyofunguliwa na DPP dhidi ya Zombe na wenzake.

Aidha jopo hilo lilisema  mahakama yake inatoa fursa kwa DPP kuwasilisha ombi la ukomo wa muda Mahakama Kuu wa kuomba waongezewe muda wa kukata rufaa upya kama wataona wana haja ya kufanya hivyo.
Baada ya uamuzi huo wa mahakama ya rufaa kutolewa ndio DPP aliwasilisha Mahakama Kuu ombi hilo ambalo jana lilishindwa kuanza kusikilizwa.
Agosti 17  mwaka 2009, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilitoa hukumu ya kihistoria ya kesi ya mauji ya watu wanne iliyokuwa ikimkabili Zombe na wenzake ambapo jaji Salum Massati ambaye hivi sasa ni jaji wa mahakama ya rufani aliwaachilia huru Zombe na wenzake ambao walikuwa wakikabiliwa na kesi hiyo kwa maelezo kuwa upande wa jamhuri ulishindwa kuleta ushahidi mzuri ambao ungewea kuishawishi mahakama hiyo iwaone washtakiwa hao wana hatia.


Baada ya hukumu hiyo ya mahakama kuu, DPP hakulidhishwa na hukumu hiyo Oktoba 7 mwaka 2009 akakata rufaa Mahakama ya Rufaa ,  kupinga hukumu hiyo ambayo kwa mujibu wa ratiba ya vikao vya mahakama ya rufaa,rufaa hiyo ilikuwa imepangwa kuanza kusikilizwa jana lakini ikashindikana.

Mbali na Zombe, washitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Christopher Bageni, Ahmed Makele, WP 4593 PC Jane Andrew, D 1406 Koplo Emmanuel Mabula, D 8289 DC Michael Shonza, D. 2300 Abeneth Saro, D.4656D/Koplo Rajabu Bakari na D.1317D/XP Festus Gwasabi na jana washtakiwa wote walifika mahakamani hapo.

Washitakiwa hao walidaiwa kuwa Januari 14, mwaka 2006 waliwaua wafanyabiashara watatu wa madini wa wilayani Ulanga, mkoani Morogoro; Ephraim Chigumbi, Sabinus Chigumbi na Mathias Lukombe pamoja na dereva teski Juma Ndugu, mkazi wa Dar es Salaam kwa madai kuwa walikuwa majambazi.
Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Agosti 30 mwaka 2013




No comments:

Powered by Blogger.